Mkuu, watu wengi huwa tunadhani kuwa usomi ndio kipimo cha mtu mwenye hekima na busara. Ni kweli mtu msomi licha ya kuheshimika katika jamii lakini pia anatumika kama mshauri katika masuala mbalimbali yakiwemo ya kitaaalamu au hata ya kijamii, pale itakapohitajika ushauri katika kupata suluhu iwapo kutatokea kusigishana katika jamii.
Lakini vidato pekee haviwezi kupambanua kiwango cha busara na hekima alizo nazo mtu. Na hii inatokana na jinsi wasomi wetu walivyofinyangwa kuanzia katika malezi mpaka huko mashuleni. Kama elimu ndiyo kipimo cha hekima na busara ni dhahiri kabisa leo kusingekuwepo na ufisadi na ubadhirifu ambayo hufanywa na wasomi wanaotegemewa. Kama elimu ndiyo kipimo cha hekima na busara ni dhahiri kabisa Halima Mdee asingesema kwenye mkutano wa hadhara kuwa Wassira ana sura mbaya kama ya sokwe mtu.
Kwa hiyo, Lusinde hakuhitaji kuwa msomi ili asimwage yale matusi. Alichohitaji ni hekima na busara tuu. Naamini kabisa mtu aliyeishia darasa la saba ana uwezo wa kuwa na hekima na busara ya kutoongea matusi ya aina ile hadharani tena kwenye mkutano wa kampeni za kisiasa.