Mh Makonda: Mkandarasi barabara ya Makongo shida nini!

gango2

JF-Expert Member
Aug 31, 2011
1,941
2,251
Ni takribani mwezi mmoja sasa umepita Tangu mlipokuja na magreda na magari mengi kuzindua ujenzi wa barabara ya MAKONGO "tarehe 1 November"

Sasa tunaanza kukosa matumaini tena maana mlipoondoka siku hiyo na magari hayo nayo yakaondoka, tunaendelea kula vumbi kama kawaida! hakuna hata dalili kuonyesha kuna kitu kinaendelea kwenye ujenzi huu!

Barabara hii ina hali mbaya sana kwani kifusi kilichomwagwa mwanzo kilikuwa na mawe sasa baada ya mvua kunyesha udongo unaondoka unaacha mawe hivyo ni shida sana magari kupita.


===
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Tanzania, Paul Makonda amesema barabara ya Makongo Juu itajengwa kwa kiwango la lami kwa muda wa mwaka mmoja.

Mkuu huyo wa Mkoa pia alizindua ujenzi wa barabara ya Madale yenye urefu wa kilomita sita, utakaofanyika kwa mwaka mmoja na nusu, akibainisha kuwa kukamilika kwa ujenzi wa barabara hizo kutaondoa kero kwa wananchi, kupunguza foleni kwenda katikati ya Jiji.

Ujenzi wa barabara ya Makongo Juu yenye urefu wa kilomita 4.5 utagharimu Sh8.9 bilioni zinazojumuisha malipo fidia na uhamishaji na miundombinu ya maji na umeme.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo pamoja na watendaji wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad) ni miongoni mwa walioshuhudia uzinduzi huo. Kampuni ya Jasco ndio inajenga barabara hiyo.

"Poleni sana wakazi wa Makongo Juu na watumiaji wa barabara hii, sio kama fedha hazikuwepo ila mlikosa kiongozi mwenye ushawishi na anayejenga hoja, "amesema Makonda.

Awali, Chongolo amesema kwa kipindi kirefu wakazi wa eneo hilo walikuwa wakitaniwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa mtu atakayeonekana na vumbi anatokea Makongo Juu jambo ambalo hivi karibuni litakuwa historia.

Chanzo: Mwananchi
 
Makonda msanii tu .... mwaka Jana mbele ya rais aliahid hyo barabara ingeanza kujengwa kabla mwaka haujaisha.Mwaka huu tena kaja na magreda kabisa baada ya tararira kaondoka yy na magreda yake.Vumilieni tu muda wa kuwekewa lami ukifika mtawekewa
 
Ni takribani mwezi mmoja sasa umepita Tangu mlipokuja na magreda na magari mengi kuzindua ujenzi wa barabara ya MAKONGO 'tar 1 November"


Sasa tunaanza kukosa matumaini tena maana mlipoondoka siku hiyo na magari hayo nayo yakaondoka, tunaendelea kula vumbi kama kawaida! hakuna hata dalili kuonyesha kuna kitu kinaendelea kwenye ujenzi huu! Barabara hii inahali mbaya sana kwani kifusi kilichomwagwa mwanzo kilikuwa na mawe sasa baada ya mvua kunyesha udongo unaondoka unaacha mawe hivyo ni shida sana magari kupita.
Hivi unamjua Kweli Paul Makonda au Unamsikia? Ebu Muulize Chabruma atakupa TANTALILA ZAKE huyo Daudi Albert Bashite.
 
Wadau,hiyo kampuni ya Jasco hats huku Mbagala walianza kazi za kujenga barabara za dmdp julai 15,sasa wana mwezi wa pili ujenzi umesimama,hali ya barabara imezidi kuwa mbaya hasa baada ya mvua nyingi zinazo nyesha sasa.
 
Hapo juu nimesoma barabara hio itajengwa kwa mwaka mmoja. Kilometa 4.6 zinajengwa kwa mwaka mmoja?!! Subirini mwaka uishe mumuulize
 
Hapo juu nimesoma barabara hio itajengwa kwa mwaka mmoja. Kilometa 4.6 zinajengwa kwa mwaka mmoja?!! Subirini mwaka uishe mumuulize

nikweli hata sie limetutia wasiwasi sana barabara ya km 4.6 kujengwa mwaka mmoja???? yaani hii barabara inaukakasi sana
 
Paulo Makonda a.k.a bashite yupo kajaa tele huku


sema naona atakuwa ana ID nyingine
1575195645482.png
 
Wadau,hiyo kampuni ya Jasco hats huku Mbagala walianza kazi za kujenga barabara za dmdp julai 15,sasa wana mwezi wa pili ujenzi umesimama,hali ya barabara imezidi kuwa mbaya hasa baada ya mvua nyingi zinazo nyesha sasa.
Hiyo Barabara mpk kiongozi aende
Ila lazima Kuna wanasiasa wameingilia budget sijui umenielewa!

Ova
 
Barabara 6km inajengwa mwaka mmoja na nusu? Na 4.5 inajengwa ndani ya mwaka mmoja!!!
Kuna tatizo mahala, huu uzinduzi ulifanyika baada ya ile kiki ya kuomba hela za ujenzi wa hospitali ya Ubungo na mtu moja kusema kwamba wabunge wa upinzani hawawatei wananchi wao, baada kushambulia ubungo akakimbilia jimbo la kawe. Haya ndiyo matokeo yake.
 
Shida wakandarasi wengi hawajalipwa! wee unataka barabara iishe kama serikali haijalipa kazi itaendeje?
Ni takribani mwezi mmoja sasa umepita Tangu mlipokuja na magreda na magari mengi kuzindua ujenzi wa barabara ya MAKONGO "tarehe 1 November"

Sasa tunaanza kukosa matumaini tena maana mlipoondoka siku hiyo na magari hayo nayo yakaondoka, tunaendelea kula vumbi kama kawaida! hakuna hata dalili kuonyesha kuna kitu kinaendelea kwenye ujenzi huu!

Barabara hii ina hali mbaya sana kwani kifusi kilichomwagwa mwanzo kilikuwa na mawe sasa baada ya mvua kunyesha udongo unaondoka unaacha mawe hivyo ni shida sana magari kupita.


===
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Tanzania, Paul Makonda amesema barabara ya Makongo Juu itajengwa kwa kiwango la lami kwa muda wa mwaka mmoja.

Mkuu huyo wa Mkoa pia alizindua ujenzi wa barabara ya Madale yenye urefu wa kilomita sita, utakaofanyika kwa mwaka mmoja na nusu, akibainisha kuwa kukamilika kwa ujenzi wa barabara hizo kutaondoa kero kwa wananchi, kupunguza foleni kwenda katikati ya Jiji.

Ujenzi wa barabara ya Makongo Juu yenye urefu wa kilomita 4.5 utagharimu Sh8.9 bilioni zinazojumuisha malipo fidia na uhamishaji na miundombinu ya maji na umeme.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Daniel Chongolo pamoja na watendaji wa Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroad) ni miongoni mwa walioshuhudia uzinduzi huo. Kampuni ya Jasco ndio inajenga barabara hiyo.

"Poleni sana wakazi wa Makongo Juu na watumiaji wa barabara hii, sio kama fedha hazikuwepo ila mlikosa kiongozi mwenye ushawishi na anayejenga hoja, "amesema Makonda.

Awali, Chongolo amesema kwa kipindi kirefu wakazi wa eneo hilo walikuwa wakitaniwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa mtu atakayeonekana na vumbi anatokea Makongo Juu jambo ambalo hivi karibuni litakuwa historia.

Chanzo: Mwananchi
 
Back
Top Bottom