Mgogoro wa Waislam UDOM waingia hatua mpya: Sheikh Ponda atoa tamko zito

Basi waishi ktk misingi ya Umma,na sio ktk preferences zao ambazo zinataka dini yao ipewe kipaumbele wakati kipaumbele ni umma kama one group na sio individual religious groups.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuishi katika misingi ya umma maana yake ni kuwepo kwa RELIGIOUS TOLERANCE na siyo ABSENCE OF RELIGION.

Religious tolerance ndiyo maana huwa tuna siku za OFF kwa ajili ya sikukukuu za kidini za Eid na Christmass hata kama NCHI YETU HAINA DINI ( ila watu wake wana dini)
 
Kuishi katika misingi ya umma maana yake ni kuwepo kwa RELIGIOUS TOLERANCE na siyo ABSENCE OF RELIGION.

Religious tolerance ndiyo maana huwa tuna siku za OFF kwa ajili ya sikukukuu za kidini za Eid na Christmass hata kama NCHI YETU HAINA DINI ( ila watu wake wana dini)
UMMA unajumlisha yote hayo! Wanaofanya kazi hapo wengi wamezaliwa miaka ya kabla ya tisini? Unahisi miaka hyo kulikua na uzalishaji mkubwa wa wasomi ktk dini ya uislam? Sasa ni vp utegemee ratio iwe sawa? By the way ni ngumu kupata equal proportion kwa sababu recruitment haijabase kubalance proportions,ila ktk taaluma na vigezo vingi vingine visivyo changamana dini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
UDOM kwa muda mrefu ilikumbwa na tuhuma za udini. Sasa serikali inajaribu kuondoa hili tatizo lakini kuna upande unang'ang'ania maana ulinufaika na udini hapo awali.

Mbona UDSM ni ya miaka mingi ila ina kanisa moja na msikiti mmoja na hakuna fujo za udini. Wakristo madhehebu yote wanasali kwa kupokezana. Waislamu wanaswali as usual, sasa why UDOM?

Kuna watu walitaka dini fulani ihodhi hicho chuo siyo!

Kwanza serikali haijakataa ujenzi wa msikiti isipokuwa taratibu hazijafatwa.

Kila MTU amuheshimu mwenzake.

Tanzania ni ya wote, na UDOM siyo ya dini Fulani.
 
Kuna wakati unaweza kumhamisha mtu au kumbadilishia majukumu yake kwa lengo la kumwepushia hatari yeye mwenyewe au jamii anayoitumikia. Kama hakuna stahiki zake alizodhulumiwa basi nia hiyo ni njema kuliko kusubiri tatizo liwe kubwa.

Hata hivyo mijadala inayohusu dini inahitaji umakini,weledi na kuzingatia mipaka.
Sisi sote ni jamii moja na tunastahii Kupendana na Kuheshimu Imani ya kila mmoja.

Sent using Jamii Forums mobile app
 


My take:

Huu mgogoro usipotafutiwa ufumbuzi wa hekima utaleta impression mbaya sana katika jamii.

Vijana wa Kiislamu na Wafanyakazi waislamu wachache waliobakishwa pale UDOM baada ya wenzao kuhamishwa watakuwa na grievances na dhana mbaya sana juu ya uongozi wa chuo na serikali na hivyo kuzalisha watu wenye hisia za kutilia mashaka mifumo ya nchi hii.

Kibaya zaidi ile dhana ya Mfumo Kristo kwamba ndo unatawala nchi hii inaweza kupata legitimacy katika fikra za wasomi hawa wa Kiislamu. Kama wasomi watatoka katika vyuo huku wakiamini kuwa kweli kiba mfumo Kristo katika nchi hii basi ni hatari sana huko mbeleni maana kikawaida tulitegemea Taifa lingewatumia hawa wasomi kuelewesha wenzao kuwa hiki kitu hakipo.

Kwa Tanzania Taasisi ya Ponda ni Taasisi inayosikilizwa sana na waislamu nchini na Sheikh Ponda ni kiongozi wa Waislamu mwenye kuheshimiwa sana na Waislamu na hili tamko litasambaa nchinini katika misikiti yote na kuleta impact pengine isiyotakiwa katika nchi yetu.

Ni muhimu kwa serikali kupitia Waziri wa Elimu mama Ndalichako kuingilia kati na kulitatua suala hili maana Linagusa hisia za Waislamu nchini.

