Mh. Joseph Selasin: Asante Rais Kikwete

Mh. Joseph Selasin: Asante Rais Kikwete


Huo ni wajibu wake na ni lazima atekeleze kwa kuwa anakusanya kodi.Kama si ufisadi barabara hii ilitakiwa ikamilike muda mrefu.
.......

Hivi wewe ulipokuwa unafaulu Darasani mbona Wazazi wako hawakuita kukupongeza kwa sababu eti ni wajibu wako kusoma na kufaulu?

Hizi ni akili za kitoto tu unastahili kusamehewa kwa vile hujui hata usemalo.
 
Duh umekomaa kwa propaganda.nimefurahi ujasiri wako wa kutumia makosa ya mwenzako kujiimarisha kisiasa
Ninachokiona hapa unacheza siasa na wanasiasa vijana wenye misimamo mikali kama ya kwako ni hatari sana kwa amani ya nchi yetu.type ya akina Tundu Lissu na Sheikh Ponda
Ninachojua ni kwamba unahiandaa kugombea Rombo ndiyo maana uko vitani na nimeona jinsi ulivyokomaaa na hili kwenye mitandao na hasa page yako ya facebook na twitter.hoja ulizojenga ni kweli lakini kumbuka mtu huwa anakosea na hata wewe utakapokua mbunge utafanya makosa
Misimamo mikali kama hii itazidi kutuletea machafuko tu mkuu.Watu wa Rombo jihadharini na wanasiasa wa aina hii.Selasini anapiga kazi na hakuna wa kumtoa na Chadema tukifanya makosa huyu kumpitisha huyu Saanane basi yatatokea ya Tarime endapo atajiunga na CCM na kugombea tena huko

Kwani CDM wao na hoja zao za mabadiliko watakuwa hawakusanyi kodi? Maendeleo yatakuja kwa kutumia mishahara yao ya mifukoni? kazi kweli kweli. Subirini 2015 mtakavyokung'utwa na wananchi kwa vile sasa wameshajua kuwa CCM iko kikazi zaidi tofauti na ninyi mnaokesha kutaka kuingia ikulukwa majungu kama haya na kubeza yaliyofanywa na serikali.
 
Hivi wewe ulipokuwa unafaulu Darasani mbona Wazazi wako hawakuita kukupongeza kwa sababu eti ni wajibu wako kusoma na kufaulu? Hizi ni akili za kitoto tu unastahili kusamehewa kwa vile hujui hata usemalo.

Huyu anafanya makusudi tu na vilevile kuna mantiki katika hoja yake.hatuwezi kubatiza miradi majina ya watu ambao wanatekeleza wajibu wao.
Hilo la baba kumpongeza huoni anampongeza kwa ni mtoto?na kisaikolojia mtoto anahitaji motisha.kwa hiyo Rais ni mtoto
 
Chadema wataona 2015.Nilimuona Ben Saanane akiponda uchaguzi wa vijana CCM kwamba ni Mnada huku akisahau uchaguzi wa BAVICHA ambao alikua mgombea walienguliwa kwa Rushwa.

Nilimwambia hawawezi kupambana na UVCCM siku walipokua wakirushiana maneno makali na Beno Malisa pale Rose Garden.

Pia yeye ni sehemu ya waliohusuka kupandikiza mamluki Uvccm wakishirikiana na akina Sango kasera na Makondo ambao walikua wagombea makamu mwenyekiti kwa lengo la kuidhoofisha UVCCM ili asipate changamoto andapo atashinda uchaguzi wa BAVICHA.Aachane na CCM.
 
hongera mheshimiwa joseph selasin, mbunge wa rombo kwa kuwa muwazi kuhusiana na utendaji murua wa rais jk kwa kuwezesha ujenzi wa barabara jimboni mwake.

