Bashungwa atoa miezi miwili Mkandarasi Kukamilisha Daraja la Mto Ruaha Mkuu - Kilombero

Nyakijooga

Senior Member
Dec 9, 2018
123
202
WhatsApp Image 2024-02-23 at 19.11.16_30e3b8c2.jpg
Waziri wa Ujenzi, Innocent Bashungwa ametoa miezi miwili kwa Mkandarasi wa Kampuni ya M/s Reynolds Construction Company kukamilisha ujenzi wa Barabara ya Mikumi-Kidatu-Ifakara, sehemu ya Kidatu-Ifakara (Km 66.9) kwa kiwango cha lami pamoja na Ujenzi wa Daraja la Mto Ruaha Mkuu.

Waziri Bashungwa ametoa maagizo hayo tarehe 23 Februari 2024, wilayani Kilombero mkoani Morogoro mara baada ya kukagua Barabara hiyo na Daraja la Mto Ruaha Mkuu na kutoridhishwa na kasi ya ujenzi ambapo Mkandarasi yupo nje ya muda wa mkataba wa kukamilisha mradi huo.
WhatsApp Image 2024-02-23 at 19.11.19_1177034d.jpg

WhatsApp Image 2024-02-23 at 19.11.14_74a62073.jpg
“Sijaridhishwa na kasi ya mkandarasi, hivyo nimempa miezi miwili awe amekamilisha hii barabara, asipofanya hivyo akija kuomba kazi yoyote ndani ya nchi hii hatuwezi kumpatia,” amesema Bashungwa.

Aidha, Bashungwa ameongeza kuwa Mkandarasi ameshalipwa Fedha zote za kutekeleza mradi huo kwa wakati na Daraja hilo linajengwa kwa viwango imara Sambamba na Ujenzi wa Barabara zake.

Amesema Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, anataka barabara hiyo iwe barabara ya kitaifa kwani inaunganisha Mkoa wa Tanga-Morogoro-Njombe pamoja na nyanda za juu kusini hadi kufika bandari ya Mtwara.

“Kuanzia bandari ya Tanga-Handeni kuja Turiani-Kilosa-Mikumi kupita Kidatu-Kilombero kwenda ifakara -Mlimba hadi lupembe mkoani Njombe hadi Kibena inaunganishwa kwa kiwango cha lami” amesema bashungwa

Akitoa Taarifa ya Mradi, Meneja wa Wakala wa barabara nchini (TANROADS) Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Alinanuswe Kyamba, amesema ujenzi wa barabara hii unafadhiliwa na mfuko wa maendeleo wa Nchi za ulaya, ukishirikiana na shirika la Msaada la Uingereza ( UKAID) pamoja na Shirika la Kimarekani la Maendeleo ya Kimataifa( USAID).

Vilevile, ameongeza kuwa Ujenzi wa barabara hiyo na Daraja la Mto Ruaha Mkuu ni sehemu ya mkakati wa Taifa kusaidia wakulima wadogo kupitia program ya Uendelezaji kilimo katika Ukanda wa kusini mwa Tanzania-SAGCOT, walioko katika Bonde la Mto Kilombero ili kuyafikia masoko ya uhakika ya mazao yao kipindi chote cha mwaka.

Kwa upande wake Mbunge wa Kilombero, Abubakar Asenga, amesema daraja hilo ni sehemu ya Barabara ya Kidatu -Ifakara na ni daraja ambalo linasubiliwa sana na Wananchi hao kwani kukamilika kwake kutafungua Fursa kwa wakazi wa kilombero na Mkoa kwa ujumla.

Naye, Mbunge wa Mikumi Denis Londo, ameishukuru Serikali ya Awamu ta sita chini ya Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa iliyofanyika ya utekelezaji katika Mkoa wa Morogoro.

IMG-20240223-WA0018.jpg

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Aache porojo za kitoto!

Kama mkandarasi alikwishalipwa fedha yote,na kazi alitakiwa kuikamilisha toka 2020,imekuwaje asivunjiwe mkataba na ashitakiwe ili alipe fidia?

Tunasikia kila siku serikali ya Tanzania inashitakiwa Mahakama za kimataifa kwa kuvunja mikataba mbona hatusikii yenyewe ikishtaki?
 
Back
Top Bottom