Mgogoro Hifadhi ya Ngorongoro kuna siri nzito. Nani wapo nyuma ya Wamasai?

Mkuu hizi agenda watu hawasukumi bure... kuna pesa nyingi sana watu wanavuta kutoka kwa foundations mbalimbali duniani.

Angalia NGO ya Maria Sarungi ililipewa pesa kiasi gani mwaka 2018

1644525727493.png


Unaweza kujikuta unasukuma gari la wenzako bila kujua. Ndio maana watu wengi mtandaoni wakianza kupiga kelele kuhusu jambo moja wanageuka kama makasuku, maneno yaleyale na inawezakana yanaandikwa na mtu mmoja
 
Hao wanaopinga kutolewa kwa wamasai ni Wakenya wanaotaka kuiua Ngorongoro ili vivutio vinavyoleta ushindani na vile vya Kenya vipungue Tanzania. Bahati mbaya wamasai wa kenya ni sawa sawa na hawa wa Tanzania hivyo inaweza kuwa ni mamluki wao pia.
Ni kweli kabisa mkuu. Kuna tetesi kuwa hii hifadhi yetu inahujumiwa
 
Mgogoro wa Hifadhi ya Ngorongoro kuhusu wakazi wanaoishi ndani ya eneo hilo umekuwepo kwa miaka mingi, kwa muda wote huo hakuna utatuzi rasmi wa nini kinatakiwa kifanyike.

Juzikati baada ya bwana Maulidi Kitenge na wenzake kutembelea hifadhi hiyo, alitoa ushauri wa Serikali kufanya mpango wa kuwahamisha wakazi waliopo ndani ya eneo hilo kwa sababu kadhaa.

Baadhi ya sababu ni kuwa mara kadhaa raia wanashambuliwa na wanyama wakali, hakuna huduma za kijamii na ongezeko la watu ni hatari kwa uhai wa hifadhi hiyo.

Kitenge alishambuliwa kila kona japo wapo ambao walimuunga mkono kuwa alichozungumza ni mtazamo wake kwa kile alichokiona.

Nimeingia chimbo kufuatilia kiundani kuna nini nyuma ya pazia katika sakata hilo, nilichobaini ni kuwa kuna nguvu kubwa sana baina ya pande mbili.

Kwanza ilinishangaza kuona kama kweli wananchi wapo katika mazingira magumu kama alivyosema Kitenge, inakuwaje wao hawataki kuondoka kwa kisingizio kuwa ‘wamezoea’.

Baada ya kuzungumza na vyanzo rasmi kadhaa kutoka kwenye hifadhi hiyo ni kuwa suala hilo la kuwahamisha ni ngumu sana kwa kuwa kuna nguvu kubwa ya ‘WAZITO’ nyuma ya pazia.

Sababu ya KWANZA ni kuwa WAZITO hao wa ndani ya nchi na wengine wa nje ya nchi wanaowasapoti wakazi wanaoishi ndani ya hifadhi (Wamasai) wana maslahi yao binafsi, ambayo yanawapa faida kuwa na ndiyo maana wanafanya juu chini kuwaunga mkono ili kuhakikisha hawaondoki.

Ile hoja kuwa idadi ya watu inavyoongezeka wanahatarisha uhai wa hifadhi hiyo, ikapingwa na wenyeji kuwa wamekuwepo eneo hilo kwa miaka mingi na hakuna kilichoharibika, nimeona siyo hoja ya msingi.

Kwa kawaida kila binadamu ana mahitaji yake, kadiri idadi ya watu inavyoongezeka ni wazi kuna mahitaji nayo yanatakiwa kuongezeka.

Wakati wanaanza kuishi hapo hifadhini miaka ya 1950 inaelezwa kuwa idadi ya wakazi ilikuwa elfu 8 au 9, lakini sasa hivi takwimu zisizo rasmi inadaiwa wapo zaidi ya watu laki mbili.

Tuwe wakweli, hii ni mbaya na wanapoelekea lazima kutakuwa na madhara ndani ya hifadhi.

Jiulize kama mtu ana nia njema ya kuwahamisha sehemu wanapokuwa hatarini kushambuliwa na wanyama, kupewa huduma za kijamii, kuboreshewa mahitaji binafsi, lakini yote bado wanakataa! Kwa nini? Kuna nini?

