Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Status
Not open for further replies.
sorry to burst your bubble.. suala hili limefikia tamati ya kiutuzima. Nadhani na sisi tuliache liishie hivyo hivyo na turudi kwenye Kagoda yetu, EpA, Meremeta na wenzake. Kama wangekuwa na la kufanya wangefanya na habari toka ndani sana, kijana wetu alikosea tu kidogo na ninaamini atakuwa amejifunza.


Kiongozi Mwamakijiji,

With due respect napenda nitofautiane na wewe kwa hili. Kwa Watanzania haijalishi kama hili suala wamefikia tamati kiutu uzima au la. Hili swali kwa sasa ni public issue. Mengi alianza in public na Waziri kijana akalisemea in public. Watanzania wanayo haki ya kujua majibu ya maswali yote.

Na kama humu JF unadhani kama eti kwa sasa tuliache na kurudi on other issues, I am afraid tutakua tunaingia katika ufisadi upya. Ni lazima tupressurize ili kupata facts zote kama:

Ni nani aliyemtishia Mengi kifo na ikiwezekana afikishwe mbele ya vyombo vya sheria.

Ni waziri yupi kijana aliyetaka kumujumu Mengi? Tunapenda kuona pia sheria inachukua mkondo wake.

Na baada ya hayo serikali itoe maelezo ya kuridhisha kwa Wananchi kama vikao hivyo kweli vilikuwapo vinginevyo ijisafishe kabisa kwa kuchukua hatua kwa wote waliuohusika na njama hizi. Ikigundulika ni kweli, Wanaharakati wachukue hatua kulipigia kelele hili na kama kuna namna sheria pia ichukue mkondo wake.

Mwishoni, naomba wewe Mwanakijiji, utoe makala katika CHECHE, Watanzania wapate kujua based on information na facts zilozopatikana mpaka sasa. Usipofanya hivyo, nitakuwa na maswali Mengi sana ya kujiuliza juu yako.

Mwanakijiji, hizi ni zama mpya na mambo ya kishikaji hayapo tena. Mwizi aitwe mwizi, Mhujumu aitwe mhujumu, nk na kwa wote hao sheria zichukue mkondo wake.

Usitukatishe tamaa, wengi tumekuwa tukikuona kama mmoja wa viongozi wetu hapa JF. Au wameanza kukununua?

Nimesema tulitoa kiingilio kwenye Movie Hii, Trailler imekwisha tunasubiri Movie. Kama Movie hakuna, turudishiwe pesa na turudi home tuwaaambie Wadau ni nani waliochemsha na kwa vipi.
 
dah hapa kitu ambacho mie sikielewi ni kuwa mbona naona kuna wanaomtete masha alafu kila mara twaagwa kuwa ni mwisho wa wao kumtetea mtu asiyeteteeka,bt still twazidi ona maneno ya kumtetea kila siku toka day 1 de saga ilipoanza?!

swali langu la msingi kama lilivyoulizw ana mmoja wetu na naomba lijibiwe hilo tu na siyo ku quote part nyingine ya maneno yangu!maana najua hao mawakili wa masha watarudi tena kujibu!

je kwani masha alipotoa vitisho vyake vya kumpa mengi siku 7 si alisema ana do dat as waziri wa mambo ya ndani n ana protect maslahi ya wananchi?
sasa iweje twaambiwa tena tumsubiri masha arudi trip la geneva sijui wapi huko?!
kwani wahusika wooote wa wizara ya mambo ya ndani nao wamekwenda geneva?

ni hayo tu
 
sorry to burst your bubble.. suala hili limefikia tamati ya kiutuzima. Nadhani na sisi tuliache liishie hivyo hivyo na turudi kwenye Kagoda yetu, EpA, Meremeta na wenzake. Kama wangekuwa na la kufanya wangefanya na habari toka ndani sana, kijana wetu alikosea tu kidogo na ninaamini atakuwa amejifunza.

Katika mazungumzo yetu tusije kumdestroy isipokuwa kama yeye mwenyewe anatupa sababu hasa ya kufanya hivyo, hili la yeye na Mengi sidhani kama linafikia kwenye level hiyo. Tunachotaka kuona ni jinsi gani anashughulikia uhalifu uliopo sasa na kama atasimamia kampeni dhidi ya mauaji ya Albino angalau kwenda huko vijijini na kuonekana na wananchi.

Sijamuona Masha akisimama na maaAlbino kuonesha kuwa kweli anajali na yuko on top of it (haina maana hajawahi kufanya hivyo).


Kama ilivyowekwa wazi mwazo wake tunataka na tamati yake iwe wazi!Si walikimbilia kwenye runinga wote kutuabadilsha.