Amediriki kutamka mbele ya rais jk kuwa "ingekuwa amri yake barabara husika ingeitwa jakaya kikwete road"


source: Taarifa ya habari tbc, saa 2 usiku, october 30, 2012




tubadilishe ama tuirekebishe katiba na tumwongezee kipindi kingne kiongozi shupavu kama jk aendelee kuiongoza nchi hii
mimi pia ni pro-chadema lakini sina kinyongo hata chembe na rais kikwete
 
Chadema wataona 2015.Nilimuona Ben Saanane akiponda uchaguzi wa vijana CCM kwamba ni Mnada huku akisahau uchaguzi wa BAVICHA ambao alikua mgombea walienguliwa kwa Rushwa
Nilimwambia hawawezi kupambana na UVCCM siku walipokua wakirushiana maneno makali na Beno Malisa pale Rose Garden.Pia yeye ni sehemu ya waliohusuka kupandikiza mamluki Uvccm wakishirikiana na akina Sango kasera na Makondo ambao walikua wagombea makamu mwenyekiti kwa lengo la kuidhoofisha UVCCM ili asipate changamoto andapo atashinda uchaguzi wa BAVICHA.Aachane na CCM

Nje ya mada....

Kwanza sijawahi kutuhumiwa kutoa au kupokea rushwa uchaguzi wa BAVICHA

Hata hivyo usilete mambo yasiyowahusu wana JF hapa.Najua unajaribu kujinasua kwenye hoja ya kuvuruga chama chenu na umekua ukisema hadharani kwamba ubamtaka nani achukue nafasi yako.

Kajibu hoja za vijana ndani ya chama chako kuhusu tuhma za Rushwa huku ukijua ulikua na wajibu wa kusimamia mchakato huru na wa haki.Ni aibu kwa vijana kama ninyi kuendekeza rushwa kama wazee wenu.Hakuna ajenda ya vijana

Btw:Hamna ubavu wa kuzuia mabadiliko yanayoongozwa na CHADEMA
 
hivi ritz hunaga likizo.....mbona wafanyakazi wengine wanapewa likizo na nape?....au kanuni ni double standard?

Ritz ni kama ofisi. Akiwa likizo mmoja mwingine ana kaimu. Ukifuatilia sana utagundua kuwa mawazo na mitizamo yake hubadiilikabadilika kutegemeana na nani yuko 'shift'. Ila wote wana msimamo mmoja wa kidini.
 
Duh umekomaa kwa propaganda.nimefurahi ujasiri wako wa kutumia makosa ya mwenzako kujiimarisha kisiasa
Ninachokiona hapa unacheza siasa na wanasiasa vijana wenye misimamo mikali kama ya kwako ni hatari sana kwa amani ya nchi yetu.

Type ya akina Tundu Lissu na Sheikh Ponda ninachojua ni kwamba unahiandaa kugombea Rombo ndiyo maana uko vitani na nimeona jinsi ulivyokomaaa na hili kwenye mitandao na hasa page yako ya facebook na twitter.

Hoja ulizojenga ni kweli lakini kumbuka mtu huwa anakosea na hata wewe utakapokua mbunge utafanya makosa.

Misimamo mikali kama hii itazidi kutuletea machafuko tu mkuu.Watu wa Rombo jihadharini na wanasiasa wa aina hii.

Selasini anapiga kazi na hakuna wa kumtoa na Chadema tukifanya makosa huyu kumpitisha huyu Saanane basi yatatokea ya Tarime endapo atajiunga na CCM na kugombea tena huko.

Karibu JF-Post yako ya kwanza

-Sijawahi kutangaza hata siku moja nitagombea ubunge Rombo au popote.Leta ushahidi

-Pia uache kutisha watu.Let democracy prevail
 
Jk hajashtuka sifa alizopewa..........hahaaaa siasa bana.........

Niliisha sema kwa JK lazima CDM waisome namba , na hapo bado kila mbunge wa cdm atapiga goti kwake kutoa shukrani
 
Niliisha sema kwa JK lazima CDM waisome namba , na hapo bado kila mbunge wa cdm atapiga goti kwake kutoa shukrani

Ukitaka kujua rais wako anapenda sifa za kijinga, subiri iko siku watampongeza kunya mavi ya kizungu.....................sifa za kizungu
 
Mbunge mpuuzi siku zote utamjua tu kwani kikwete ndie aliyeleta hiyo barabara?.....another shibuda
 
Kwani CDM wao na hoja zao za mabadiliko watakuwa hawakusanyi kodi? Maendeleo yatakuja kwa kutumia mishahara yao ya mifukoni? kazi kweli kweli. Subirini 2015 mtakavyokung'utwa na wananchi kwa vile sasa wameshajua kuwa CCM iko kikazi zaidi tofauti na ninyi mnaokesha kutaka kuingia ikulukwa majungu kama haya na kubeza yaliyofanywa na serikali.

CHADEMA itakusanya kodi na kuweka vipaumbele kulingana na sera makini zitakazowaletea wananchi maendeleo na kwa wakati

Hii ndiyo tofauti ya Chadema na CCM

Kumbuka 'Haki iliyocheleweshwa ni sawa na haki iliyonyimwa'
 
Nivema kuwapa motisha/kuwasifia viongozi wetu wanapofanya vizuri kama J.selasini,na pia tusihofu kuwaambia pale wanapo boronga.Niwachache mno kama selasini,kwani wengi hutukuza mabaya,hata kama ni moja kati ya mia.Atayaacha 99mazuri nakwenda kwa baya 1.Big up J.selasini
 
Vijana hizo roho za kwa nini mpaka lini? Mh Selasini amesema ukweli wake wewe unapata shida gani? Kama serikali ya Mh Kikwete imefanya jambo jema waache wasifiwe, tatizo nini vijana mnapenda kulaumu tu?

Mbona hizo barabara alizojenga Mh Kikwete ndizo mnazitumia kufanyia maandamano yenu? Au mtaanza kuandamana pembeni ya barabara?

Mimi nasema hivi mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni - kama hutaki jitundike. Liwalo na liwe (Mh. Pinda)

Wewe ndo yule mzazi ambaye akileta nyama anawasimangia wanawe eti shukuruni sana mmezaliwa kwangu la sivyo hizi finyango mngezisikilizia mbali. Kazi ya ujenzi wa nchi siyo ombi na siyo jambo la kuliona ajabu ni wajibu wenu kulitekeleza.

Kinachowafanya mkurupuke na kujenga ni nini na huo uwezo mmeupata wapi wakati kila siku mnailaani nchi kuitamkia umaskini?
 
Wewe ndo yule mzazi ambaye akileta nyama anawasimangia wanawe eti shukuruni sana mmezaliwa kwangu la sivyo hizi finyango mngezisikilizia mbali. Kazi ya ujenzi wa nchi siyo ombi na siyo jambo la kuliona ajabu ni wajibu wenu kulitekeleza.

Kinachowafanya mkurupuke na kujenga ni nini na huo uwezo mmeupata wapi wakati kila siku mnailaani nchi kuitamkia umaskini?


Ni utamaduni mzuri kushukuru au kutoa pongezi kwa jambo jema lililofanyika bila kujali ni nani aliyefanya. Sio zaidi ya hapo ndg yangu.
 
Big up mbowe pia kamwaga pongeza kwa maendeleo makubwa ya barabara je mbowe pia nataka kurudi ccm acheni wivu wa kike serikali ya ccm imejenga mtandao wa kutisha wa kutisha barabara za lami hata leo nilikua safari watu ktk gari wanakiri kuwa serikali yao inafanya kazi sana hasa ktk miundombinu ya barabara CCM HAIIIIIII hoyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee,asanteni walipa kodi kukiamini ccm kusimmia kodi zenu kujenga mabarabra Tabora nao wanakula lami ,hakika ahadi zinatekelezwa
 
Safi kada wa cdm kwa kuwa mkweli na kukubali ukweli mana kina slaa wanapinga kila kitu hata penye ukweli

Watu wa kaskazini wapo makini na unafki kwao hauna nafasi penye kazi wanakubali tofauti na huku mbeya Rais huyo huyo alikuja kufungua mradi mkubwa wa maji jiji la mbeya wa zaidi ya shs bil 90 lakini mbunge wetu hakutokea kwa imani upinzani ni uadui na kukataa kila jambo!!! kimsingi elimu inahitajika sana kwa baadhi ya maeneo.
 
Back
Top Bottom