Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Mengi Vs Masha tuhuma, vitisho na matokeo!

Status
Not open for further replies.
Ndugu wanaJF,

Tumesikia mambo mengi kutokana na na saga la Masha VS Mengi. Bila kujali tuhuma Mengi alizoziweka juu ya waziri kijana ambaye hakutajwa jina na Mengi.

Masha kama waziri mwenye dhamana ya usalama wa raia na mali zao, aliahidi kuchukua hatua dhidi ya yule ambaye anataka kumdhuru raia Mengi na mali zake, hivyo kutaka kupata vidhibitisho kutoka kwa mengi. Ili kutimiza azma hiyo Masha alimuomba/mlazimisha Mengi kuwakilisha vielelezo vya ushahidi kwenye ofisi yake, na kama akishindwa vile vile Mengi angechukuliwa hatua kwa kuipaka serikali na vyombo vyake matope ama kafanya uchochezi.

Siku saba zilishakwisha, Mengi hakupeleka vielelezo kama alivyotakiwa, Masha kama waziri na ofisi yake kwa ujumla imekaa kimya bila kusema chochote baada ya siku saba kuisha.

Hivyo Sababu za masha kujiuzulu ni hizi hapa:
Masha ameshindwa kutimiza wajibu wake kama waziri kulinda raia na mali zao, ameshindwa ahadi yake aliyoitoa siku 12 tu zilizopita. Hivyo Masha ni Muongo amaudanganya UMMA.

Inawezekana kabisa 99% ni kweli Masha alihusika kwenye huo mpango wa kutaka kumfilisi Mengi hivyo kauogopa kutimiza yale mamlaka yaliyo chini yake kwa hofu ya kumtokea puani(kumbuka Balali alifanya press akasema yeye ni safi, Mgonja nae hivyo hivyo, Mramba ndio usiseme na wote walitishia kwenda mahakani leo wao ndio wako huko) Kwa mifano hiyo inatosha kusema Masha anahusika kwenye hiyo plan.

Masha angekuwa muungwana, alipoona hiyo ahadi yake haitekelezeki alipaswa kurudi kwenye press na kuomba msamaha kwa kauli yake aliyeitoa na kusema alikuwa mislead hivyo either anaifuta kauli yake ama atuambie wamefikiria kuchukua hatua ingine (maelewano nje ya vyombo vya dola), na kama ni hivyo kwani Mengi anaugomvi gani na Masha kama Masha hausiki kwenye hiyo tuhumaaa???? Leo ni siku ya 5 Kimya chake ni dharau kubwa kwa wananchi wa Tanzania, Hivyo hafai kuongoza umma wa watanzania

Mwisho nitoe wito kwa viongozi wengine kutojiona wao ni miungu kuwa hawakosei, sisi kama binadamu tunakosea na tunapokosea kiungwana tunaomba msamaha, tuache dharau na kujikweza kama Masha.

Masha Tukosa imani na wewe, Maalbino wanauwawa uko kimya kutatua tatizo,
Vikongwe wanauwawa uko kimya, tangu uingie kwenye hiyo wizara ujambazi umeongezeka, Usalama wa raia na hata wa rais umekuwa mashakani (kumbuka yaliyotokea Mbeya), n.k Hufai jiuzulu, Masha jiuzulu
Hapa sielewi, kwani Masha alisema atamchukulia hatua ndani ya siku saba au Mangi atoe ushahidi baada ya siku saba? inawezekana anajipanga who knows?

JF pazuri bwana a lot of PERCEPTION and BLA BLA
 
Sababu za masha kujiuzulu ni hizi hapa:
Masha ameshindwa kutimiza wajibu wake kama waziri kulinda raia na mali zao, ameshindwa ahadi yake aliyoitoa siku 12 tu zilizopita. Hivyo Masha ni Muongo amaudanganya UMMA.
Mkuu kichakoro ,
Karibu sana Jamvini na tunafurahia sana kupata mawazo kutoka kwa watanzania ,tuendeleze libeneke.

Una uhakika Gani kama Masha ameudanganuya Umma,AU umeshaenda Kumuuliza ana mpango wa kuchukua hatrua gani?siku zote tuwe wavumilivu na tupime jambo lenyewe huku tukisubiri maamuzi.

Umma unaouongelea hapa ni upi?


Inawezekana kabisa 99% ni kweli Masha alihusika kwenye huo mpango wa kutaka kumfilisi Mengi hivyo kauogopa kutimiza yale mamlaka yaliyo chini yake kwa hofu ya kumtokea puani(kumbuka Balali alifanya press akasema yeye ni safi, Mgonja nae hivyo hivyo, Mramba ndio usiseme na wote walitishia kwenda mahakani leo wao ndio wako huko) Kwa mifano hiyo inatosha kusema Masha anahusika kwenye hiyo plan.