Yaani unataka kusema kama picha basi umemeumekatika!
 
sorry to burst your bubble.. suala hili limefikia tamati ya kiutuzima. Nadhani na sisi tuliache liishie hivyo hivyo na turudi kwenye Kagoda yetu, EpA, Meremeta na wenzake. Kama wangekuwa na la kufanya wangefanya na habari toka ndani sana, kijana wetu alikosea tu kidogo na ninaamini atakuwa amejifunza.

Katika mazungumzo yetu tusije kumdestroy isipokuwa kama yeye mwenyewe anatupa sababu hasa ya kufanya hivyo, hili la yeye na Mengi sidhani kama linafikia kwenye level hiyo. Tunachotaka kuona ni jinsi gani anashughulikia uhalifu uliopo sasa na kama atasimamia kampeni dhidi ya mauaji ya Albino angalau kwenda huko vijijini na kuonekana na wananchi.

Sijamuona Masha akisimama na maaAlbino kuonesha kuwa kweli anajali na yuko on top of it (haina maana hajawahi kufanya hivyo).

na masuala ya kagoda, epa, meremeta yakiamuliwa kuisha kiutu uzima tusilalamike. hivi hapa hoja ilikuwa lau ama kitendo cha waziri kupendekeza kumhujumu mwananchi? sidhani ni vyema hili likaisha kiutu uzima kwani leo imeshindikana kwa mengi (asante kwa kuwa na vyombo vya habari) lakini kesho yaweza kuwa mimi au mtu mwengine asiye maarufu wala kuwa na access na vyombo vya habari.
 
While Mengi is not exactly clean, Masha is the loser any way you cut this.
 
Date::12/15/2008
Suluhu la Masha, Mengi latafutwa
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

BAADA ya wiki moja kupita huku mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi akiwa hajawasilisha uthibitisho wa tuhuma alizotoa hadharani kuwa kuna "waziri kijana" anataka kuhujumu biashara zake, duru za habari zinaeleza kuwepo jitihada kumaliza sakata hilo kwa mwafaka kati yake na Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha.

Jitihada hizo zimekuja kufuatia kile kinachoonekana kwamba, mjadala huo hauna maslahi kwa taifa na unaweza kusababisha mgawanyiko katika nchi.

Wakati jitihada hizo zinafanyika, hadi mwisho wa 'notisi' ya siku saba iliyokuwa Ijumaa iliyopita, Mengi alikuwa hajawasilisha ushahidi huo, huku waziri Masha akiwa safarini kikazi Geneva, Uswisi ambako alitarajiwa kurejea jana.

Duru za habari ambazo Mwananchi imezipata kutoka serikalini, zinasema juhudi za kutafuta suluhu baina ya 'wazito hao' zinafanyika baada ya sakata hilo kuonekana kuchukua mwelekeo mbaya kwa taifa.

Kwa mujibu wa duru hizo za habari za kuaminika, ndani ya serikali kunafanyika juhudi za kutoendeleza suala hilo kama lilivyowahi kutokea kwa aliyewahi kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, Wilson Masilingi, katika serikali ya awamu ya tatu.

Duru hizo za kiserikali zinasema, hata ndani ya Jeshi la Polisi kumekuwa na jitihada za kutaka suala hilo lisiendelezwe kwa hoja kuwa halina maslahi kwa taifa.

Alipoulizwa kuhusu suala hilo, msemaji mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Isaac Nantanga alijibu: "Any thing can happen (lolote linaweza kutokea)."

Kwa mujibu wa Nantanga, serikali haina ugomvi na Mengi hivyo inaweza kutumia njia yoyote kumaliza suala hilo kwa taratibu.

Hata hivyo, Nantanga alifafanua kwamba hadi sasa bado anasubiriwa Waziri Masha ambaye alitarajiwa kurejea jana akitokea Geneva, Uswisi.

Aliongeza kwamba licha ya kusubiriwa Waziri Masha, ni vema Watanzania wakafahamu kwamba, uamuzi wa kumtaka Mengi kuwasilisha uthibitisho ulikuwa na lengo la kulinda haki na usalama wa raia huyo kama Mtanzania mwingine.

"Pia ieleweke, serikali haina ugomvi na Mengi. Alichofanya waziri ambaye wizara yake ina dhamana na usalama wa raia na mali zao, ilikuwa ni kutafuta uthibitisho na kumlinda mfanyabiashara huyo, na wala si vinginevyo," alisisitiza Nantanga na kuongeza:

"Lakini, wacha tumsubiri waziri maana tunatarajia atarejea leo (jana). Lakini nasisitiza serikali haina ugomvi na Mengi."

