Mimi nadhani uamuzi wa kuwafutia lesseni ni hasara kwa serikali yenyewe, imetumia muda na gharama kuwasomesha,bado tunaupungufu mkubwa wa madaktari na hilo pengo la madaktari 319 pengo lao ki-uhalisia haliwezi kuzibika kwa muda mfupi. Ndiyo tunasema wapo 700 wanaomaliza mwezi ujao lakini bado uwepo wao ulikuwa hauwaondowi hao 319 kazini bali ilikuwa inapunguza uhaba mkubwa wa madaktari Tanzania.
Ni vyema uamuzi huu ukaangaliwa kwa njia pana zaidi ili kuepuka maamuzi ya kukomoana, mgomo umeisha wapewe onyo la waruhusiwe kuendelea na kazi. Katika hali ya kawaida ni kwa vile tu hana tabia ya kufanya tathmini ya maamuzi yetu, kufukuza madk 319 kunaathiri pia uchumi wa nchi kwa namna moja au nyingine.