Suala hili lilikuwa raised hata mbele ya mheshimiwa rais alipoongea na viongozi wa dini majuzi

Hekima kubwa inahitajika katika suala hili.
**** mashekhe wenye akili na busara alafu kuna mashekhe watia fujo fujo tu.

Shekhe ponda ni mtu wa fujo,anaweza akawakusanya waislamu waandamane kwa jambo la kijinga na waislamu wakapigwa hapo na kuuwawa kwa jambo ambalo hata wangelipata basi mambo yangekuwa vile vile kama mwanzo.

Huyu shekhe ponda ni muislamu flani mwana siasa siasa hivi,mjanja mjanja hivi,anatia fujo na kuwatilia fujo waislamu waanze fujo

Uislamu sio dini ya kipumbavu namna hii,mgogoro sijui wa huko UDOM chuo kinamilikiwa na waislamu au serikali?
Mimi nashangaa sana sisi waislamu yutakua lini?

Hivi mtu mfano akakuambia nilikujengea msikiti sasa nautaka mwenyewe usisali humo wewe unang'ang'ania wa kwako?
Amekukataza kusali ama amekukataza kusalia kwenye msikiti ambae ulikuwa katika himaya yake?

Juzi kuna mtu wangu anasoma chuo cha mwalim nyerere pale kigamboni dar,kanipa malalamiko kwamba msikiti ambao wanaswalia hapo chuoni wameutaka wenyewe utawala wa chuo,mimi nikamuuliza kuna kanisa humo ndani?
Akaniambia hakuna.

Nikamuuliza tena mkataba hapo mwanzo ilikuwa ni eneo la msikiti au chuo tu kilijitolea na katika ramani hapakuwa na plan pajengwe msikiti?
Akaniambia chuo tu walisaidia waislamu wajenge msikiti kwa Muda na sio kwamba ndo iwe ya kudumu.
Mimi nikamuambia sasa hapo mnataka kugombana nini na ilhali wameitaka sehemu yao na wala nyie hawajawakatazeni kusali ?

Ananiambia kuna waislamu wanasema tusikubali tuandike barua majuu.
Nikamuambia hao ni waislamu wajinga wasiojielewa na kuuelewa uislamu wao unasema vipi,acha wachukue eneo lao alafu kama ikibidi atumwe mtu mwenye busara zake akaombe tena,na sio fujo fujo tu.

Sasa waislamu wengine kama akina ponda wanaonekana mashekhe kumbe ni watu watia fujo,wanataka kuchafua amani kwa sababu ambazo hata sio za maana kabisa

Kuna mwingine alikuwa anaitwa Ilunga,ALLAH AMREHEMU NA AMSAMEHE YEYE NA SISI huyo naye alikuwa na sera kama za ponda,jambo dogo mfumo kristo matokeo yake walikuwa wakiwahamasisha watu kuandamana,wanapigwa wanakufa kwa sababu ya msahafu kukojolewa.
Sasa kati ya kukojolewa msahafu na kufa lipi kubwa hapo ambalo linapaswa likingwe lisitokee?

Kwa kweli nyie waislamu mlioko mavyuoni usomeni uidlamu wenu,msiwasikilize mashekhe watia fujo na watu waliokuwa wanasiasa siasa wajanja wajanja.

Mtakosa mlichofuata kwa sababu za kijinga.
 
Uhamisho wao unaonyesha kuna dhana ya "dini" zao kuwa sababu ya uhamisho wao!.
Haiwezekani ukahamisha watu 11 halafu 100% ya hao uliowahamisha wakawa wa dini moja then ukaja kusema kuwa hakuna kitu behind!

Utakuwa unadanganya!
Na kinachokufanya uone kuna udini ni huo udini uliokujaa mkuu.

Ni sawa na mimi nianze kuona fulani amefukuzwa kazi kwasababu ni Mhaya,hapo kati ya mimi na aliyemfuta kazi ni yupi mkabila?
 
UMMA unajumlisha yote hayo! Wanaofanya kazi hapo wengi wamezaliwa miaka ya kabla ya tisini? Unahisi miaka hyo kulikua na uzalishaji mkubwa wa wasomi ktk dini ya uislam? Sasa ni vp utegemee ratio iwe sawa? By the way ni ngumu kupata equal proportion kwa sababu recruitment haijabase kubalance proportions,ila ktk taaluma na vigezo vingi vingine visivyo changamana dini.

