Mwanakijiji iwapo taarifa zimefahamika kwa nini watu tununue hizo taarifa na tusipewe bure?
Je Watanzania wasioweza kuchangia hizo dola 30 lakini wanataka kufahamu huo uozo wa meremeta wafanyeje? ilhali kuna watanzania wanaufahamu huo uozo lakini wanauza hata taarifa?.
Mimi ninapinga kwa nguvu zote, hatua hii ya mwanakijiji kuuza hizi taarifa muhimu, taarifa za kuwakomboa watanzania lakini zinageuzwa kuwa za kuuzwa instead.
Kwa jinsi hizi taarifa zilivyo muhimu, thamani yake ni kubwa sana kiasi kwamba hizi dola 30 zitakwamisha lengo la kumkomboa Mtanzania aliye masikini ajabu (dola 30 kwake ni mshahara wa mwezi).
sana sana kinachofanyika kwa hizi dola 30 ni kutugawa Watanzania katika kundi la walionacho na wasionacho linapokuja suala muhimu la kukomboana sisi kwa sisi, kwa sababu hakuna ushahidi kwamba mwenye hizo dola 30 ndo mwenye brain muscle, au patriotism kubwa, au uwezo wa kuleta mabadiliko ya kweli katika ile nchi kuliko mlalahoi, mshinda njaa, ambaye hana kitu lakini anaumia kweli kweli kutokana na madudu haya yaliyomo kwenye MereMeta.
Mwanakijiji fikiria mara mbili kabla hujatuuzia hizi taarifa.
Mkuu mimi naamini kwanza hata gharama aliyoitoa kama kweli wewe ni mzalendo ni ndogo sana kumbuka amepata taarifa ameziweka kwenye kitabu/kijarida vyote hivyo vinagharama zake sasa kuchangia gharama hizi kwa manufaa ya taifa wewe unaona siyo sahihi.MKJJ amejitoa mhanga kwa ajili ya nchi yetu hilo pekee lilitakiwa tumpongeze.
....Mods kutokana na uzito wa habari hii naelekea kufikiri kikosi cha 'usalama' humu jamvini wamo Alert kwa lolote litakalotokea,kwa kipindi cha siku2hizi tutatembelewa sana humu ndani!!
**Ni mawazo binafsi tu!
...Mkuu ngoja kwanza 'MTOTO' azaliwe halafu wakati maalumu ukifika utatuelezea yaliyojiri.....bila shaka ni makubwa.you have no idea mambo yaliyotokea siku hizi chache..mengine yanachekesha na kuudhi kwa wakati mmoja.
Buuu...haya wajameni this is all what I have....
password: meremeta1997
Mkuu mwanakijiji, Mungu wa rehema akulinde na kukubariki kwa kazi nzuri unayolifanyia taifa letu, nasema asante sana.
Amen, awasute sute maadui zako, awaangamize kwa motona upepo wa kisuli suli, awagharikishe kama farao na jeshi lake walivogharikishwa kwenye bahari ya shamu!
nyinyi mnataka kuwatibua mafisadi sasa!
Na watibuke tu ndo tuwajue..kabla kiboko hajachokozwa unaweza kudhani ni gogo liko kwenye maji ,, lakini tibua kidogo ndo utajua kama ni kiboko au gogo.
FYI, juzi niliangalia tena documentary ya mapanki, ili kuwa na background nzuri ya hii kitu....nakuhakikishia safari hii nimeielewa zaidi kuliko mwanzoni!
you have no idea mambo yaliyotokea siku hizi chache..mengine yanachekesha na kuudhi kwa wakati mmoja.