Mnyika ni Mbunge kijana na makini sana. Lakini zaidi sana, ni muungwana. Ukisoma hoja yake ameomba radhi kwa wana_ubingo na wafanyakazi kwa yeye binafsi kutokuwakilisha mapendekezo ya marekebisho juu ya suala hili lililopitishwa 'kinyemela'. Naomba ninukuu kutoka kwenye blog yake...
'Ikumbukwe kwamba kifungu cha kufuta mafao ya kujitoa kilichozua mgogoro hakikuwepo wakati muswada uliposomwa kwa mara ya kwanza bungeni tarehe 1 Februari 2012 bali kiliwasilishwa kupitia jedwali la marekebisho ya Wizara lililowasilishwa tarehe 13 Aprili 2012 bila malengo na madhumuni yake kuelezwa kwa ukamilifu.
Kupitishwa kwa kifungu hicho kumethibitisha maneno niliyoyatoa bungeni kuwa tumefika hapa tulipo kutokana na uzembe wa bunge na wabunge na kwa hili pamoja na mchango nilioutoa bungeni kwa maandishi siku hiyo juu ya haja ya kuwa mfumo mpana zaidi wa pensheni na hifadhi ya jamii (universal pension and social security) pamoja na kuwa sikuunga mkono kifungu husika kilichoingizwa kinyemela naomba radhi kwa wananchi wa Ubungo na wafanyakazi kwa kutokuwasilisha jedwali la marekebisho kupinga kifungu hicho kuingizwa.'
Pamoja na kwamba wabunge wote wana wajibu wa kutetea yale yaliyo na maslahi kwa wananchi, yeye amechukua dhamana na kukili kosa.
Sasa nirudi kwa mtoa mada..Umeongea vizuri kwa asilimia fulani lakini unakosea kwa shutuma na maneno makali dhidi ya Mnyika. Alichokisema Mnyika ndio mapenzi ya wafanyakazi walio wengi.
Ikumbukwe kuwa lengo kuu la mwanasiasa yeyote yule ni kuongoza/kutawala kama lilivyo lengo la chama chochote cha siasa ni kushika hatamu. Hii ndio elimu ya siasa ninayoifahamu na wanazuoni wa siasa watakubaliana nami. Sasa mwanasiasa anapofanya jambo lenye maslahi kwa wananchi wake anaowaongoza ni kwamba anakuwa anatimiza malengo yake. Tuache unafiki, huo ndio ukweli.
Sasa nirudi kwenye suala la mafao na kwani wafanyakazi wanaona bora wajitoe wakati unaporuhusu. Ukweli ni kwamba mfumo wa mafao Tanzania si mafao bali ni wizi mtupu. Narudia ni wizi mtupu. Najua humu kwenye jamvi watu wanapenda data, haya soma hapa: Old Age Pension
Natumia tu mfano uliotolewa na NSSF wenyewe. Mtu ambaye anawastani wa mshahara Tsh 360,000 aliyefanya kazi miaka 20 (240 months) akistaafu anapewa Lump Sum (mafao mkupuo) Tsh 3,240,000 halafu pensheni ya mwezi (Monthly Pension) Tsh 135,000.
Sasa kwa nini nasema wizi mtupu, mtu huyu kwa miaka 20 anakuwa ameweka akiba ya Tsh 17,800,000 (yaani 72,000 kila mwezi mara miezi 240). Sasa mtu aliyeweka akiba kiasi hicho unampa Tsh 3,240,000 na kila mwezi Tsh 135,000. Watu wanaojua hesabu twende pamoja..Hii inamaana itamchukua mtu miezi 104 kumaliza akiba yake sawa na miaka takribani 9 baada ya kustaafu. Sasa ni wangapi wanaishi kiaka 69?? Ijulikane hapa kwamba bado hapo unakula ela yako hamna riba!!! Huu ni mfano wa NSSF ambao kwangu mimi ndio mfuko kandamizi kuliko yote.
Formula ya PPF ni tofauti kidogo ila bado nayo ni kandamizi. Wenye muda wafuatilie:
:: PPF Pensions Fund ::-
Niseme tu, kwa mtu anayepata wastani wa mshahara Tsh 2,000,000 leo akistaafu, mafao ya mkupuo (Lump Sum) ni Tsh 62M kwa LAPF/PSPF; Tsh 14.4M kwa NSSF, na Tsh 22.5M kwa PPF wakati Pension ya mwezi (monthly pension) ni Tsh 333,333 LAPF/PSPF; 600,000 NSSF, na 450,000. Hii ni kama utakuwa umefanya kazi kwa miaka 15 ya vigezo (miezi 180) ambayo ni lazima. Kwa kipindi hizo, michango ya yako na mwajiri (20% kwa mwezi Tsh 400,000 kwa miezi 180) ni Tsh 72M. Hapa utaona mfuko wa kujiunga ni PSPF na LAPF.
Swali la mwisho, kama leo napata mshahara wa Tsh 2,000,000 na pension ya juu ya mwezi ninayoweza kupata ni Tsh 600,000, je ni kweli maisha yangu yatabaki vile vile? Tusijidanganye, kwa mfumo kwa kitanzania HAPANA. Kwa yeyote anayemfahau mstaafu ambaye anaishi maisha mazuri kwa pensheni amtaje. Wengi wanaoishi vizuri ni wale waliojiandaa na kuanzisha miradi kabla ya kustaafu.
Nimalizie kwa kusema, watanzania pia inabidi tuwatendee haki wanasiasa wa vyama vya upinzani. Mara nyingi tunawakumbuka wakati wa shida kama sasa tunasikia humu jukwaani watu wanauliza wabunge wa CHADEMA walikiwa wapi? Wakati wa mavuno tunawatosa! Hii sio sawa; sasa ndio hivyo tunakula jeuri yetu. Kama upinzani tunaona unatetea maslahi yetu basi tuwape nafasi na CCM wawe wapinzani ili wajifunze.
Suala la kulazimisha watu wasile chao mpaka miaka 55-60 halikubaliki!