Sent using Jamii Forums mobile app

Kabla ya Uhuru ni kweli Waislamu walikuwa nyuma nyuma mno kielimu kulinganisha na Wakiristo.

Hii ilitokana na kwamba Serikali ya Kikoloni kwanza haikuwa na Interest ya kutoa elimu kubwa kwa raia wote lakini Ikalipa privilege Kanisa kutoa huduma za Shule. Kwa kanisa hii ilikuwa ni opportunity kubwa sana kwake kwa sababu ilikuwa ni TOOL ya Evangelism( Kusambaza Ukiristo kwa Watanganyika maporini huko).

Kwa hiyo Kanisa likajenga shule nyingi, na ili usome katika hizo shule ilibidi mtoto Abatizwe au Ajifanye ni Mkiristo. Wazee wa Kiislamu wengi wao hili la kubatizwa watoto wao liliwakwaza kwa hiyo hawakukubali watoto kubatizwa au Kuchukua majina ya Kikiristo.

Moja ya Sababu iliyowafanya Waislamu wazipokee harakati za Uhuru ni hili suala la Kunyimwa fursa ya Kielimu, Waislamu wa Tanganyika waliunda hadi chama walichokiita AMNUT ( All Muslims ...party) na lengo la Chama hicho ilikuwa ni kwamba Tucheleweshe uhuru mpaka waislamu nao wasome walingane na wakiristo ndo tupewe nchi!. In contrast Waislamu walio wengi waliunga mkono TANU kwa imani kuwa tukishajitawala hili gepu litapungua chini ya serikali mpya ya kizalendo.

Alipoingia Nyerere alijitahidi kadri ya uwezo wake, na mwaka 1985 katika moja ya speech zake za kuaga alijisifu kuwa Tumepiga hatua katika suala la Elimu na kwamba sasa hivi hana hofu anapotaka kuteua wasaidizi waje wa kumsaidia kazi maana wasomi wapo dini zote!!. Hiyo ilikuwa mwaka 1985

Hii ikuonyeshe kuwa Waislamu walilipokea kwa dhati suala la elimu baada ya uhuru.

Hata hivyo limekuwa suala la kushangaza kidogo kuwa Waislamu wanaoanza primary school kwa wingi sana hata katika mikoa yenye waislamu wengi, Wingi wao bado haujawa reflected katika vyuo vikuu, Wapo Waislamu waliosoma wengi kulinganisha na miaka ya nyuma, lakini proportion yao katika elimu za juu haiakisi proportion yao katika Taifa.

Kumbuka kwa mujibu wa Sensa ya Mkoloni ya mwaka 1954, Waislamu nchi hii walikuwa wengi kuliko Wakiristo, kwa hiyo ni sahihi kabisa kusema wakati Tanganyika inapata uhuru mwaka 1961 nchi hii ilikuwa na MAJORITY waislamu.

Kuna Mtafiti bwana Ernest Chahali anaendesha Utafiti katika masomo yake ya PhD katika suala hili la masuala ya Waislamu katika elimu.

Unaweza kumsikiliza katika Podcast yake hapa akijaribu kuelezea mtizamo wake hapa:

Uchambuzi Kuhusu Matokeo Ya Kidato Cha Nne
 
Uhamisho wao unaonyesha kuna dhana ya "dini" zao kuwa sababu ya uhamisho wao!.
Haiwezekani ukahamisha watu 11 halafu 100% ya hao uliowahamisha wakawa wa dini moja then ukaja kusema kuwa hakuna kitu behind!

Utakuwa unadanganya!
it's plain to see kuwa hapa huu uhamisho sio sawa. Lakini nani atakubali hiyo fact. Kutakuwa na lame excuses zaidi ya elfu ku justify hilo jambo.
 
Kwamba..."tunataka msikiti ujengwe...na serikali itoe tamko"....

Tamko limeshatolewa na Mama Kabaka.

Msikiti lazima ujengwe UDOM....ulazima huu unatoka wapi?

Kabla ya hapo waliishi vipi wanajumuia wa UDOM?

Tusilete maswala ya imani katika taasisi za umma!

