KakindoMaster
JF-Expert Member
- Dec 5, 2006
- 1,356
- 91
Wakuu mtanisamehe pale nitakapokuwa nimekosea unajua umri tena kumbukumbu zinapotea.
Wakati wa uongozi wa jenerali Mbona kuliwahitokea kutunishiana misuli kati ya Mkapa na Mboma katika kipindi ambacho Mboma alikaribia kustaafu. Nyepesi nyepesi zilisema ilikuwa ni mambo ya pesa(labda ndo hiyo Meremeta) ili kumpooza Mboma, vibali vya kuingiza sukari toka nje bila ushuru vilitolewa. Baada ya magazeti kuandika kuhusu utolewaji huo wa vibali na waziri wa fedha(Yona)bila kufuata taratibu wakaona watumie kofia ya jeshi, lakini ukweli ni kuwa matani ya sukari iliyoingizwa yalimnufaisha Mboma, kuanzia ushuru.
Nimekaa nikafikiri kwanini Mkapa amekuwa jeuri kwa kashfa zote hizi, kwanini JK amekaa kimya kuwachukulia hatua hawa majambazi,wakati nchi yake inateketea,kwanini viongozi wetu wanatuibia na kuja kutudanganya waziawazi kama akina Pinda, kwa nini wabunge wetu baadhi wako kimya na wengine wanatetea maafisadi? Hii gut na courage wanaitoa wapi? Nikagundua wanaitoa kwetu sisi wananchi. Yaani kwa kuibiwa kote huku na bado tunadanganywa na viongozi tunaotegemea wachukue hatua, tumeshindwa hata kuandamana tu!!! Viongozi wetu wanajua kama wao nimazumbukuku basi sisi wanachi nimazumbukuku no. 1. Pinda asingekuja na utumbo huu kama angejua kuwa wananchi tutachukua hatua.
Maandamano ya amani ya kushinikiza uwajibikaji, majibu sahihi ya kashfa zote na uchukuliwaji wa hatua kwa wahusika wote ndo dawa.
Mkuu
Nafikiri inatakiwa maandamano ya amani hili kushinikiza serikali Isiendelee kudanganya wananchi na pia iweze kushughulikia mambo yote ya mafisadi.
Sijasikia wapinzani wakiomba kibali kuhakikisha mikoa mbali mbali wanaandamana kuhakikisha haki inatendeka wote walioiba mali zetu bila kuangalia ni nani wanashughulikiwa.