UPANDE WA PILI ni ule ambao wanaitazama kesho ipoje na maslahi ya taifa. Hao sasa ndiyo wapo upande wa aliozungumza Kitenge, lakini wanashambuliwa kinoma.

Ni kweli haiwezekani taifa liwepo bila wananchi, lakini hao wananchi hawawezi kuwepo bila kuwa na utaratibu maalum wa jinsi ya kuishi na kuendelea, na kama nchi lazima iwe na mfumo na utaratibu wa kufanya mambo kwa maslahi ya watu wake na maslahi ya taifa kwa jumla.
wamasai wanatumika kuweka mifugo ya vigogo tu vigogo wan ngo'mbe kibao zinakul nafasi za hifadhi,ngo'mbe laki 8 huku kati ya hiyo no 3% tu ndio za wamasai.
 
Kwani wamasai hawaishi kwa muingiliano na wanyama katika mbuga zingine zozote ila Ngorongoro crater hadi iwe unique factor ya watu kwenda kuitembelea ??...

Kwa ukubwa wa Ngorongoro na ikolojia yake unadhani hii haitoshi kuwafanya watu kuitembelea ??..

Leo tukisema tukimege kipande cha ruaha au mikumi ili kitumike kwa shughuli za kibinadamu bado kuna serengeti au selous inayotoa same experience Je, tukiiweka Ngorongoro crater hatarini kuna option gani nyingine tuliyonayo kui_replace
tatizo siyo wamasai bali kuna vigogo wameweka mifugo kwenye Hitadhi wakiwatumia wamasai.
 
Sasa kama hauna taarifa sahihi inafaa kabisa usiandike kitu. Ngorongoro Conservation Area ndio ilianzishwa miaka hiyo. To be precise ni mwaka 1959.

Lakini Maasai hatujaanza kuishi Ngorongoro miaka hiyo mkuu tumekuwepo since time immemorial.

Sasa mnaotaka tuondoke inabidi na sisi tuhoji kwanini hamuondoki huko mnapoishi.
It's a matter of time mtatoka tu mtake msitake....watu laki 2 mnatoa wapi kuni za kupikia kila siku? Kama sio kuharibu mazingira? Msituletee habari ya miaka 70 iliyopita!
 
Ni kweli kabisa mkuu. Kuna tetesi kuwa hii hifadhi yetu inahujumiwa
Hii hifadhi inahujumiwa kabisa na ni rahisi kufanya hivyo kutokana na umbo lake na udogo wake ukilinganisha na Serengeti iliyopakana na Masai Mara. Nilifanya utafiti kidogo ndani ya hifadhi hii nikaona kuwa hata mimea imeanza kuota ambayo sio mimea ya asili, sasa unajiuliza wanyama wataendelea kuwepo pale kwa hali hii? Je ni nani ameleta mbegu hizi kama sio hawa binadamu wema na wenye nia mbaya wanaojificha nyuma ya sheria ya kikoloni? Hivi sisi Tanzania si tulipinga sheria ya kikoloni ya kugawa mpaka ziwa Nyasa? sasa inakuwaje huku tunafumbia macho mbuga ambayo inapata tuzo za utalii za kimataifa?
ANALYSIS
Tanzania yenye eneo kubwa 945k sq km ni zaidi ya eneo ukijumlisha Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda 875k sq km. Population ya Tanzania ni 60m lakini ya Kenya 54m, Uganda 46m, Rwanda 13m na Burundi 12m inafanya jumla kuwa 125m. sasa ukiondoa 30% ya ardhi ya Tanzania ambayo ni hifadhi na mapori ya akiba, population density ya Tanzania inakuwa 91 people per sq km, wakati ya Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi kwa pamoja bila kuondoa hifadhi na mapori ya akiba ni 143 people per sq km. Hivyo wenzetu wana pressure ya maeneo kuliko sisi. ndio maana mbuga zetu zimebaki bora kwa sababu hazina muingiliano mkubwa na watu. sasa upenyo uliopo NCAA ndio wanataka kuutumia kutudhoofisha, tuamke!
RECOMMENDATION
Sheria ya kuruhusu makazi ndani ya Ngorongoro ifanyiwe mrekebisho ili wakaazi ndani ya NCAA wahamishwe kisheria, kwa vyovyote vile zoezi litapingwa lakini serikali ina mkono mrefu izuie kuhujumiwa.
 
