Level aliyopotelea mhanga inaitwa 4130 kuna madai tofauti kuhusu kupotea kwake,(1) mashine hatari kabisa iitwayo scoop na yenye nguvu za kutisha ilimgonga,na kisha operator wa mashine ile kumbeba ktk mashine na kisha kumtupa ktk shimo refu maarufu kwa jina la open hole ili kuficha ushahidi.(2)alipowaaga wenzake kuwa anaenda kujisaidia bila shaka kwa bahati mbaya mno akatumbukia ktk open hole ambayo ipo kama mita 20 tu kutoka pale alipokuwa na wenzake.(3)kachukuliwa na majini au mizimu,mimi ni mfanyakazi wa BARRICK kitengo cha chini ya ardhi,japokuwa wengi hawasadiki ila kule chini kuna mauzauza mengi sana,siku moja miezi miwili tu iliyopita saa 11:30 jioni nikiwa nimechelewa kutoka chini ya ardhi ktk level ile ile ya 4130 aliyopotelea mhanga,niliitwa na mtu asiyeonekana,sikuitika,na mahali pale watu wote walikuwa wametoka ilikuwa maeneo ya rockbreaker.