ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,279
- 7,685
Umeongea point kwa mara ya kwanza tangu nikufahamu
Asante Kadu nitaendelea kujitahidi kuongea kwa akili zaidi. Asante sana...
Last edited by a moderator:
Umeongea point kwa mara ya kwanza tangu nikufahamu
Saa hizi serikali ndo imekuwa "haina utaratibu wa kukaa meza moja na wadau mbalimbali?!!
Nyie watu kwa kugeuza maneno, hivi ni serikali ndiyo ilikataa kuongea na madaktari pale Karimjee siyo?
Safi sana, imekula kwao. Wameingizwa kichwakichwa na magwanda. Haya sasa, kila mtu afe na lwake, hakuna wa kuwatetea...si Mbowe, Lema, Slaa au Mnyika. Wao wanaendelea kupeta na posho zao wakati maskini ma dr uchwara wameachwa juani solemba.
Mimi nilitegemea uwahurumie walalahoi wenzio manake kiukweli ndio ambao wanateseka mpaka sasa hivi.....madaktari inawahusu nini?......kilaza wewe!
Safi sana, imekula kwao. Wameingizwa kichwakichwa na magwanda. Haya sasa, kila mtu afe na lwake, hakuna wa kuwatetea...si Mbowe, Lema, Slaa au Mnyika. Wao wanaendelea kupeta na posho zao wakati maskini ma dr uchwara wameachwa juani solemba.
Mimi nilitegemea uwahurumie walalahoi wenzio manake kiukweli ndio ambao wanateseka mpaka sasa hivi.....madaktari inawahusu nini?......kilaza wewe!
Imekula kwa madaktari muda wao wote wamefanya kazi ya bure, kwani kwa sasa inabidi waanze upya shule, ni huruma sana kwao ila ni funzo next time wawe waangalifu na wanasiasa uchwara wa cdm
Wewe pia ni kilaza. Badala ya kuwahurumia ma-dr limbukeni wazembe wachumia tumbo ambao sasa kimenuka kwao, unaleta unafiki wa kuwahurumia walalahoi ambo hao ma-dr wamewaua bila sababu. Huna hoja, kama wewe ni dr uliyegoma, pole, imekula kwako.
Wee naona ndio wale wale wa magamba mnaoendelea kuzisikiliza na kuamini ngojera za Serikali DHAIFU, "Serikali haina uwezo"...Hakuna hata neno moja lililobadilishwa. Madaktari wamegoma mara tatu sasa na mara zote Serikali imeshindwa kutimiza madai mbali mbali ya Madaktari ikiwemo kuboresha sekta ya afya nchini kwa kisingizio "serikali haina uwezo" wakati nci yetu ina utajiri wa hali juu. Ila inapokuja kwenye matanuzi ya Serikali DHAIFU siku zote huwa na uwezo wa kutanua.
Masikini serikali! (Mwanahalisi)
![]()
Na editor - Imechapwa 04 July 2012
![]()
Maoni ya Mhariri
SERIKALI imefunga milango na madirisha. Haitaki tena majadiliano na madaktari juu ya mazingira ya kazi na ujira.
Hii inakuja baada ya mgomo wa madaktari na utekaji na utesaji kinyama wa Dk. Steven Ulimboka, mwenyekiti wa Jumuiya ya Madaktari Tanzania.
Ni kama Rais Jakaya Kikwete ametangaza kuwa asiyekubaliana naye amejifukuza kazi. Tishio kali!
Lakini ndani ya gazeti hili, daktari mmoja amenukuliwa akisema, "…wakati mwingine ninamwangalia mgonjwa, nina uwezo wa kumwokoa, lakini hakuna vifaa. Anakufa mbele yangu."
Huo ni upande mwingine ambao serikali haijaangalia. Yenyewe imekazania kusema "…madaktari wanataka posho! Posho! Posho!"
Daktari anayenukuliwa anaona bila vifaa, hospitali yake ni kituo cha mwisho; mahali pa kusubiria kifo. Serikali haitaki kusikia hilo. Sasa serikali imeona, kwa vitendo kuwa ingekuwa na vifaa, Dk. Ulimboka asingepelekwa Nairobi na, au Afrika Kusini.
Serikali inaona kila siku, kwamba kama kungekuwa na vifaa, viongozi wake wasingekuwa wanapiga foleni kwenda kutibiwa nje. Kinachokosekana si maarifa, bali zana na mazingira bora ya kazi. Serikali haitaki kusikia.
Sasa serikali inasema italeta madaktari kutoka nje ya nchi. Kwamba tayari imetenga Sh. 200 bilioni kuwagharamia.
Serikali imefanya lini makubaliano na madaktari hao? Hizo fedha serikali imezitoa wapi kulipa watu wa nje? Maandiko matakatifu yaliishaonya: Usichukue chakula cha watoto na kumpa mbwa!
Je, madaktari wa nje watakuja na vifaa? Kama hawatakuwa na vifaa si watakuwa wanafanya utalii tu wa kujifunza lugha au kufanya tafiti za kuendeleza utaalam wao?
Tunatangaziwa haraka kuwa baadhi ya madaktari wamekubali kurejea kazini. Hivi serikali inaamini wanakwenda kufanya kazi kwa moyo uleule?
Serikali yoyote ikifunga milango ya mawasiliano, hata kwa njia ya migomo; inakuwa imeziba mifereji ya fikra na matumaini ya muwafaka. Yanakuwa maisha ya kuvimbiana.
Tunaitaka serikali kufanya mambo yafuatayo: Kwanza, iunde tume huru ya kuchunguza waliomtendea unyama Dk. Ulimboka. Pili, iwasikilize madaktari. Tatu, ituhakikishie kuwa italinda uhai wetu na mali zetu.