Wizara ya Maliasili iharakishe kupitia sheria ya Mamlaka ya Ngorongoro ili ikipendeza Wamasai wahamishwe ili kuiacha mamlaka ya ngorongoro iendelee kubaki kama urithi wa Taifa.
 
Mkuu hizi agenda watu hawasukumi bure... kuna pesa nyingi sana watu wanavuta kutoka kwa foundations mbalimbali duniani.

Angalia NGO ya Maria Sarungi ililipewa pesa kiasi gani mwaka 2018

View attachment 2115332

Unaweza kujikuta unasukuma gari la wenzako bila kujua. Ndio maana watu wengi mtandaoni wakianza kupiga kelele kuhusu jambo moja wanageuka kama makasuku, maneno yaleyale na inawezakana yanaandikwa na mtu mmoja
Kwa hiyo unaamini katika kutetewa? Huwezi kujitetea? Kama wewe huwezi kujitetea, ni wewe. Wengine wanaweza bila kutegemea hizo NGOs.
 
Kitenge ni nani? Kuna watu wenye akili na elimu waliokwisha kuandika mengi kuhusu hili suala na siyo huyo Kitenge kanjanja anayechumia tumbo lake bila haya.
Kina nani hao wenye akili na elimu ambao hayo maandiko yao mengi waliyoyaandika yalikubaliana na uharibifu wa mazingira unaoendelea katika kreta?
 
Kina nani hao wenye akili na elimu ambao hayo maandiko yao mengi waliyoyaandika yalikubaliana na uharibifu wa mazingira unaoendelea katika kreta?
Wewe umewekeza akili yako kuwa uharibu wa mazingira unasababishwa na wamasai tu. Ndiyo maana nikasema ingefaa zaidi mkasoma hizo research zilizofanyika na siyo nyie mnaozungumza kama kasuku tu kama alivyo huyo Kitenge mwenye uwezo wa kuzungumza maneno kama amemeza tape recorder bila kutumia akili.
 
Sasa ukisema Ngorongoro ni world heritage inamaana na kila kilichopo hapo ikiwemo Wamasai.

Moja ya vitu unique na vinavyoipa hiyo hadhi Ngorongoro ni ule muingiliano kati ya Mmasai na maliasili. Hiyo ni sifa moja wapo. Sasa ukitutoa unakuwa umeharibu.
Kwa hiyo population yenu ikifika 2million muachwe tu muishi Ngorongoro ?
 
Sasa ukisema Ngorongoro ni world heritage inamaana na kila kilichopo hapo ikiwemo Wamasai.

Moja ya vitu unique na vinavyoipa hiyo hadhi Ngorongoro ni ule muingiliano kati ya Mmasai na maliasili. Hiyo ni sifa moja wapo. Sasa ukitutoa unakuwa umeharibu.
Nadhani tatizo kubwa ni ongezeko ambalo linapunguza nafasi za kukaa. Jinsi watu wanavyoongezeka na pia mifugo kuongezeka basi wanyama pori wanaanza kupotea. Kama serkali ina mahali pa kuwapeleka wafugaji na mifugo yao nadhani itakuwa vizuri. Inatakiwa ikubukwe kuwa hadi sasa wamasai ni watu wanaofaidi sheria ya TZ wa ardhi kuwa ya umma. Sasa hivi wamasai wengi wametapakaa TZ nzima. Huko wanakokwenda ni TZ na hawabughudhiwi, lakini wao kudai kuwa hapo ni kwao toka enzi wanasahau kuna uwezekano wa wao kupewa sehemu. Kwa nini wanakataa kuhama, kama kuna sehemu mbadala. Mbona WaTZ wengine huhama kupisha ujenzi wa shule, viwanja vya ndege, n.k.? Kwani hao wanaohama hawakuwa na haki na sehemu hizo!!!
 
