wanatakiwa wasamehewe, lakini msamaha usiwe wa haraka kiasi hicho, waachwe kwanza wakae home kama mwaka mmoja ivi ili wakione cha moto, kwa ujinga wao wa kuwagomea watz ambao wamewaridhia wasomeshwe kwa kodi zao halafu kuwatibu watoa kodi hawataki wanajifanya kugoma. wakikaa mtaani wakiombaomba nauli kama mwaka ivi, watapata adabu, ndio wasamehewe. nachelea kusema kuwa, kutowasamehe kabisa ni hasara kwasababu wamesoma kwa pesa za kodi zetu halafu hawajarudisha matunda ya kodi zetu kwa kuwatumikia wananchi, ikizingatiwa kuwa hawa madoctor hata kulipa deni la mkopo nasikia hawalipi kama course zingine. pia tuna uhaba wa madoctor hivyo serikali ijifanye mjinga siku ipite wawasamee ili tupate watu wa kutibu raia wetu. kama kuangukiwa tu serikali imeangukiwa hivyo mbabe ni serikali hakuna haja ya kuendeleza mashindano nyasi ambao ni raia zitaumia tu.