Sidhani kama Lusinde ndiye yuko under microscope. Otherwise, utakuwa una-narrow tatizo na kufanya solution isipatikane. Tatizo hapa ni Watanzania wenyewe. Kama walikuwa tayari kuwa pale kusikiliza na kushangilia kwa yale waliokuwa wanayasikia, basi wao ndio wanatakiwa kuwa under microscope. Labda na wale waliomchagua pia. Kumbuka Lusinde ni mwakilishi wa watu na possibly ata-reflect waliomchagua.
Kama hao Watanzania wangekataa kusikiliza matusi, angeyasemea wapi? Ndio maana hata chama chake kinaweza kisimchukulie hatua zozote kwa sababu kinajua wazi walio na tatizo ni akina nani.
Kwa hiyo, badala yake, hotuba yake ya matusi ingekufanya binafsi upende kujua kwa undani baadhi ya mambo ya msingi kuhusu Watanzania waliokuwa wanamsikiliza na kumshangilia kama:
1. Wanazo akili timamu kweli?
2. Kama hawana akili sheria inasemaje kwa mtu asiye na akili?
3. Kama wanazo kwa nini walishangilia matusi yale?
4. Je historia yao ikoje?
5. Malezi yao yalikuwaje?
6. Na mengine ambayo wadau mtapenda kuongezea.