MGOMO: Madaktari 319 wafutiwa leseni

Ok replacement iko wapi? Au anawafukuzatu kwa hasira zake?, asidhani kuwa ni kama kubadili baraza la mawaziri.

Do not personalize the matter aisee, anayewafukuza ni nani hapo?
Kuhusu replacement, sijasikia chuo chochote kufungwa ama kwa dharura madaktari kutoka nchi rafiki, ongeza na wastaafu (the most experienced staff), so dont ask that!!
 
Baraza la Madaktari la Tanganyika????

Kumbe Tanganyika inaishi bado??
 
Mimi nafikiri Serikali ingefikiri zaidi na kuondoa Jazba kwa hili. Mimi nikifikiria uhaba wa wataalamu hawa nchini mwenu na gharama ilizotumia Serikali yenu kuwasomesha miaka mitano na muda wote wa Intern nafikiri ni gharama kubwa sana.

Kwani adhabu hii ni kubwa sana ukilinganisha na kosa lao kwani
1. Intern Doctor haruhusiwi kufanya kazi peke yake bila kuwa na Dr (ikumbukwe ma Dr walikuwa wamegoma)
2. Vile vile intern mtu anaweza kufanyia nchi yoyote ile ambayo itakuwa miongoni mwa Commonwealth Countries na kuweza kutambuliwa katika nchi hizo.
3. Wanaweza kufanyia kazi zao katika Hospital za Znz kwani mambo ya afya hayamo katika mkataba wa muungano wenu. Ndio maana hata MAT ina operate Tanganyika Tu.

Kuna haja ya kukaa pamoja madaktari na Serikali kulimaliza suala hili kwa manufaa ya wananchi. Kusiwe na mshindi wala wa kushindwa kwa faida na manufaa ya wananchi wenu na ustawi wa nchi yenu.

Busara ni muhimu sana kutumika katika suala hili na kuondoa jazba na ubabe.
 
Hivi hawa mawakili wa serikali wanafanyakazi kwa kutumia taratibu zipi?Unampeleka mtuhumiwa mahakamani huku upepelezi bado maana yake nini?
 
Interns Doctors karibuni kwenye real world. Sheria na utawala bora at work. Mkopi pamoja na wenzako acheni kudanganya hawa vijana wadogo wasiyojua procedures za kuleta trade dispute (nadhani hata wewe hujui). You had the sympathy za watu lakini mili overdo.
Kama JK alivyosema kama you are not satisfied go and knock the next door. (Hii ndiyo Real world ilivyo). Interns , at the end of the day it is your life na siyo ya Mkopi. Mkopi anafaidi handouts toka kwa Donors anayewajua yeye(the ones pulling the strings)
 
Kila siku nasema CCM kumejaa vichwa maji na Serikali yake, yaani madaktari wanaddai haki yao then wanakuja kufutiwa leseni zakoo, hatari kwa kweli na 2015 sio mbali......
be sincere mkuu, 2015 ni mbali ukilinganisha na matatizo tunayopitia. Chukulia mfano kama mtu anateswa kwa staili ya Dr. Ulimboka Stephen kwa interval ya miezi mitatu mitatu itakuwaje!?

Lakini pia maswali ya msingi ya kujiuliza hapa:
1. Inachukua muda gani kumfunza daktari mpaka kufuzu?
2. Ni wanafunzi wangapi (vijana) wako tayari na wana uwezo wa kusomea hii fani?
3. Watatumia muda gani na gharama kufidia hilo pengo la madaktari 319?

Lakini swali zaidi tunaloweza kulitumia kujifunza ni kama serikali ingelitumia strategy hii hii kuwasimamisha/kuwafukuza kazi wabadhirifu serikalini si tungelikuwa tunaizidi China kwa maendeleo!????

 
Interns Doctors karibuni kwenye real world. Sheria na utawala bora at work. Mkopi pamoja na wenzako acheni kudanganya hawa vijana wadogo wasiyojua procedures za kuleta trade dispute (nadhani hata wewe hujui). You had the sympathy za watu lakini mili overdo.
Kama JK alivyosema kama you are not satisfied go and knock the next door. (Hii ndiyo Real world ilivyo). Interns , at the end of the day it is your life na siyo ya Mkopi. Mkopi anafaidi handouts toka kwa Donors anayewajua yeye(the ones pulling the strings)
such wonderful ideas ....japo nasikitika na kukiri kuwa tumetumia mawazo haya haya kwa zaidi ya miongo miwili iliyopita na kupelekea nchi kuwa listed kati ya OMBA OMBA watatu bora duniani!?

Keep it up mkuu

 
Kuwafutia leseni ina maana kuwa hawaruhusiwi ku-practice medicine Tanzania; ila bado wanaweza kwenda nchi nyingine inayotambua medical degrees za MUHS na kufanya kazi chini ya daktari mwingine kwa muda fulani kabla ya kuanza kufanya kazi zao independently. Sisi wananchi tusioweza kwenda kutibiwa na kufanyiwa check-up nje ya nchi ndio loosers zaidi kwenye sakata hili.

