Kijana Fungwe Charles Wiliam aliwaaga wenzake majira ya saa 5 usiku akiwa night shift tarehe 18/05/2014,kuwa anaenda kujisaidia, kwa mazingira ya underground mtu anaweza kwenda kujisaidia sehemu yoyote yenye kificho kama drift,remuck au kwenye face,(hizo ni mining terminologies) tangu alipoondoka hadi mwisho wa shift hakuonekana hadi leo,hali ya sintofahamu imetanda mgodini,wafanyakazi hasa wa vitengo vinavyoshuka underground wana mashaka na hatima zao,wanaenda kazini wakiwa na hofu kuu,hakuna ajuaye mwenzao kaenda wapi! nguo zake zote na kitambulisho chake bado vipo,sheria za mgodi ni kuwa,mchimbaji yeyote anayeenda chini ya ardhi ni lazima aache kitambulisho chake juu,kama uthibitisho kuwa yupo chini,na hiyo ni kwa sababu za kiusalama,kitambulisho hicho ndo funguo wa kufungulia geti la kuu la kutoka nje,wazazi wa kijana huyo wapo mgodini hawajui hatima ya mtoto wao alipo,kampuni imeagiza mbwa kutoka south africa ili kusaidia ktk zoezi la kumtafuta kijana huyo ambaye dalili za kuwa hai ni asilimia 0%.