Ubabe wa serikali utawaumiza zaidi wananchi wanaotegemea hospitali za serikali, siyo hawa madaktari waliofutiwa leseni kwani bado wana ubongo wao. Leseni ni karatasi tu, kulifuta hakuondoi knowledge ambayo madaktari hawa wameshajisheenza vichwani mwao. Time will tell!! Miaka kadhaa iliyopita, Mwinyi mdogo aliwafukuza madakatri Tanzania kutokana na mgomo kama huu; baada ya muda kidogo nikakutana na dakatri mmoja aliyefukuzwa Tanzania akiwa anaendelea na taaluma yake huko Trinidadi tena kwa heshima kubwa sana.
Kwa vile viongozi wetu wamejijengea tabia ya kwenda kutibiwa nje ya nchi hata mafua tu; hawaoni kabisa umuhimu wa kuendeleza sekta ya tiba nchini. Kufungwa kwa hospitali ya Dr. masau kulitokana na waziri kutaka masau ashirikiane na hospitali moja huko india ambako serikali ilikuwa inapeleka wagonjwa wa moyo. kulikuwa na kila suspicion kuwa waziri mhusika alikuwa na faida kutokana na wagonjwa wa kitanzania kupelekwa katika hospitali hiyo ya india; in other words, kuwapo kwa hospitali inayotoa huduma nzuri tanzania kwao ni kuwakoseasha ulaji. After all hata wanapokwenda kufanyiwa check-up ya mafua wanalipwa per diem kama kawaida; an added advantage.
Wwakati waziri mkuu wa kenya alipougua, alilazwa Hospitalini Nairobi, lakini kwetu kiongozi akiugua, ni lazima apelekwa nje ya nchi. Mzee mandekla hutibiwa Afrika ya kusini pale pale, je sisi tutakomboka lini iwapo viongozi tulio nao ndio hao?.
Ningekuwa daktari mimi, kila mtu kwenye meza yangu angepata aspriri hata kama ana ugonjwa wa moyo hadi pale watu wote watakapoamka na kuiondoa serikali hii madarakani kwa kura nyingi. Kura chache hazitishi kwa vile watachakachua. watu hao hao wakishatibiwa wanasimama upande wa serikali kuwalaani madaktari.