Kama wanaruhusiwa waende huko! Walijifanya kufuata mkumbo kwa kuiga ... kwa tembo, sasa wamepasuka msamba, walipogoma walikuwa wengi sasa kila mmoja atalia kivyake maana hakuna tena "sisi' imegeuka "mie" kila mtu na barua yake ya kufutiwa.

Mi naona ni sawa, ila ili haki itendeke, si intern tu, kwani sheria haiwahurusu waliothibitishwa na wenye leseni za kudumu?

Hapa nahitaji mwongozo wana JF
 
Ilichofanya serikali ni sawasawa,hawa watoto hawajui kama serikali ipo! wanafanya watakacho kiholela tu, wacha sasa wasage rumba mtaani mpaka visigino viende upande! wanafata mkumbo tu kazi yenyewe hawajapata, haya sasa! hawajui mgoma u,meathiri watu kiasi gani! watalijua jiji.
Acha kujidanganya kuwa Daktari anaweza kusaga rumba mtaani,dispensaries zenyewe na hospitali binafsi
zina uhaba wa madaktari,hivyo wakati wanajiweka sawa hawawezi kufa njaa.unafikiri sawa na wanasiasa?
mtu kama Maige ameondolewa uwaziri anapiga kelele kama chizi.Daktari ana elimu si ya kusoma chuo cha magogoni kama siasa ala!!!!!!
 
Safi sana naiunga mkono serikali kwa hatua inazochukua,

Serikali haiwezi kuyumbishwa na watu wachache kwa tamaa ya mshahara mkubwa na kufanya mgomo bila kujali afya za watu. Kiukweli umeona kazi haina maslahi acha mwenyewe kimya kimya nenda kwenye maslahi manono suala la mgomo halikubaliki hata kidogo.

Kama unaona mshahara mdogo acha kazi mwenyewe nenda kagombee ubunge ukapate mshahara mnono lakini si kufanya mgomo ambao madhara yake watu wamepoteza maisha.

Sasa tunaambiwa mgomo umeisha vipi wale waliokufa kutokana na mgomo watarudije tena si ndiyo tumewapoteza ukimuona mtu anashabikia mgomo huyo si mtu wa kawaida ni mnyama na mwendawazimu kutokana na kutokujali uhai wa watu,kataa mgomo dai maslahi yako kwa njia salama ili kulinda afya za watanzania wote!
 
Mimi nafikiri Serikali ingefikiri zaidi na kuondoa Jazba kwa hili. Mimi nikifikiria uhaba wa wataalamu hawa nchini mwenu na gharama ilizotumia Serikali yenu kuwasomesha miaka mitano na muda wote wa Intern nafikiri ni gharama kubwa sana.

Kwani adhabu hii ni kubwa sana ukilinganisha na kosa lao kwani
1. Intern Doctor haruhusiwi kufanya kazi peke yake bila kuwa na Dr (ikumbukwe ma Dr walikuwa wamegoma)
2. Vile vile intern mtu anaweza kufanyia nchi yoyote ile ambayo itakuwa miongoni mwa Commonwealth Countries na kuweza kutambuliwa katika nchi hizo.
3. Wanaweza kufanyia kazi zao katika Hospital za Znz kwani mambo ya afya hayamo katika mkataba wa muungano wenu. Ndio maana hata MAT ina operate Tanganyika Tu.

Kuna haja ya kukaa pamoja madaktari na Serikali kulimaliza suala hili kwa manufaa ya wananchi. Kusiwe na mshindi wala wa kushindwa kwa faida na manufaa ya wananchi wenu na ustawi wa nchi yenu.

Busara ni muhimu sana kutumika katika suala hili na kuondoa jazba na ubabe.

Seriously naomba kuufahamu uraia wako baru.....
 
Interns Doctors karibuni kwenye real world. Sheria na utawala bora at work. Mkopi pamoja na wenzako acheni kudanganya hawa vijana wadogo wasiyojua procedures za kuleta trade dispute (nadhani hata wewe hujui). You had the sympathy za watu lakini mili overdo.
Kama JK alivyosema kama you are not satisfied go and knock the next door. (Hii ndiyo Real world ilivyo). Interns , at the end of the day it is your life na siyo ya Mkopi. Mkopi anafaidi handouts toka kwa Donors anayewajua yeye(the ones pulling the strings)
Well stated black and white.....
 