Hata wakristu, kuna ulazima upi wa wao kupewa eneo la kujenga mijumba ya ibada?

Acheni vyuo viwe mahali ambapo watu WANAPASWA KUFAHAMU kwa kupata maarifa na si maswala ya kujengana imani.
 
Niliwahi kusikia kwa chini chini Udom kuna mambo ya udini miaka iliyopita, sasa nini tena wakati ule ni wakristo walikuwa wanalalamika sasa ni Waislam kuna nini UDOM?
 
**** mashekhe wenye akili na busara alafu kuna mashekhe watia fujo fujo tu.

Shekhe ponda ni mtu wa fujo,anaweza akawakusanya waislamu waandamane kwa jambo la kijinga na waislamu wakapigwa hapo na kuuwawa kwa jambo ambalo hata wangelipata basi mambo yangekuwa vile vile kama mwanzo.

Huyu shekhe ponda ni muislamu flani mwana siasa siasa hivi,mjanja mjanja hivi,anatia fujo na kuwatilia fujo waislamu waanze fujo

Uislamu sio dini ya kipumbavu namna hii,mgogoro sijui wa huko UDOM chuo kinamilikiwa na waislamu au serikali?
Mimi nashangaa sana sisi waislamu yutakua lini?

Hivi mtu mfano akakuambia nilikujengea msikiti sasa nautaka mwenyewe usisali humo wewe unang'ang'ania wa kwako?
Amekukataza kusali ama amekukataza kusalia kwenye msikiti ambae ulikuwa katika himaya yake?

Juzi kuna mtu wangu anasoma chuo cha mwalim nyerere pale kigamboni dar,kanipa malalamiko kwamba msikiti ambao wanaswalia hapo chuoni wameutaka wenyewe utawala wa chuo,mimi nikamuuliza kuna kanisa humo ndani?
Akaniambia hakuna.

Nikamuuliza tena mkataba hapo mwanzo ilikuwa ni eneo la msikiti au chuo tu kilijitolea na katika ramani hapakuwa na plan pajengwe msikiti?
Akaniambia chuo tu walisaidia waislamu wajenge msikiti kwa Muda na sio kwamba ndo iwe ya kudumu.
Mimi nikamuambia sasa hapo mnataka kugombana nini na ilhali wameitaka sehemu yao na wala nyie hawajawakatazeni kusali ?

Ananiambia kuna waislamu wanasema tusikubali tuandike barua majuu.
Nikamuambia hao ni waislamu wajinga wasiojielewa na kuuelewa uislamu wao unasema vipi,acha wachukue eneo lao alafu kama ikibidi atumwe mtu mwenye busara zake akaombe tena,na sio fujo fujo tu.

Sasa waislamu wengine kama akina ponda wanaonekana mashekhe kumbe ni watu watia fujo,wanataka kuchafua amani kwa sababu ambazo hata sio za maana kabisa

Kuna mwingine alikuwa anaitwa Ilunga,ALLAH AMREHEMU NA AMSAMEHE YEYE NA SISI huyo naye alikuwa na sera kama za ponda,jambo dogo mfumo kristo matokeo yake walikuwa wakiwahamasisha watu kuandamana,wanapigwa wanakufa kwa sababu ya msahafu kukojolewa.
Sasa kati ya kukojolewa msahafu na kufa lipi kubwa hapo ambalo linapaswa likingwe lisitokee?

Kwa kweli nyie waislamu mlioko mavyuoni usomeni uidlamu wenu,msiwasikilize mashekhe watia fujo na watu waliokuwa wanasiasa siasa wajanja wajanja.

Mtakosa mlichofuata kwa sababu za kijinga.
Duh ww ni katika waleeee waislam wasio jielewa kwanza ukishajenga tu msikiti hua sio mali yako tena mali ya Mungu mwenyewe pili kwani kudai haki za ki msingi kunaubaya gani waislam wanahaki ya kimaumbile kuswali swala5 hili haliwagusi wa upande wa pili kwani wao siku zao hua ni jmoc au jpili fungua akili yako kaka

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi taratibu za kuajiri huwa wanaangaliaga dini au VIGEZO vya muhusika?
Ratio ya wasomi ukuangalia Kwa hizi dini ni TOFAUT kabisa ...huyu jamaa enzi za jk slijambishwa Kwa jiwe atapotea mpk mfupa shauri yake jpm hapendi uchochez

Sent using Jamii Forums mobile app
 
'Shehe' Ponda atuambie tu sasa hivi highest bidder wake ni nani. Haya mengine ni mbwembwe tu.
 
