JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,309
- 5,464
Mgogoro wa Hifadhi ya Ngorongoro kuhusu wakazi wanaoishi ndani ya eneo hilo umekuwepo kwa miaka mingi, kwa muda wote huo hakuna utatuzi rasmi wa nini kinatakiwa kifanyike.
Juzikati baada ya bwana Maulidi Kitenge na wenzake kutembelea hifadhi hiyo, alitoa ushauri wa Serikali kufanya mpango wa kuwahamisha wakazi waliopo ndani ya eneo hilo kwa sababu kadhaa.
Baadhi ya sababu ni kuwa mara kadhaa raia wanashambuliwa na wanyama wakali, hakuna huduma za kijamii na ongezeko la watu ni hatari kwa uhai wa hifadhi hiyo.
Kitenge alishambuliwa kila kona japo wapo ambao walimuunga mkono kuwa alichozungumza ni mtazamo wake kwa kile alichokiona.
Nimeingia chimbo kufuatilia kiundani kuna nini nyuma ya pazia katika sakata hilo, nilichobaini ni kuwa kuna nguvu kubwa sana baina ya pande mbili.
Kwanza ilinishangaza kuona kama kweli wananchi wapo katika mazingira magumu kama alivyosema Kitenge, inakuwaje wao hawataki kuondoka kwa kisingizio kuwa ‘wamezoea’.
Baada ya kuzungumza na vyanzo rasmi kadhaa kutoka kwenye hifadhi hiyo ni kuwa suala hilo la kuwahamisha ni ngumu sana kwa kuwa kuna nguvu kubwa ya ‘WAZITO’ nyuma ya pazia.
Sababu ya KWANZA ni kuwa WAZITO hao wa ndani ya nchi na wengine wa nje ya nchi wanaowasapoti wakazi wanaoishi ndani ya hifadhi (Wamasai) wana maslahi yao binafsi, ambayo yanawapa faida kuwa na ndiyo maana wanafanya juu chini kuwaunga mkono ili kuhakikisha hawaondoki.
Ile hoja kuwa idadi ya watu inavyoongezeka wanahatarisha uhai wa hifadhi hiyo, ikapingwa na wenyeji kuwa wamekuwepo eneo hilo kwa miaka mingi na hakuna kilichoharibika, nimeona siyo hoja ya msingi.
Kwa kawaida kila binadamu ana mahitaji yake, kadiri idadi ya watu inavyoongezeka ni wazi kuna mahitaji nayo yanatakiwa kuongezeka.
Wakati wanaanza kuishi hapo hifadhini miaka ya 1950 inaelezwa kuwa idadi ya wakazi ilikuwa elfu 8 au 9, lakini sasa hivi takwimu zisizo rasmi inadaiwa wapo zaidi ya watu laki mbili.
Tuwe wakweli, hii ni mbaya na wanapoelekea lazima kutakuwa na madhara ndani ya hifadhi.
Jiulize kama mtu ana nia njema ya kuwahamisha sehemu wanapokuwa hatarini kushambuliwa na wanyama, kupewa huduma za kijamii, kuboreshewa mahitaji binafsi, lakini yote bado wanakataa! Kwa nini? Kuna nini?
UPANDE WA PILI ni ule ambao wanaitazama kesho ipoje na maslahi ya taifa. Hao sasa ndiyo wapo upande wa aliozungumza Kitenge, lakini wanashambuliwa kinoma.
Ni kweli haiwezekani taifa liwepo bila wananchi, lakini hao wananchi hawawezi kuwepo bila kuwa na utaratibu maalum wa jinsi ya kuishi na kuendelea, na kama nchi lazima iwe na mfumo na utaratibu wa kufanya mambo kwa maslahi ya watu wake na maslahi ya taifa kwa jumla.
Juzikati baada ya bwana Maulidi Kitenge na wenzake kutembelea hifadhi hiyo, alitoa ushauri wa Serikali kufanya mpango wa kuwahamisha wakazi waliopo ndani ya eneo hilo kwa sababu kadhaa.
Baadhi ya sababu ni kuwa mara kadhaa raia wanashambuliwa na wanyama wakali, hakuna huduma za kijamii na ongezeko la watu ni hatari kwa uhai wa hifadhi hiyo.
Kitenge alishambuliwa kila kona japo wapo ambao walimuunga mkono kuwa alichozungumza ni mtazamo wake kwa kile alichokiona.
Nimeingia chimbo kufuatilia kiundani kuna nini nyuma ya pazia katika sakata hilo, nilichobaini ni kuwa kuna nguvu kubwa sana baina ya pande mbili.
Kwanza ilinishangaza kuona kama kweli wananchi wapo katika mazingira magumu kama alivyosema Kitenge, inakuwaje wao hawataki kuondoka kwa kisingizio kuwa ‘wamezoea’.
Baada ya kuzungumza na vyanzo rasmi kadhaa kutoka kwenye hifadhi hiyo ni kuwa suala hilo la kuwahamisha ni ngumu sana kwa kuwa kuna nguvu kubwa ya ‘WAZITO’ nyuma ya pazia.
Sababu ya KWANZA ni kuwa WAZITO hao wa ndani ya nchi na wengine wa nje ya nchi wanaowasapoti wakazi wanaoishi ndani ya hifadhi (Wamasai) wana maslahi yao binafsi, ambayo yanawapa faida kuwa na ndiyo maana wanafanya juu chini kuwaunga mkono ili kuhakikisha hawaondoki.
Ile hoja kuwa idadi ya watu inavyoongezeka wanahatarisha uhai wa hifadhi hiyo, ikapingwa na wenyeji kuwa wamekuwepo eneo hilo kwa miaka mingi na hakuna kilichoharibika, nimeona siyo hoja ya msingi.
Kwa kawaida kila binadamu ana mahitaji yake, kadiri idadi ya watu inavyoongezeka ni wazi kuna mahitaji nayo yanatakiwa kuongezeka.
Wakati wanaanza kuishi hapo hifadhini miaka ya 1950 inaelezwa kuwa idadi ya wakazi ilikuwa elfu 8 au 9, lakini sasa hivi takwimu zisizo rasmi inadaiwa wapo zaidi ya watu laki mbili.
Tuwe wakweli, hii ni mbaya na wanapoelekea lazima kutakuwa na madhara ndani ya hifadhi.
Jiulize kama mtu ana nia njema ya kuwahamisha sehemu wanapokuwa hatarini kushambuliwa na wanyama, kupewa huduma za kijamii, kuboreshewa mahitaji binafsi, lakini yote bado wanakataa! Kwa nini? Kuna nini?
UPANDE WA PILI ni ule ambao wanaitazama kesho ipoje na maslahi ya taifa. Hao sasa ndiyo wapo upande wa aliozungumza Kitenge, lakini wanashambuliwa kinoma.
Ni kweli haiwezekani taifa liwepo bila wananchi, lakini hao wananchi hawawezi kuwepo bila kuwa na utaratibu maalum wa jinsi ya kuishi na kuendelea, na kama nchi lazima iwe na mfumo na utaratibu wa kufanya mambo kwa maslahi ya watu wake na maslahi ya taifa kwa jumla.