Msemaji huyo mkuu wa mambo ya ndani, alisisitiza kwamba, Mengi ana haki ya kuhakikishiwa usalama wake na mali ndiyo maana serikali imeamua kumwomba asaidie kupata uthibitisho ili sheria ichukue mkondo wake.

Masha wiki moja iliyopita alimpa Mengi siku saba athibitishe tuhuma hizo vinginevyo angekabiliwa na nguvu za kisheria.

Sakata hilo tayari limevuta hisia tofauti baada ya wanasiasa wengi kumuunga mkono Mengi, baadhi wakidai wana ushahidi kuthibitisha kuwa Waziri Masha ndiye aliyewasilisha hoja hiyo ya kumuhujumu Mengi, huku Baraza la Wazee Mkoa wa Dar es Salaam likiuelezea mgogoro huo kuwa ni wa maslahi binafsi na si fikra za Watanzania.

Wazee hao, ambao pia walikemea mjadala wa Tanzania kujiunga na Jumuiya Kiislam Duniani (OIC), walisema malumbano yaliyopo hayawasilishi mawazo ya wananchi bali maslahi binafsi ya kibiashara na kisiasa.

Hii si mara ya kwanza kwa Mengi kuingia katika malumbano na wanasiasa, katika awamu ya tatu aliingia katika malumbano na Masilingi, akielekeza makombora mazito ya tuhuma za kuwepo mchezo mchafu katika zabuni ya uuzaji wa hoteli ya Kilimanjaro, sasa Kempinski.
 
suala kina Mgonja kupelekwa mahakani leo ni sehemu ya mkakati wa kupooza hii issue ya Masha Vs Mengi.

Waandishi wa habari mliopo hapa Jamvini pamoja na kesho kutoa reporti ya GM kupelekwa kikaangioni mkumbusheni Masha in the front page alichokiahidi kwa umma. Ahadi ni Deni, lakini pia ni wajibu wa kiongozi kutimiza wajibu wake, vinginevyo awaombe radhi wananchi, then tuamue kumsamehe ama kumfukuza kazi.
 
Katika pita pita yangu mitaani nilinasa haya mazungumzo kati ya watu wanne. Natoa sehemu ya kwanza tu na itaendelea..............

Kichuguu!
Nadhani haujamuelewa aliyeweka hilo bandiko!


Fundi Mchundo asante sana kwa kunibip.

Mag3, samahani kwa kuweka maneno yasiyo yako mdomoni mwako. Nilisoma yale makubwa ambayo mengi ni upupu, kumbe sikuwa nimeangalia huo utangulizi hapo juu.
 
suala kina Mgonja kupelekwa mahakani leo ni sehemu ya mkakati wa kupooza hii issue ya Masha Vs Mengi.

Waandishi wa habari mliopo hapa Jamvini pamoja na kesho kutoa reporti ya GM kupelekwa kikaangioni mkumbusheni Masha in the front page alichokiahidi kwa umma. Ahadi ni Deni, lakini pia ni wajibu wa kiongozi kutimiza wajibu wake, vinginevyo awaombe radhi wananchi, then tuamue kumsamehe ama kumfukuza kazi.

WE KWELI KICHAKA, simini kama una amini hivyo na unataka na sisi tuamini hivyo. SIAMINI NA SIPENDI KUAMINI.

Kwakuwa suala la Mgonja liko connected na YONA + Mramba na hoa walikamatwa kabla ya issue na MANGI na MASHA unataka kutueleza nini hapa? Du kwahumini wa Wengi tuko Mengi.
Tujitahidi kuepuka visingizio jamani jamani.
 
Date::12/15/2008
Serikali yatafakari hatua dhidi ya Mengi
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

BAADA ya wiki moja kupita bila ya mfanyabiashara maarufu nchini, Reginald Mengi kuwasilisha uthibitisho wa tuhuma alizotoa hadharani za kuwepo "waziri kijana" ambaye anataka kuhujumu biashara zake, serikali sasa inatafakari taratibu za kisheria za kushughulikia sakata hilo.

Hatua hiyo mpya ya serikali imekuja wakati Mengi akiwa kimya huku habari za kiserikali zikilidokezea gazeti hili kuwa kuna mipango ya chini kwa chini ya kumaliza sakata hilo kabla halijawa kubwa na kugawa watu wa kada mbalimbali.

Uamuzi huo pia umekuja baada ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha kurejea nchini juzi akitokea Geneva, Uswisi alikoenda kikazi.

