Mfanyakazi wa Barrick apotelea mgodini

Mfanyakazi wa Barrick apotelea mgodini

Watanzania Tunakufa huku hawa Wazungu wakiondoka na Dhahabu na pia hawafanyi kazi ngumu kama wanazofanya hawa Watanzania lakini Mshahara wao mkubwa zaidi ya mara 3 wa hawa wafanyao kazi ngumu.
 
poleni kwa janga la kupotea kwa mfanyakazi mwenzenu je mkasa huo umetokea eneo gani la mgodi yaani zone gani na level ipi .maana ina tisha sana
 
Mpaka saa 2 usiku huu timu ya uokoaji haijafanikiwa kumpata mfanyakazi huyo! Peter Burger meneja mkuu wa kampuni amesema watatumia wataalam wa kimataifa...hali si shwari

Kuna level moja hapo inaitwa 1800 Kama (sijakosea) 44 east ilichomoka na raia kibao.msalimie Chundu
 
Sijajua kama kuna ukweli
Poleni watanzania na hasa Wachimbaji mnaoshuka ardhini
Mpaka saa hizi hakapatikana?
Niliuona uokoaji wa Wachimba mogodi huko Chile kwenye Luninga, wao walikuwa na vifaa vingi vya mawasiliano.
NI kweli hatujafikia huko ? ili kila anayeshuka shimoni akawa na mawasiliano?
Maana hakuna tofauti na Kaburi mtu kuzama peke yako
 
Watanzania Tunakufa huku hawa Wazungu wakiondoka na Dhahabu na pia hawafanyi kazi ngumu kama wanazofanya hawa Watanzania lakini Mshahara wao mkubwa zaidi ya mara 3 wa hawa wafanyao kazi ngumu.

Hiyo kawaida in normal life cku zote anaye2mia nguvu sana ndio hupata mshahara kiduchu kuliko yule atumiaye nguvu kidogo.
 
Hiyo kawaida in normal life cku zote anaye2mia nguvu sana ndio hupata mshahara kiduchu kuliko yule atumiaye nguvu kidogo.

Mkuu ndivyo ilivyo job anayopiga ticha ni kubwa na ngumu kuliko anayopiga mbunge lakini cheki gepu la mishahara yao ni kubwa kupindukia.!!
 
Hiyo kawaida in normal life cku zote anaye2mia nguvu sana ndio hupata mshahara kiduchu kuliko yule atumiaye nguvu kidogo.

anayetumia nguvu kidogo anatumia akili nyingi ndo maana malipo yake makubwa!
 
Jina lake anaitwa Fungwa William bado hajapatikana mpaka sasa! wakati huo huo meneja amelazimisha watu wapelekwe chini ya ardhi kufanya kazi wakati kuna ajali na bado hajaokolewa.
 
Poleni watanzania na hasa Wachimbaji mnaoshuka ardhini
Mpaka saa hizi hakapatikana?
Niliuona uokoaji wa Wachimba mogodi huko Chile kwenye Luninga, wao walikuwa na vifaa vingi vya mawasiliano.
NI kweli hatujafikia huko ? ili kila anayeshuka shimoni akawa na mawasiliano?
Maana hakuna tofauti na Kaburi mtu kuzama peke yako

Mgodi huu wa bulyanhulu umefika mbali sana! ajali nyingi ila hazitangazwi ni mwezi jana tu tumezika mwenzetu leo siku ya tatu mwenzetu hajulikani aliko
 
Nashukuru mungu maisha yangu ya mgodini miaka mitano ,nimetoka salama,tuombe mungu huyo miner mwenzetu apatikane akiwa hai,
 
Bado wanaendelea kutafuta bila mafaniko sijui itakuwaje kama hapatikani. Je wataendelea na ulipuaji kesho?
 
Haya sasa wadhungu wameanza kuwatoa waswahili naniii ili wapate dhahabu nyingi....
 
Back
Top Bottom