Habarini wana jamii wenzangu,
Tangu muda mrefu kumekuwapo na mjadala mrefu juu ya mfumuko wa bei, hasa kwa bidhaa za chakula. Wachambuzi wengi wamekuwa wakilaani jambo hili, hasa ndugu zetu waishio maeneo ya mjini.
Sasa mimi naomba kuelimishwa, kwani kila mfumuko wa bei ni hatari katika uchumi? Mbona Mimi naona kama huu mfumuko wa bei, hasa kwenye hizi bidhaa za chakula huku kijijini kwetu kama zinasisimua zaidi watu kulima. Maana baada ya kupanda bei ya vyakula mwaka huu mashamba ya mahindi yamekuwa mengi, kila shamba la mikorosho watu wamepiga matuta na kupanda mahindi.
Na kama factor nyingine hazitatokea, mbona naona kwa Kasi hii wafanya biashara wa mahindi watamtafuta wakumuuzia, maana asilimia kubwa ya watu watakuwa wamezalisha zaidi ya nusu ya mahitaji Yao. Sasa naomba munipe darasa, kwani kila mfumuko wa bei ni hatari kwenye uchumi, au Kuna namna fulani mfumuko wa bei una stimulate production?
Tangu muda mrefu kumekuwapo na mjadala mrefu juu ya mfumuko wa bei, hasa kwa bidhaa za chakula. Wachambuzi wengi wamekuwa wakilaani jambo hili, hasa ndugu zetu waishio maeneo ya mjini.
Sasa mimi naomba kuelimishwa, kwani kila mfumuko wa bei ni hatari katika uchumi? Mbona Mimi naona kama huu mfumuko wa bei, hasa kwenye hizi bidhaa za chakula huku kijijini kwetu kama zinasisimua zaidi watu kulima. Maana baada ya kupanda bei ya vyakula mwaka huu mashamba ya mahindi yamekuwa mengi, kila shamba la mikorosho watu wamepiga matuta na kupanda mahindi.
Na kama factor nyingine hazitatokea, mbona naona kwa Kasi hii wafanya biashara wa mahindi watamtafuta wakumuuzia, maana asilimia kubwa ya watu watakuwa wamezalisha zaidi ya nusu ya mahitaji Yao. Sasa naomba munipe darasa, kwani kila mfumuko wa bei ni hatari kwenye uchumi, au Kuna namna fulani mfumuko wa bei una stimulate production?