Mhudumu wa Mochuari "amchimba mkwara" waziri

Mhudumu wa Mochuari "amchimba mkwara" waziri

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,204
Reaction score
162,774
Mhudumu wa kitengo cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Rufaa Mbeya,Eugene Vurugu amemtishia naibu waziri wa afya,Dr.Saif Rashid kuwa ikitokea amefariki akiwa mkoani Mbeya,basi maiti yake italazwa sakafuni kutokana na uhaba wa majokufu ya kuhifadhi maiti katika kitengo hicho.

Mhudumu huyo alisema kitengo hicho kina majokofu sita na hulazimika kuhifadhi maiti kwa zamu ili angalau maiti zisiharibike.

"Hata wewe Waziri ukifa leo,hakuna pa kukuweka.Utawekwa sakafuni kusubiri maiti nyingine zipoe halafu utaingizwa ndani kwa kuingizwa maiti mbili kwenye eneo la mtu mmoja"alisema Vurugu.

CHANZO:Mwananchi

MY TAKE:
Mfanyakazi huyu atasalimika kweli kwa kumwambia waziri ukweli huu hadharani?

Huyu mtumishi anastahili kupandishwa cheo kwa ujasiri wake wa kutetea mazingira mazuri ya kazi.
 
Hawa watu (wahudumu wa mortuary) huwa vichwa vyao havipo vizuri. They care less!! Wana-guts sana!

Sent from my BlackBerry 9810 using JamiiForums
 
Kabla hujauliza swali jiulize hivi: Waziri Juma Akukweti alifiaje Mbeya?

Akukweti hakufia Mbeya wewe! mimi mwenyewe nilikuwa shuhuda wa ile ajali.
mh aliungua sana kwa mafuta ya ndege hasa sehemu za tumbo mpaka kwenye mgegedo!
mimi ndo alinitajia namba za mke wake kwa taabu nimpigie mkewe kumpa taarifa!
back to the topic;
huyo attendant yupo sahihi kabisa lakn kwakuwa serkali ya ccm siyo sikivu usishangae yakamtokea ya Steve Ulimboka!
 
kabla waziri hajafa, saa nyiingi kashaa vushwa mipaka! Chezea CCM wee! labda ikiwa ni ajali ya gari.
 
Safi sana hao jamaa huwa hawakopeshi.Kwanza hapo najua huyo waziri alitetemeka kimoyomoyo baada ya kuambiwa hivyo.Chezeya kifo weye!!!
 
kaongea ukweli lakini sababu watz tunadharau watampuuza kwavile anafanya kazi hiyo. kszi ni ngumu sana hats kukiwa na mazingira mazuri lakini yeye anaziwekea zam Haiti inamaana hana Mda was kupumzika hata ningekuwa mm ningesema kama wataningoa meno bac lakini ukweli wameupata
 
Kasahau wanafia India na Sauth Africa waziri afie Mbeya itakuwa maajabu alichotakiwa kufanya angembebesha maiti moja mgongoni angalau angejua uchungu
 
hata akifia mbeya watampeleka kwanza india kwa uhakika zaidi ndio waje wamzike mbeya
 
Namtambua vema muhudumu huyu.......anapga maji ile mbaya halaf kuna sku akaniomba bia pale central police nkamjibu sna hela akanambia .....utanikuta tu kwenye anga zangu... ukweli nlicheka sana
 
Back
Top Bottom