Baada ya Mengi kutuhumu kuwa kuna "waziri kijana" ambaye anataka kumbambikizia kodi ili ashindwe kulipa na baadaye kufilisiwa, Waziri Masha alijitokeza na kumtaka mfanyabiashara huyo kuwasilisha uthibitisho wa tuhuma zake na kwamba akishindwa kufanya hivyo atachukuliwa hatua za kisheria.

Wakati Masha, ambaye simu yake ya kiganjani jana ilikuwa ikiita bila majibu, ameamua kuwa kimya, msemaji wa mfanyabiashara huyo, Abdulhamin Njovu alisema bosi wake hapendi kuzungumzia tena suala hilo.

Hata hivyo, msemaji mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Isaac Nantanga, aliliambia gazeti hili kwamba serikali inaangalia sheria zikoje katika kushughulikia suala kama hilo.

"Kwa sasa serikali inatafakari... haiwezi kuamua tu kuchukua hatua. Kinachofanyika ni kuona sheria inasemaje maana huyu bwana ameshindwa kutoa uthibitisho," alisema Nantanga.

Nantanga aliongeza kuwa kutokana na suala hilo kuwa la kisheria, serikali nayo haitaki kukurupuka katika maamuzi ya jambo hilo na kwamba si suala la kusema "kesho hatua zitachukuliwa" bali kuangalia sheria inasemaje.

"Hili si jambo la haraka namna hiyo, ni jambo la kisheria zaidi," alifafanua.

Alirudia kauli yake ya juzi kuwa serikali haina uadui na Mengi bali ilichofanya ni kutaka kulinda usalama wake na mali kutokana na vitisho alivyoeleza kupata.

Hatua hiyo mpya ya serikali kusema inatafakari namna ya kushughulikia sakata hilo, inazidi kuonyesha na kuthibitisha kwamba upo mpango wa kuzima suala hilo kwa taratibu za muafaka bila kuendelea kulikuza.

Jitihada hizo, ambazo zimeripotiwa katika gazeti hili jana, zimekuja kutokana na kile kinachoonekana kwamba mjadala huo hauna maslahi kwa taifa na unaweza kusababisha magawanyiko.

Wakati jitihada hizo zinafanyika, hadi mwisho wa 'notisi' ya siku saba iliyokuwa Ijumaa iliyopita, Mengi alikuwa hajawasilisha ushahidi huo.

Hata hivyo, licha ya kurejea tofauti na ilivyokuwa awali, Masha hakuweza tena kuzungumzia suala hilo katika siku ya jana ambayo ni zaidi ya siku tatu kati ya zile saba alizotoa kwa Mengi.

Ukimya wa Masha unaelezwa ni sehemu ya mpango wa chini kwa chini ndani ya serikali, kutaka kuzima suala hilo kama lilivyowahi kutokea kwa aliyewahi kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Utawala Bora, Wilson Masilingi, katika serikali ya awamu ya tatu.
 
Nimegundua kuwa pande zote katika sakata hili ni wapuuzi. Kuna unafiki na uzandiki.
 
Mkulu Mag,

Naona umefanya kazi nzuri sana kukumbushia maandishi (ambayo wengine wanayaita ukweli) ambayo baadhi ya watu wameandika hapa kwenye hii thread kuanzia imeanza. Baada ya muda yataongezeka majina behind every quote iliyowekwa hapo juu ili kuwakumbusha walichosema mwanzoni (by the way, most of them ni za the same person).

Good job sana kwa kutunza kumbukumbu na kuonesha jinsi watu wanavyogeuka geuka kama vinyonga kwenye hii issue ya Masha Vs Mengi.

MWK asante sana na huo ni utangulizi tu, makubwa yatafautia - naomba mnivumilie. La kusikitisha ni kuwa wakurupaji itawachukua muda kunielewa. Nafikiri msimamo wangu unaeleweka.
 
Hii issue imeishia wapi??????

Ina maaana tumeshahau, na Masha kasahau ahadi aliyotoa hadharani?????

kweli sisi ni wadanganyika.

Its now time to call for resignation of Mr waziri for being Promiseless
 
Ndugu wanaJF,

Tumesikia mambo mengi kutokana na na saga la Masha VS Mengi. Bila kujali tuhuma Mengi alizoziweka juu ya waziri kijana ambaye hakutajwa jina na Mengi.

Masha kama waziri mwenye dhamana ya usalama wa raia na mali zao, aliahidi kuchukua hatua dhidi ya yule ambaye anataka kumdhuru raia Mengi na mali zake, hivyo kutaka kupata vidhibitisho kutoka kwa mengi. Ili kutimiza azma hiyo Masha alimuomba/mlazimisha Mengi kuwakilisha vielelezo vya ushahidi kwenye ofisi yake, na kama akishindwa vile vile Mengi angechukuliwa hatua kwa kuipaka serikali na vyombo vyake matope ama kafanya uchochezi.

