Hili ndilo jibu Mkuu
kwani hapa kuna watu wanataka MAUJIKO kuwa kazi ya kufanya chini ya ardhi (Jehanamu ni rahisi kivivyo) Mtenda Kaya alichotuelewesha ni kuwa hawa wenye Migodi km wa Bulyankulu wao ni pesa kwanza kwani mfanyakazi kapotea wanaambiwa kazi itaendelea na hata vyombo habari havitangazi bali ni Member wa JF
Mtendaji wa kaya wala usikate tamaa kutuhabarisha sisi watanzania kuhusu huyo mwenzetu na Wazazi wake waliofika hapo kumtafuta mtoto wao,
Hao wanaokupinga kuwa kufanya kazi Kaburini ni rahisi wana yao na usikute ni wale wanaopachikwa na maGodfather hivyo kuchota wakitakacho lakini walala hoi ni kila mahali ndio wanaoumia
huwezi kusema ukiwa kwenye kitengo cha Ventilation ni shushi wakati unaambiwa mwenzako kapotea
niheri wote kuwa na umoja ili Miner wote wawe katika maisha bora na salama
Kazi zisimame mpaka Wiliam apatikane huo wizi wa dhahabu ni hasara kwetu hakuna tunachoambulia
nawashangaa wanaonipinga...uhalisi wa mambo ni kwamba wawekezaji hawa wanatuua kabisa.....sasa hivi walisha anza kulipua miamba wakati kuna mtu alishapotea...maana yake nini
Mkuu sina haja ya kutafuta ujiko eneo hili tunapotumia majina yasiyo yetu na hata hapa hujanifahamu.Nimeingia hapo Buly kama Miner Trainee na trainers wangu akina Mwakitalu,Gibu na Caroly na uwezo na mipangi niliyokuwa nayo ndiyo iliyonipa nafasi ya kwenda long hole na si Convetional kwa Fritz Kussel kwenye ma-jack leg.Kuna watu wako hapo miaka nenda miaka rudi akiwemo yule Jumbo Operator anayeitwa Mhina ambaye naambiwa kaacha hivi karibuni alikuwepo Tangu TBRJ unawajua hawa wewe?Silicosis ni tatizo kwa watu waliokuwa na matatizo yao na wewe unaweza ukiwa makini...achana na pombe za Kakola na wanawake wa hapo piga kazi miaka yako mi 3 au mi 4 utakuwa umetoka.
Poleni watanzania na hasa Wachimbaji mnaoshuka ardhini
Mpaka saa hizi hakapatikana?
Niliuona uokoaji wa Wachimba mogodi huko Chile kwenye Luninga, wao walikuwa na vifaa vingi vya mawasiliano.
NI kweli hatujafikia huko ? ili kila anayeshuka shimoni akawa na mawasiliano?
Maana hakuna tofauti na Kaburi mtu kuzama peke yako
Tuna hofu kuu imetubini tuwe tunakaa ki makundi makundi tuwapo chini ya ardhi! kumbuka mgodi huu umefika mbali sana Hatua 3940 kutoka surface
Ni mbali mno kutoka usawa wa ardhi
Mpaka leo hii tarehe 28 may hawajafanikiwa kumpata! Kwakweli ni utata tupu hata hamu ya kazi imekwisha wakati huo huo meneja alisharuhusu uzalishaji kuendelea! Miner wote hatuna amani kabisa hata vyama vyetu TAMICO na NUMET navyo viko kimya..kwa mawazo yangu vyama hivi vingeshawishi mgomo mpaka mwenzetu atakapopatikana...Tatizo jingine kubwa Simu wanapewa ma supervisor tu na baadhi ya ma operator wa mashine kubwa kama Jumbo unakuta katika kundi la wafanyakazi 50 Kuna wanne au watano wenye Simu...wengine hatupewi simu tunapokuwa underground...pia kuna simu zimewekwa za mezani chini ya ardhi ambazo ziko mbali mno na maeneo ya kazi! Baba na mama wa ndugu aliyepotea wapo wamepewa hifadhi ndani ya mgodi....mpaka sasa hata serikali ya wilaya haijatamka lolote na hakuna chombo chochotw cha habari kimelipoti isipokuwa Jf pekee...NAWASILISHA
Hapa mi nailaumu serikali kwa kuwa sheria inasema linapotokea suala kama hili lazima mkaguzi wa migodi wa kanda (zonal mining officer) aje akague aandae ripoti ya kuufungia mgodi au kuruhusu uzarishaji kuendelea baada ya kujiridhisha.
Pia na nyie wafanyakazi hamna umoja mpaka leo hamna chama kimoja chenye nguvu mmegawanyika mara NUMET mara TAMICO hebu kuweni na organization moja yenye nguvu inayoweza kumtikisa kaburu.
