Ninafuatilia bunge jioni hii SUGU amesema serikali ni ya wapumbavu, Kigwangala yeye kawaita wabunge wa CHADEMA wapuuzi kisa walikuwa wanamzomea,kwa kifupi wabunge wengi hawajadili hoja za msingi na badala yake wanajadili mambo ya vyama vyao ,bunge limejaa vijembe na upuuzi mwingine.
Kwa bunge letu hili tuna haki ya kuwa maskini milele.
Mkuu hapa dawa ni moja tu ya kutuondoa ktk huo umaskini wa milele, dawa hiyo ni kukikataa chama kinacho ongoza serikali yenye viongozi wasio na muono wa mbali, viongozi wasiokubali kukosolewa hata pale wanapokosea, viongozi waiokuwa tayari kuwajibika pale mamlaka zao zinapokosea, viongozi wa chukua chako mapema, viongozi wa elimu za kuunga unga.
Hapo mkuu ndo tutauacha umaskini tulionao.