Mgogoro wa Hifadhi ya Ngorongoro kuhusu wakazi wanaoishi ndani ya eneo hilo umekuwepo kwa miaka mingi, kwa muda wote huo hakuna utatuzi rasmi wa nini kinatakiwa kifanyike.

Juzikati baada ya bwana Maulidi Kitenge na wenzake kutembelea hifadhi hiyo, alitoa ushauri wa Serikali kufanya mpango wa kuwahamisha wakazi waliopo ndani ya eneo hilo kwa sababu kadhaa.

Baadhi ya sababu ni kuwa mara kadhaa raia wanashambuliwa na wanyama wakali, hakuna huduma za kijamii na ongezeko la watu ni hatari kwa uhai wa hifadhi hiyo.

Kitenge alishambuliwa kila kona japo wapo ambao walimuunga mkono kuwa alichozungumza ni mtazamo wake kwa kile alichokiona.

Nimeingia chimbo kufuatilia kiundani kuna nini nyuma ya pazia katika sakata hilo, nilichobaini ni kuwa kuna nguvu kubwa sana baina ya pande mbili.

Kwanza ilinishangaza kuona kama kweli wananchi wapo katika mazingira magumu kama alivyosema Kitenge, inakuwaje wao hawataki kuondoka kwa kisingizio kuwa ‘wamezoea’.

Baada ya kuzungumza na vyanzo rasmi kadhaa kutoka kwenye hifadhi hiyo ni kuwa suala hilo la kuwahamisha ni ngumu sana kwa kuwa kuna nguvu kubwa ya ‘WAZITO’ nyuma ya pazia.

Sababu ya KWANZA ni kuwa WAZITO hao wa ndani ya nchi na wengine wa nje ya nchi wanaowasapoti wakazi wanaoishi ndani ya hifadhi (Wamasai) wana maslahi yao binafsi, ambayo yanawapa faida kuwa na ndiyo maana wanafanya juu chini kuwaunga mkono ili kuhakikisha hawaondoki.

Ile hoja kuwa idadi ya watu inavyoongezeka wanahatarisha uhai wa hifadhi hiyo, ikapingwa na wenyeji kuwa wamekuwepo eneo hilo kwa miaka mingi na hakuna kilichoharibika, nimeona siyo hoja ya msingi.

Kwa kawaida kila binadamu ana mahitaji yake, kadiri idadi ya watu inavyoongezeka ni wazi kuna mahitaji nayo yanatakiwa kuongezeka.

Wakati wanaanza kuishi hapo hifadhini miaka ya 1950 inaelezwa kuwa idadi ya wakazi ilikuwa elfu 8 au 9, lakini sasa hivi takwimu zisizo rasmi inadaiwa wapo zaidi ya watu laki mbili.

Tuwe wakweli, hii ni mbaya na wanapoelekea lazima kutakuwa na madhara ndani ya hifadhi.

Jiulize kama mtu ana nia njema ya kuwahamisha sehemu wanapokuwa hatarini kushambuliwa na wanyama, kupewa huduma za kijamii, kuboreshewa mahitaji binafsi, lakini yote bado wanakataa! Kwa nini? Kuna nini?

UPANDE WA PILI ni ule ambao wanaitazama kesho ipoje na maslahi ya taifa. Hao sasa ndiyo wapo upande wa aliozungumza Kitenge, lakini wanashambuliwa kinoma.

Ni kweli haiwezekani taifa liwepo bila wananchi, lakini hao wananchi hawawezi kuwepo bila kuwa na utaratibu maalum wa jinsi ya kuishi na kuendelea, na kama nchi lazima iwe na mfumo na utaratibu wa kufanya mambo kwa maslahi ya watu wake na maslahi ya taifa kwa jumla.
Wewe jiulize nani yupo nyuma ya Kitenge na Balile?
Kwanini Fred Manongi anatumia fedha za mkopo wa Covid kuwalipa watu waeneze chuki dhidi ya Wamaasai?
Manongi must go. Manongi ajiuzulu au afukuzwe kazi.
 
Na wengi mnaoshadadia kudhalilishwa na kutweza kwa utu wa Wamaasai ni viajiriwa vya NCAA. Vinapenda mshahara tu badala ya kwenda kwao kulima tangawizi na kufuga kuku.
 
Back
Top Bottom