Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

Mgomo: Madaktari waiangukia serikali!

nategemea tamko la madaktari kupitia MAT na sio hawa mamluki
 
Upumbavu,yaani alichotendewa ulimboka kidogo wanae wapoteze baba na mke mume,na mama na baba mtoto,leo hii mnasema hv,yaani madaktari wana poor vision namna hii,u should hav cn this early,mmeua wangapi?halafu ndo mnajua,ningekuwa raisi nawafuta kazi maana inaonyesha mapungufu makubwa kwa wanaoitwa wasomi,
kipindi kile watu mnashabikia ulimboka nilisema kuwa madaktari hawana akili mkapinga sana hapa...leo ndo unawaona? hwa majamaa hawana maana ndo maana wanapasua kichwa badala ya mguu. siku ukipeleka mtoto wako wakatahiri angalia wasijekumng'oa macho badala ya govii.
 
Another Saga!!!! Lazima kuna nguvu kubwa juu ya tamko hili!!!!!
 
Kwa hiyo wanataka na Nyoni, Nkya na Mponda warudi kwenye nafasi zao?
 
Ahsante kwa info......but mods unganishen uzi huu na ule mwininge....
 
Kabla yhawajasamehewa wapelekwe Mabwepande wapate kibano cha kung'olewa meno na waseme kama "hawakutumwa na Chadema" kwi kwi kwi!!!!
 
Zomba mimi kinacho nishangaza ni kwamba kwa nini ni leo? Leo ni mwezi wa tisa kwa nini hawakuomba msamaha toka mwanzo? Watu wamekufa kwaajili yao leo ndio wanajifanya kuomba msamaha!

Hivi wewe roho inakuuma hawa madaktari kuomba msamaha? maana naona post zako humu hazina raha kabisa.

Punguza ghadhab, kuwa na amani moyoni, fikiria faida ya watanzania walio wengi na upige debe hawa vijana wasamehewe.
 
Unazungumzia walimu ambao wanaednelea na kazi na maisha yao kama kawaida!
Kwanini tunakosa huruma na hawa young professionals?

What have you just Said? Professionals My @zz! This guys arent supposed to be doctors whatsoever. Na huyo wanayemkiss_@ss is not a medical teacher kuwapa udaktari.
 
Akisoma tamko la madaktari la kuwaomba radhi wananchi na rais Mh JK kwa usumbufu uliosababishwa na mgomo wao wa mwezi wa sita mwaka huu,
Pia pamoja na kumwomba radhi MH Rais waesema kuwa wanatambua jitihada zake za kutatua mgogoro ule pia juhudi zake za kutatua changamoto za afya nchini.
Source:Redio wapo yaliotokea leo jion saa moja
My take
mlio karibu na hawa mabwana mtujuze nini kimewakuta je ule mgomo ulikuwa feki?

Mkuu, ni baadhi ya madaktari mkuu, si madaktari wote...wale...soma thread ikiyoandikwa "madaktari kimenuka" kuna info zaidi.
 
Inatia shaka sana wanataaluma wa Kitanzania! Inapokua graduate wa fani inayoheshimika kama ya udaktari wa binadamu anapofanya mambo bila kupima kwanza matokeo ya matendo yake. Daktari anagoma kufanya kazi yake ya WITO bila kupima athari kwa wagonjwa, jamii na kwake yeye binafsi. Anaacha kufanya kazi bila kufikiria kama kuna watu watakufa, bila kufikiria kuwa atanyimwa mshahara na rushwa pia.
Leo anasingizia MAT imewatosa tena anasema kwa unafiki kuwa atawahudumia wananchi kwa moyo mweupe. Ni unafiki ambao hata Shetani atakataa kumtuma useme. Nitakubali akisema NJAA IMEMBANA.Tuliwabembeleza kwa utu wakakataa katakata kutusikiliza. Tuliwalaumu pande zote Serikali na jumuia ya madaktari waache kupigania juu ya Afya za watanzania. Wakaamua kupambana bila kupima matokeo ya vita yao, leo wanawageuka wenzao chama chao na kutueleza upuuzi huu. Hata serikali ikiwaamini madaktari wasioaminika nayo itakuwa ni ya kipuuzi tu. UTAMWAMINIJE MTU ASIYEAMINIKA KUMKABIDHI TENA ROHO ZA WATANZANIA? Nawaombeni wote msifanyie majaribio roho zetu
 
Anayeomba kusamehewa asamehewe ila iwe fundisho kwa wengine. W ajaze upya mkataba wa ajira. Pia wasitumiwe na wanasiasa ili wananchi waichukie serikali.
 
Angalau wameomba msamaha kwa uhaini walioufanya kwa watanzania maskini
 
Ngoja niende makitaba ntarudi baadae...lazma kuna chama nyuma ya hii kama kivuli, CC.........?????nakuja
 
Kwa sababu registrars wana usajiri unaowaruhusu kufanya kazi mahali kwingine nje ya serikali. Huwezi kuwafananisha na interns ambao hawaruhusiwi kufanya kazi hospitali yoyote.

Wakisamehewa Huyo wanayemuomba msamaha ndo atawapa udaktari kamili?
 
Hoa madaktari walioomba msamaha ni wasaliti wakubwa wa ukombozi wa Mtanzania, wanajali matumbo yao tu, wao hawakujua kuwa ukombozi una gharama? Kwanza wamejidhalilisha sana, kumbe mlichokuwa mnakidai hamkukiamini na sasa mnasingizia MAT, hamjui ni jinsi gani serikali ilishughulika kipuuzi na tatizo lenu? NYIE NI WAOGA NA WACHUMIA MATUMBO TU, NA HISTORIA ITAWAKUMBUKA KWA KUSALITI MAPAPMBANO.

Anyway rudini kazini mkiitwa, sisi tutaenelea kupigania ukombozi wa nchi hii mpaka mwisho.[/QUOTE]

Mbalinga
, acha kuwadanganya vijana wenzako...wale wanaojiita kwamba ni wapambanaji na wataendelea kupambana hadi mwisho wamefanya nini so far? Assume wasingeomba msamaha, nini ambacho wange-achieve baadae baada ya mahakama kutoa maamuzi? Kama wenzako asilimia kubwa wako kazini wewe unajifanya unapambana bila kauli, bila kuwahimiza wengine kwa njia za uamsho, bila ushirikiano, unategemea kuitwa mpambanaji?

Mimi siwezi kuwajaji hawa madaktari maana wenzao wengi hawakuwa tayari kupambana au waliwekwa chambo na wenzao, so wakashindwa vita. Retreating is also a technique not to kill the whole army!! Wakajipange!!

Serikali ilifanikiwa ilipowagawa na wakatawalika kwa mafanikio, na hao wanaoitwa mabingwa wakarudi nyuma, wakawaacha vijana wasio na option nyingi wawe mbele... (very weak seniors!!!)

Watanzania wenyewe hawakuwa tayari kwa mabadiliko, wakakaa kimya bila kushinikiza serikali irudishe hali ya huduma ya afya tena hata Dr. Ulimboka alipotekwa na kuumizwa, wananchi hawajaandamana wala kuitaka serikali iwajibike...tena hata baada ya Gazeti kufungiwa hawajachukua hatua zenye tija...sasa wale wanaorudi nyuma baada ya kuona vita hawaiwezi bado, msiwalaumu.

Nawasilisha.
 
Inanikumbusha siasa za udsm kutoa matamko afu kesho yake umoja wa vyuo vikuu TAHLISO unakuja na tamko lake kubatilisha maazimio ya udsm.
 
Back
Top Bottom