Kwa hili, serikali ni sawa na kupiga ngumi ukuta. Watawarudia tu hawana ujanja
 
Ndo maana mimi namshukuru Mungu kwa dawa zake ambazo hazichakachuliki na wala haziwezi kuwa na mgomo wa kutibu. Mnaohangaika na hospital's medicine mtakoma, mimi nikiugua tu fasta nabeba jembe langu naenda kuchimba mizizi ya miti inayotibu ugonjwa husika.
Tazama yuaja na mawingu, na kila jicho litamuona na hao waliomchoma, na kila kabila la wanadamu wataomboleza.
 
usipoteshe umma kama dhaifu anavyofanya wewe kibaraka wa mafisadi RITZ madr wanataka vitendea kazi na sio mishahara huo uongo kawadanganye makada wenu kwenye mataputapu mnayohongwaga na magamba
 
Ubabe wa serikali utawaumiza zaidi wananchi wanaotegemea hospitali za serikali, siyo hawa madaktari waliofutiwa leseni kwani bado wana ubongo wao. Leseni ni karatasi tu, kulifuta hakuondoi knowledge ambayo madaktari hawa wameshajisheenza vichwani mwao. Time will tell!! Miaka kadhaa iliyopita, Mwinyi mdogo aliwafukuza madakatri Tanzania kutokana na mgomo kama huu; baada ya muda kidogo nikakutana na dakatri mmoja aliyefukuzwa Tanzania akiwa anaendelea na taaluma yake huko Trinidadi tena kwa heshima kubwa sana.

Kwa vile viongozi wetu wamejijengea tabia ya kwenda kutibiwa nje ya nchi hata mafua tu; hawaoni kabisa umuhimu wa kuendeleza sekta ya tiba nchini. Kufungwa kwa hospitali ya Dr. masau kulitokana na waziri kutaka masau ashirikiane na hospitali moja huko india ambako serikali ilikuwa inapeleka wagonjwa wa moyo. kulikuwa na kila suspicion kuwa waziri mhusika alikuwa na faida kutokana na wagonjwa wa kitanzania kupelekwa katika hospitali hiyo ya india; in other words, kuwapo kwa hospitali inayotoa huduma nzuri tanzania kwao ni kuwakoseasha ulaji. After all hata wanapokwenda kufanyiwa check-up ya mafua wanalipwa per diem kama kawaida; an added advantage.

Wwakati waziri mkuu wa kenya alipougua, alilazwa Hospitalini Nairobi, lakini kwetu kiongozi akiugua, ni lazima apelekwa nje ya nchi. Mzee mandekla hutibiwa Afrika ya kusini pale pale, je sisi tutakomboka lini iwapo viongozi tulio nao ndio hao?.

Ningekuwa daktari mimi, kila mtu kwenye meza yangu angepata aspriri hata kama ana ugonjwa wa moyo hadi pale watu wote watakapoamka na kuiondoa serikali hii madarakani kwa kura nyingi. Kura chache hazitishi kwa vile watachakachua. watu hao hao wakishatibiwa wanasimama upande wa serikali kuwalaani madaktari.

kuna thread humu jamvini inaeleza kuwa John Komba amekwenda India kucheck afya!
 
Interns wengi walifukuzwa kabla ya hotuba ya Rais. Hivyo kugoma kwao si kwa kutokuheshimu hotuba ya Rais na ninaamini interns wengi wako tayari kuendelea na kazi. Lengo lisiwe kuwakomoa. Tuwasaidie wapewe msamaha na kurudishwa kazini. By the way, kujifunza is what internship is for! Wameshajifunza.
 
kila siku nasema ccm kumejaa vichwa maji na serikali yake, yaani madaktari wanaddai haki yao then wanakuja kufutiwa leseni zakoo, hatari kwa kweli na 2015 sio mbali......

hayo maneno hapo kwenye wino mweusi uliokolea si ya kweli! Mbona hao hao waliojaa maji vichwani wanapochukua kadi za cdm mnawaita majembe/jembe?? haya ndio mambo yanayochelewesha ukombozi wa kweli! Unafiki mwingiiiiiii..!!
 
Unataka suluhu gani tena wakati Madaktari ndio wameanzisha mgomo wakitaka mshahara mkubwa wewe ulikuwa unataka wanachotaka madaktari wanachotaka wapewe tu sababu ni madaktari serikali hawezi kutoa milioni 7.700.000 subirini Chadema wakichukuwa nchi watawalipa milioni 10.
stop :rant:!!
watu wanajaribu kuelewa kimantiki adhari za mgomo na sasa adhari za kufutiwa leseni kwa interns, wewe upo busy na mshahara na CHADEMA.

hawa interns ndo wanaotibu shangazi zako kule kijijini kwenu Masokeni...sasa watatibiwa na Profesa tall water ambaye haitaji leseni ya kutibu.
Hawa interns wanafanya kazi chini ya registrars na specialists.........mbona hao hawajafutiwa?

Serikali ndio inayo-paralyse medical services yenyewe....na huku inajichanganya kwenye mahakamani, inatafsiri sheria yenyewe kwamba MAT wamedharau mahakama, wameamua kwamba hiyo ni jina....

hii akili nafikiri ndo akili ya akina Ritz...akili ya kwenda kwenye Family Planning Summit kwa vile Bill gates na Belinda watakuwepo pia.
Akili ya kuhemea vijihela vya miradi ya kupuuzipuuzi tu, wakati umeacha watu wanaondoka na mali ndani kwako!
 
Back
Top Bottom