Siku saba zilishakwisha, Mengi hakupeleka vielelezo kama alivyotakiwa, Masha kama waziri na ofisi yake kwa ujumla imekaa kimya bila kusema chochote baada ya siku saba kuisha.

Hivyo Sababu za masha kujiuzulu ni hizi hapa:
Masha ameshindwa kutimiza wajibu wake kama waziri kulinda raia na mali zao, ameshindwa ahadi yake aliyoitoa siku 12 tu zilizopita. Hivyo Masha ni Muongo amaudanganya UMMA.

Inawezekana kabisa 99% ni kweli Masha alihusika kwenye huo mpango wa kutaka kumfilisi Mengi hivyo kauogopa kutimiza yale mamlaka yaliyo chini yake kwa hofu ya kumtokea puani(kumbuka Balali alifanya press akasema yeye ni safi, Mgonja nae hivyo hivyo, Mramba ndio usiseme na wote walitishia kwenda mahakani leo wao ndio wako huko) Kwa mifano hiyo inatosha kusema Masha anahusika kwenye hiyo plan.

Masha angekuwa muungwana, alipoona hiyo ahadi yake haitekelezeki alipaswa kurudi kwenye press na kuomba msamaha kwa kauli yake aliyeitoa na kusema alikuwa mislead hivyo either anaifuta kauli yake ama atuambie wamefikiria kuchukua hatua ingine (maelewano nje ya vyombo vya dola), na kama ni hivyo kwani Mengi anaugomvi gani na Masha kama Masha hausiki kwenye hiyo tuhumaaa???? Leo ni siku ya 5 Kimya chake ni dharau kubwa kwa wananchi wa Tanzania, Hivyo hafai kuongoza umma wa watanzania

Mwisho nitoe wito kwa viongozi wengine kutojiona wao ni miungu kuwa hawakosei, sisi kama binadamu tunakosea na tunapokosea kiungwana tunaomba msamaha, tuache dharau na kujikweza kama Masha.

Masha Tukosa imani na wewe, Maalbino wanauwawa uko kimya kutatua tatizo,
Vikongwe wanauwawa uko kimya, tangu uingie kwenye hiyo wizara ujambazi umeongezeka, Usalama wa raia na hata wa rais umekuwa mashakani (kumbuka yaliyotokea Mbeya), n.k Hufai jiuzulu, Masha jiuzulu
 
Jk amfute kazi aliyevujisha siri ya mkutano wa baraza lake la mawaziri. Inapaswa iwe kama alivyotendewa lowasa aliyesemekana kummegea siri mengi juu ya ule ugomvi wake na manji .

Serikali inapaswa idumu ktk usiri wa mipango mikuu ya kidola. Haiwezekani leo tunamjadiri fmes then kesho raia mwema front page au fmes anaenda ktk redio mbao yake na kupiga mkwara!!!!

Usalama wa nchi unatikiswa na aina hii ya ujasiri kiburi wa watu wa aina ya mengi.
 
Jk amfute kazi aliyevujisha siri ya mkutano wa baraza lake la mawaziri. Inapaswa iwe kama alivyotendewa lowasa aliyesemekana kummegea siri mengi juu ya ule ugomvi wake na manji .

Serikali inapaswa idumu ktk usiri wa mipango mikuu ya kidola. Haiwezekani leo tunamjadiri fmes then kesho raia mwema front page au fmes anaenda ktk redio mbao yake na kupiga mkwara!!!!

Usalama wa nchi unatikiswa na aina hii ya ujasiri kiburi wa watu wa aina ya mengi.

Spinning zimeanza, si kuna sheria ya siri za serikali?????? Kwa nini Masha asimchukulie hatua Mengi kwanza kwa kupata siri za serikali. Pili Masha ajiuzulu kwa kupanga kuharibu mali za raia wema kinyume cha majukumu yake kwenye hiyo anayoiita siri ya serikali.

Mengi amekiri hadharani kapata siri ya serikali, Ni wajibu wa serikali kuikanusha siri hiyo ama kuikubali, na kukaa kwake kimya maana yake ni kweli walikua na huo mpango ukiongozwa na Mh Masha. Hivyo kwa sababu huo mpango ni batili na Masha ndio kiongozi wa huo mpango ajiuzulu kwa nini asubiri hadi Kikwete amuachishe kazi?????

Masha ng'atuka Kabla ya fagio lachuma
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom