Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

specialists wajiandae kula vichwa 300 wakianza na dr swakala

dr. Swakala alikua anatetea madai ya hao specialists pia ambao leo wanaendelea na kaz huku swakala akiwa amesimamishwa, huon kua kua alichofanya n sahihi kutokana na unafk, usaliti wa hao mabingwa...
 
Vigeugeu hawa! Kwa mwenendo huu nchi haitakombolewa kamwe. Mafisadi wataendelea kutunyonya damu huku tukiwapigia magoti na makofi juu!
 
Mtu akikiri kosa, na kwa nini wasiadhibiwe?..basi wasamehewe lakibi wale watu waliokuwa wakisema watawafungulia madaktari kesi..haya sasa ndio hao sasa..waahtakini!!
 
Those so called doctors. Are they not imposters?
 
Oooooh! My poor Tanzania! Tunaweza kukonect hili tamko na ukimya wa Dr. Ulimboka sasa.
 
Kama wameomba radhi waburuzwe mahakamani wote na viongozi wao kwa kusababisha usumbufu mkubwa na kusababisha vifo kumbe walikuwa wanafanya utani. Kamata wote weka ndani!! Usaliti gani huu?
 
Hawa kweli ni WASOMI?Sijapata ona wasomi kama hawa kwa kweli!Yale yale ya Dr Ulimboka watz maskini walimchangia hadi nauli kurudi kapona kanyamazishwa!

Hamna sector inayotia aibu wasomi KAMA ma-Dr wa TZ!Hawa sio wasomi bali ni wababaishaji tu!
 
Upumbavu,yaani alichotendewa ulimboka kidogo wanae wapoteze baba na mke mume,na mama na baba mtoto,leo hii mnasema hv,yaani madaktari wana poor vision namna hii,u should hav cn this early,mmeua wangapi?halafu ndo mnajua,ningekuwa raisi nawafuta kazi maana inaonyesha mapungufu makubwa kwa wanaoitwa wasomi,
 
namkumbuka Daktari wa falsafa ambaye aliingia upinzani,magamba wakamkalia kooni akajikuta hana udiwani,hana Ubunge n.hana uhadhiriwa chuo kikuukuu cha Manzese halafu askakuta hata haki ya kufanya kazi kama wakili huku Tanganyika hana.Huyu alirudishwa CCM kama vile anabarikiwa na askofu hapo jangwani.
Hakuna tatizo kubwa kama kugawanywa na mkagawanyika kama kundi.Toba hiyo ni ngumu na hata maslahi yenu mtaambiwa myakane yote ndipo mrudi kazini,kama huyu daktari wa falsafa ya sheria!naona aibu kusikia hili

Masumbuko Lamwai...
 
Kusema kweli hata kama hawajasamehewa sidhani kama hao ndugu zetu waliopotea kama watarudi. Tuwasamehe, ni vijana waliorubuniwa, wakushtakiwa ni wale wa MAT.

hahaha!!..unaona mkuu hapo ndipo unapokosea unaposea madaktari walioko mafunzoni(intern doctors) ..as in juniour doctors, hatumaanishi ni "VIJANA" wadogo or wa makamo unavyochukulia mkuu, ni "vijana wadogo katika experience ya utabibu" na si UMRI, watu wamekula chumvi mkuu!!

Na kwa nini uwashtaki "wale wa MAT", hivi unajua mwanachama wa MAT ni yupi mkuu? halafu kama ingekuwa ukisamehewa hakuna mashtaka then migomo itadumu MILELE na vifo itakuwa kama kawaida mkuu.
 
Mtu akikiri kosa, na kwa nini wasiadhibiwe?..basi wasamehewe lakibi wale watu waliokuwa wakisema watawafungulia madaktari kesi..haya sasa ndio hao sasa..waahtakini!!
unapokiri uhalifu kinachofuata ni hukumu.nchi haiongozwi kwa misamaha bali sheria.
 
Hakuna mtu asiyeaminika kama mtanzania. umasikini ni kitu kibaya sana. mwingine atauza hadi utu wake

Na huu ndio ubaya wa kusoma shule za kukariri..yani vijana wametumia atleast miaka 20 shule lakini wamekosa creativity za kutengeneza ajira yao wenyewe..kwa staili hii hata serikali kesho ikiamua kuwa mishahara inapunguzwa kwa asilimia hamsini wataendelea kunyenyekea tu..
 
Mlimdharau Pinda aliposema LIWALO NA LIWE pamoja na Rais Kikwete alipowaambia mapema madhara ya mgomo kwenu nyie(interns) mkajifanya kichwa ngumu leo mnalia nini? Komaeni hivyo hivyo...!!


Wakati Rais anazungumzia madhara, hwa walikuwa wameshafukuzwa. Kwa hiyo hawa hawakupata muda wa kuomba msamaha...
 
Kumbe walikuwa wanafuata upepo? Sasa ndio watamjua JK alivyo na kiburi... Hawa inabidi wasisamehewe kwa sababu watarudi na hasira kwa wagonjwa, watafute tu kazi nyingine. Kama vipi wawombe radhi Blandina Nyoni, Mponda na Lucy Nkya pamoja na Dk Deo Mtasiwa waliosema hawafai
 
I wonder sijasikia registrars ambao wamepoteza ajira zao wakitetereka katika msimamo wao!
All in all hawa mamluki hawatafanikiwa kamwe.

Kwa sababu registrars wana usajiri unaowaruhusu kufanya kazi mahali kwingine nje ya serikali. Huwezi kuwafananisha na interns ambao hawaruhusiwi kufanya kazi hospitali yoyote.
 
Maskini Blandina Nyoni alipoteza Mama mzazi aliyepata Pressure baada ya kusikia Mwanaye kasimamishwa kazi, kumbe madaktari walikuwa wanabip?
 
Vigeugeu hawa! Kwa mwenendo huu nchi haitakombolewa kamwe. Mafisadi wataendelea kutunyonya damu huku tukiwapigia magoti na makofi juu!
sio vigeugeu, laana ya vifo vya watz waliokufa wakati wakiwe kwenye mgomo imeanza kuwalamba. mtaani wataishiwa kandambili hadi watatembea peku. tumewasomesha kwa kodi zetu halafu hawataki kututibu, wana faida gani sasa hawa? una zaa mtoto wako wewe mwenyewe halafu anakuja kukunyyea mbele za watu akiwa na umri mkubwa tu, au unazaa mtoto wako mwenyewe halafu akifanikiwa anakuja kukuchukua mzazi wake msukule...wana faida gani sasa hawa?.....hawakujua wanaochofanya, hawakuwa na plan B, mi nilijua wanataka kwenda zao botswana ambako nasikia nako wanawakimbiza kwasababu ya incompetence. waachwe mtaani watembee kwa mguu walau hata kwa mwaka mzima, wakose hela wawe ombaomba hadi wawe makameruni, ndo wawarudishe. hawana adabu wala staha....akiwepo na ulimboka mwenyewe.
 
Back
Top Bottom