Mpaka leo hii tarehe 28 may hawajafanikiwa kumpata! Kwakweli ni utata tupu hata hamu ya kazi imekwisha wakati huo huo meneja alisharuhusu uzalishaji kuendelea! Miner wote hatuna amani kabisa hata vyama vyetu TAMICO na NUMET navyo viko kimya..kwa mawazo yangu vyama hivi vingeshawishi mgomo mpaka mwenzetu atakapopatikana...Tatizo jingine kubwa Simu wanapewa ma supervisor tu na baadhi ya ma operator wa mashine kubwa kama Jumbo unakuta katika kundi la wafanyakazi 50 Kuna wanne au watano wenye Simu...wengine hatupewi simu tunapokuwa underground...pia kuna simu zimewekwa za mezani chini ya ardhi ambazo ziko mbali mno na maeneo ya kazi! Baba na mama wa ndugu aliyepotea wapo wamepewa hifadhi ndani ya mgodi....mpaka sasa hata serikali ya wilaya haijatamka lolote na hakuna chombo chochotw cha habari kimelipoti isipokuwa Jf pekee...NAWASILISHA
We jamaa unapotosha sana aisee na naamini kwa watu wengi ambao hawauui mgodi wanaweza kuwa wana-buy hizi cheap stories zako.Dhahabu si Zabibu kuwa utaenda kwenye mti ukachume ni lazima ifuatwe huko chini iliko.Buly si miongoni mwa migodi mirefu.Ulizia hao wasauzi ulionao hapo wakupe habari ya Anglo-Platinum huko Jberg ndo ujue kuna migodi mirefu.
Ni upuuzi kuamini kuwa kila mtu anapaswa kuwa na chombo cha mawasiliano na hakuna mgodi wa aina hiyo duniani ndo maana kuna dispatcher kwa ajili ya ku-coordinate mawasiliano huko underground na surface.Unaweza kuimajin kila mtu akiwa na mawasiliano hali ingekuwaje hapo?Na hili la kusema mgodi unazalisha wagonjwa 300 umelitoa wapi?Hii Tabia ya Kitanzania ya kulalama tu kwenye kila jambo.Huna umuhimu wa kukaa UG kwa miaka 10 you just need to work hard spend wisely then utatoka.Kama ungekuwa ni wa muda mrefu kidogo untakuwa unamfahamu Ray Lavouie mzee wa Ki-Canada ambaye kafanya UG for 40 years na Buly peke yake kafanya about 16 years mbona alitoka poa tu akiwa mzee kabisa?Usipotoshe watu JF bana.
Mh Nilisikia Juzi bungeni waktu wanaoka huko shimoni, wakirudi uraiani hawafikishi miaka 5 wanakufa, na rekodi inaonesha watu zaidi ya 300 wakiotoka kule washakufa. Ilikuwa wanaongelea inshu za NSSF na hifadhi za jamii.<br>Poleni sana wadau. Inauma manake kapotea kama ndege ya Malaysia MH370.
Mpaka leo hii tarehe 28 may hawajafanikiwa kumpata! Kwakweli ni utata tupu hata hamu ya kazi imekwisha wakati huo huo meneja alisharuhusu uzalishaji kuendelea! Miner wote hatuna amani kabisa hata vyama vyetu TAMICO na NUMET navyo viko kimya..kwa mawazo yangu vyama hivi vingeshawishi mgomo mpaka mwenzetu atakapopatikana...Tatizo jingine kubwa Simu wanapewa ma supervisor tu na baadhi ya ma operator wa mashine kubwa kama Jumbo unakuta katika kundi la wafanyakazi 50 Kuna wanne au watano wenye Simu...wengine hatupewi simu tunapokuwa underground...pia kuna simu zimewekwa za mezani chini ya ardhi ambazo ziko mbali mno na maeneo ya kazi! Baba na mama wa ndugu aliyepotea wapo wamepewa hifadhi ndani ya mgodi....mpaka sasa hata serikali ya wilaya haijatamka lolote na hakuna chombo chochotw cha habari kimelipoti isipokuwa Jf pekee...NAWASILISHA
We jamaa unapotosha sana aisee na naamini kwa watu wengi ambao hawauui mgodi wanaweza kuwa wana-buy hizi cheap stories zako.Dhahabu si Zabibu kuwa utaenda kwenye mti ukachume ni lazima ifuatwe huko chini iliko.Buly si miongoni mwa migodi mirefu.Ulizia hao wasauzi ulionao hapo wakupe habari ya Anglo-Platinum huko Jberg ndo ujue kuna migodi mirefu.
Ni upuuzi kuamini kuwa kila mtu anapaswa kuwa na chombo cha mawasiliano na hakuna mgodi wa aina hiyo duniani ndo maana kuna dispatcher kwa ajili ya ku-coordinate mawasiliano huko underground na surface.Unaweza kuimajin kila mtu akiwa na mawasiliano hali ingekuwaje hapo?Na hili la kusema mgodi unazalisha wagonjwa 300 umelitoa wapi?Hii Tabia ya Kitanzania ya kulalama tu kwenye kila jambo.Huna umuhimu wa kukaa UG kwa miaka 10 you just need to work hard spend wisely then utatoka.Kama ungekuwa ni wa muda mrefu kidogo untakuwa unamfahamu Ray Lavouie mzee wa Ki-Canada ambaye kafanya UG for 40 years na Buly peke yake kafanya about 16 years mbona alitoka poa tu akiwa mzee kabisa?Usipotoshe watu JF bana.
Wewe ni mpotoshaji mkubwa! habari ya waginjwa 300 raia mwema wameiandika sana halafu hata pale bungeni utafiti huo umetolewa! tatizo lako ni hicho cheo ulichopewa mgodini! unataka kuniambia hatua 3940 ni pafupi? usipende kuleta ujinga kwenye issue serious kuna watu hawapo bulyanhulu wanajua zaidi kuliko wewe.. fuatilia vyombo vya habari siyo kukalia magazeti ya ijumaa mbu mbu mbu wewe