Mh. Mbilinyi (Sugu) alipuka bungeni

Mh. Mbilinyi (Sugu) alipuka bungeni

Kigwangala naye anamwaga matusi...

Anasema kuwa wanaozomea wote ni wapuuzi...
 
Akichangia bungeni,mheshimiwa Joseph Mbilinyi 'sugu' amemchanachana Mwigulu kuwa ni mpumbavu,anafanya dili alafu anatumia m-pesa,akaendelea na waziri wa elimu Mulugo kuwa ana elimu ya kuungaunga na ni chenga tupu,akadai usalama wapo badala ya kumueleza rais kuwa jamaa huyo ni chenga tupu,wao wanakalia kuifuatilia Chadema na kung'oa watu kucha na meno. Pamoja na kukalishwa mara mbili na spika ili atumie lugha ya staha bado aliendelea na baada ya kumaliza kuna wabunge kadhaa walisikika wakitaka kutoa taarifa ila spika kawapotezea akamwita mchg.Natse aendelee kuchangia.
 
Kigwangala naye anachemka kishenzi...anasema kuwa serikali ispoacha upuuzi atachukua hatua mwenyewe...

Kwamba wanaandamana, wanaua watu na kung'oa kucha na meno...

Kama wataachwa yeye atahamasisha watu wa Nzega wawakamate na yeye atawashughulikia...

Amesema kuwa viongozi wote wa CHADEMA ni wapuuzi...

Na speaker hajaingilia kati...
hahaha,bunge la mwaka huu litakua tamu sana.kuanzia kesho tamthilia naweka pembeni ni bunge mwanzo mwisho.
 
Hoja yake imesaidia vipi kuboresha bajeti ya Waziri Mkuu?

Bunge sio Rock Concert, mbunge akiongea akimaliza inabidi kuwe na input alizoweka. Ukiona mbunge kamaliza halafu kinachojadili ni kwamba "kamchana Mwigulu" ujue kuna walakini.

Kwa kubainisha mojawapo ya chanzo kikubwa cha kuzorota kwa elimu. Waziri mwenye elimu ya kuungau-unga! next!
 
Kigwangala naye anachemka kishenzi...anasema kuwa serikali ispoacha upuuzi atachukua hatua mwenyewe...

Kwamba wanaandamana, wanaua watu na kung'oa kucha na meno...

Kama wataachwa yeye atahamasisha watu wa Nzega wawakamate na yeye atawashughulikia...

Amesema kuwa viongozi wote wa CHADEMA ni wapuuzi...

Na speaker hajaingilia kati...

Mkuu Speaker hana cha kufanya bali ana tekeleza maagizo ya mabosi wake.
 
Kigwangala naye anachemka kishenzi...anasema kuwa serikali ispoacha upuuzi atachukua hatua mwenyewe...

Kwamba wanaandamana, wanaua watu na kung'oa kucha na meno...

Kama wataachwa yeye atahamasisha watu wa Nzega wawakamate na yeye atawashughulikia...

Amesema kuwa viongozi wote wa CHADEMA ni wapuuzi...

Na speaker hajaingilia kati...
Sishangai. Kwao, viongozi wote wa CDM ni wapuuzi isipokuwa yule aliyempa Nchemba mkanda wa Lwakatare.
 
Nashauri wabunge wetu wazitumie dakika 5 vizuri wasiwe emotional! Waachane na Mwigulu hana maana!

Halafu huyu speaker anaendesha mambo kishabiki kabisa...

Sugu kasema serikali na akina Mwigulu ni wapumavu,

Na Kigwangala kasema CHADEMA ni wapuuzi...

Pamoja na Speaker kuingilia kati hotuba ya Mbilinyi, hakusema lolote wakati Kigwangala anamwaga matusi..

Hali hii inakera sana..
 
namkubali sana Sugu jamaa anajua jinsi ya kuwatekenya hawa mabwege!
 
Ninafuatilia bunge jioni hii SUGU amesema serikali ni ya wapumbavu, Kigwangala yeye kawaita wabunge wa CHADEMA wapuuzi kisa walikuwa wanamzomea,kwa kifupi wabunge wengi hawajadili hoja za msingi na badala yake wanajadili mambo ya vyama vyao ,bunge limejaa vijembe na upuuzi mwingine.

Kwa bunge letu hili tuna haki ya kuwa maskini milele.
 
Nafikiri bunge la tanzania linaweza kuwa ndo bunge bovu kuliko yote duniani. Bunge ambalo asilimia kubwa ya wabunge hawajui kwanini wako bungeni.
 
CHADEMA shupalieni mambo ya kumkomboa Mtanzania tafadhali wala msibishane na CCM, wenyewe wanajua wanachotetea, mtu kama Mwigulu ataongea nini wenye hekima wamsiklize?
 
Back
Top Bottom