Mimi nadhani Sheikh ponda ana hoja ya msingi. kama hakuna lingine lililo nyuma ya kuvunja mskiti, basi ana hoja za msingi katika tamko lake.
SWALI: Hivi Msikiti ulivunjwa na vibaka au serikali? Hiv wahadhiri walihamishwa na serikali au vibaka? Kwanini walihamishwa? Missile of the Nation enlighten me on that Missile of the Nation
 
Kuna uzi niliwahi kukuambia wewe ni muislamu Mkuu ukakana mara tatu kama Petro naona leo jogoo kawika umedhihirika waziwazi

Kwanini huwa mnahofu ya kujipambanua waziwazi badala yake mnajivika uhalisia usio wenu? Maana hili la msikiti huko udom umelishikia bango kwelikweli ili hali limeshawekwa sawa sasa wewe unakesha youtube kuangalia nani kalizungumzia ulileta humu kuendeleza mjadala ambao kimsingi umeshaisha

Mbona wakristo wao hatuwaoni wakilalamika ni nyie tu kila mara, ina maana kwa sasa wanafunzi hapo udom hawaswali? Au ni kusumbua tu, madarasa waliyopewa tumieni kwa ajili ya ibada allah atawasikia maana yeye ni mungu wa rehema kama aliweza kuwaruhusu kula nguruwe mkifikwa na dharula

( إِنَّمَا حَرَّمَ عَلَيْكُمُ الْمَيْتَةَ وَالدَّمَ وَلَحْمَ الْخِنزِيرِ وَمَا أُهِلَّ بِهِ لِغَيْرِ اللَّهِ ۖ فَمَنِ اضْطُرَّ غَيْرَ بَاغٍ وَلَا عَادٍ فَلَا إِثْمَ عَلَيْهِ ۚ إِنَّ اللَّهَ غَفُورٌ رَّحِيمٌ )

البقرة (173) Al-Baqara

Yeye amekuharimishieni mzoga tu na damu na nyama ya nguruwe na kilicho tajiwa, katika kuchinjwa kwake, jina la asiye kuwa Mwenyezi Mungu. Lakini aliye fikiwa na dharura bila ya kutamani wala kupita kiasi, yeye hana dhambi. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.

Atashindwaje kuwakubalia swala mkiswalia darasani!!

Sikiliza ndugu yangu, mimi nimetoa data na takwimu
Suala la mimi kuwa Myahudi, Mkiristo, Muislamu au Atheist halina mshiko hapa!

Mimi natetea haki ya yeyote ninayeoona anaonewa bila kujali dini yake, hivyo ndivyo moyo wangu ulivyo.

Sasa wewe kama unaniona eti siyo mfuasi wa YESU wa NAZARETH kwa kupinga kwangu uonevu na unyanyapaa dhidi ya ndugu zetu Waislamu basi pole ila nataka nikuhakikishie mimi ni Mfuasi wa YESU.

Wewe unadhani watu watampendaje YESU kama wale wanaojifanya Wamempokea wanatenda ubaguzi katika nafasi za utumishi tulizowapa watutumikie?

Yesu alisema mpende jirani yako, nami nawapenda Jirani zangu Waislamu!

Laiti wanayofanyiwa wao wangefanyiwa Wakiristo katika utawala wa Rais Muislam wewe usingepiga kelele humu JF na katika makanisa na vigango?

Ondoa upofu wewe tenda haki kwa binadamu wenzako, acha upofu wa UDINI
 
Acha chuki, kebehi na dharau mkuu, sisi sote ni Watanzania, angalia impact ya mustakbali wa Taifa letu, mshikamano wa kitaifa n.k!
Kuhamisha Waislamu watupu katika chuo kilichojaa watu wa imani zote kunapelekea dhana ya udini!
Huko walipohanishiwa kunanini kimepundua, kwahiyo taasisi ikitaka kuhamisha watu ianze kuangalia dini ziwe zimebalance, yani kama wamehamishwa watu kumi basi wawe tano tano maana wakizidi upande moja unaanza kulalamika na kuhamishwa tu kelele je wangefukuzwa? Achane kuhusisha kila kitu na udini kama watu wamekosa maslahi yao watumie sheria zilizopo kudai haki yao sio kila kitu kuweka udini

Sent using Jamii Forums mobile app
 


My take:

Huu mgogoro usipotafutiwa ufumbuzi wa hekima utaleta impression mbaya sana katika jamii.

Vijana wa Kiislamu na Wafanyakazi waislamu wachache waliobakishwa pale UDOM baada ya wenzao kuhamishwa watakuwa na grievances na dhana mbaya sana juu ya uongozi wa chuo na serikali na hivyo kuzalisha watu wenye hisia za kutilia mashaka mifumo ya nchi hii.

Kibaya zaidi ile dhana ya Mfumo Kristo kwamba ndo unatawala nchi hii inaweza kupata legitimacy katika fikra za wasomi hawa wa Kiislamu. Kama wasomi watatoka katika vyuo huku wakiamini kuwa kweli kiba mfumo Kristo katika nchi hii basi ni hatari sana huko mbeleni maana kikawaida tulitegemea Taifa lingewatumia hawa wasomi kuelewesha wenzao kuwa hiki kitu hakipo.

Kwa Tanzania Taasisi ya Ponda ni Taasisi inayosikilizwa sana na waislamu nchini na Sheikh Ponda ni kiongozi wa Waislamu mwenye kuheshimiwa sana na Waislamu na hili tamko litasambaa nchinini katika misikiti yote na kuleta impact pengine isiyotakiwa katika nchi yetu.

Ni muhimu kwa serikali kupitia Waziri wa Elimu mama Ndalichako kuingilia kati na kulitatua suala hili maana Linagusa hisia za Waislamu nchini.

Suala hili lilikuwa raised hata mbele ya mheshimiwa rais alipoongea na viongozi wa dini majuzi

Hekima kubwa inahitajika katika suala hili.


Nimejaribu kusoma pia kusikiliza hoja za shekhe Ponda juu ya kinachoitwa sakata la msikiti UDOM. Pamoja na kutoa pole kwa jamii ya kiislam kwa kupata usumbufu huu, mimi binafsi sijaona mgogoro zaidi ya watu ambao walishindwa kufuata sheria na kujaribu kufanya mambo ya kienyeji kwa kuruhusu taasisi za dini zijenge nyumba za ibada kwenye maeneo ya serikali.

Ilikuwa sahihi kwa uongozi wa UDOM kutenga eneo kwa ajili ya taasisi za dini ila haikuwa sahihi kuruhusu kila taasisi yenye uwezo wa kujenga ijenge. Ninachokijua ni kuwa UDOM wanawajibu wa kujenga Msikiti na Kanisa ili waumini wapate sehemu ya kuabudu, haya yamefanyika katika vyuo vikuu vingine ikiwepo Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) ambapo majengo hayo yamejengwa kwa utaratibu na kwa kifupi yanamilikiwa na vyuo. Itakuwa ni vurugu na fujo kama kila taasisi itapewa uhuru kujenga jengo watakalo, kwa mfano kuna utofauti mkubwa wa kimadhehebu hivi kweli kila dhehebu likiomba ruhusa ya kujenga itakuwa sawa? Uongozi wa UDOM kwa kiasi kikubwa ulivuka mipaka yake na huenda haukufikiria vizuri ndiyo maana baadae walijirudi. Kitu cha msingi hapa ni uongozi wa UDOM uharakishe kujenga nyumba za ibada kwa uwiano uliosawa wa kimadhehebu na kamwe wasiruhusi mtu au kikundi au Taasisi kujenga eneo la umma kwani udhibiti wake baadae utakuwa mgumu sana.
 
Basi msihusishe ukristu pambaneni na serikali wenyewe kama wenyewe au kuna mkristu aliyesema msikiti ubomolewe?

Sent using Jamii Forums mobile app

Kuna mtu kauliza je Kanisa nalo limejengwa pale?
Nimemjibu kuwa eneo la kujenga lipo kwenye ramani,Wakiristo watakapopata wasaa watajenga!

Hata hivyo kutokujengwa kwa kanisa hivi sasa kusiwakwaze Waislamu ambao wameshapata wasaa wa kuendeleza eneo lao walilolipata kwa kufuata taratibu zote!
 
Back
Top Bottom