Tayari hapa umeshasema masha alihusika kwa asilimia 99%.Wewe ndiyounao huo ushahidi na pindi utakapohitajika basi peleka maelezo yako kama alivyosema ndugu yangu zitto.Mengi angekuwa naujasiri angekuja mbele pale na kumsema wazi wazi mtu aliyemtaja kuliko kuweka siasa katika kuelezea jambo.

Masha angekuwa muungwana, alipoona hiyo ahadi yake haitekelezeki alipaswa kurudi kwenye press na kuomba msamaha kwa kauli yake aliyeitoa na kusema alikuwa mislead hivyo either anaifuta kauli yake ama atuambie wamefikiria kuchukua hatua ingine (maelewano nje ya vyombo vya dola), na kama ni hivyo kwani Mengi anaugomvi gani na Masha kama Masha hausiki kwenye hiyo tuhumaaa???? Leo ni siku ya 5 Kimya chake ni dharau kubwa kwa wananchi wa Tanzania, Hivyo hafai kuongoza umma wa watanzania
Kimya kingi kina mshindo mkuu,spika huwa na msemo mmoja anaupenda sana..Mtu mzima basi na yeye na Mengi inawezekana walikaa wakapima uhalisia wa jambo lenyewe na kuchukua maamuzi yenye manufaa kwa nchi yetu.MAsha siyo sawa na Ze comedy!

Mwisho nitoe wito kwa viongozi wengine kutojiona wao ni miungu kuwa hawakosei, sisi kama binadamu tunakosea na tunapokosea kiungwana tunaomba msamaha, tuache dharau na kujikweza kama Masha.

Masha Tukosa imani na wewe, Maalbino wanauwawa uko kimya kutatua tatizo,
Vikongwe wanauwawa uko kimya, tangu uingie kwenye hiyo wizara ujambazi umeongezeka, Usalama wa raia na hata wa rais umekuwa mashakani (kumbuka yaliyotokea Mbeya), n.k Hufai jiuzulu, Masha jiuzulu

Toa sababu za msingi ambaoz unadhani utajenga hoja masha ajiuzuru siyo kwa kuangalia jambo moja ambalo halina manufaa kwa nchi yetu.Suala la Ujambazi limekuwapo muda mrefu sana hapa nchini na chimbuko lake linajulikana sana.Watu tuna data tumekaa kimya!

Usalama wa Rais umekuwa matatani toka lini?au kuna mipango uanyoijua wewe ambayo sisi hatuijui ya kumdhulu mkwere?

Jambo lilitokea Mbeya alina tofauti na lilimpatya Bush Majuzi,Je waziri wa ulinzi wa marekani kajiuzuru.U are missing a point hapa.Usalama wa Rais hauko chini ya wizara ya Masha..waulize watu wa idara watakueleza

Kama umetumwa ,basi aliyekutuma hakujipanga vyema..

wakulu,tuendelee kukata ishu!
 
Jk amfute kazi aliyevujisha siri ya mkutano wa baraza lake la mawaziri. Inapaswa iwe kama alivyotendewa lowasa aliyesemekana kummegea siri mengi juu ya ule ugomvi wake na manji .

Serikali inapaswa idumu ktk usiri wa mipango mikuu ya kidola. Haiwezekani leo tunamjadiri fmes then kesho raia mwema front page au fmes anaenda ktk redio mbao yake na kupiga mkwara!!!!

Usalama wa nchi unatikiswa na aina hii ya ujasiri kiburi wa watu wa aina ya mengi.

Mkuu FDR.Jr,

Mambo ya siri ambayo wote wanawajibika kuyalinda ni yale yenye manufaa kwa nchi.

Mtu analeta ujinga wa kutaka kumfanyia unyama raia wa Tanzania bila sababu za maana, unataka hao wote waliosikia wakae kimya?

Huyo aliyevujisha hiyo siri alifanya la maana sana.
 
Mkuu kichakoro ,
Karibu sana Jamvini na tunafurahia sana kupata mawazo kutoka kwa watanzania ,tuendeleze libeneke.

Una uhakika Gani kama Masha ameudanganuya Umma,AU umeshaenda Kumuuliza ana mpango wa kuchukua hatrua gani?siku zote tuwe wavumilivu na tupime jambo lenyewe huku tukisubiri maamuzi.

Umma unaouongelea hapa ni upi?




Tayari hapa umeshasema masha alihusika kwa asilimia 99%.Wewe ndiyounao huo ushahidi na pindi utakapohitajika basi peleka maelezo yako kama alivyosema ndugu yangu zitto.Mengi angekuwa naujasiri angekuja mbele pale na kumsema wazi wazi mtu aliyemtaja kuliko kuweka siasa katika kuelezea jambo.


Kimya kingi kina mshindo mkuu,spika huwa na msemo mmoja anaupenda sana..Mtu mzima basi na yeye na Mengi inawezekana walikaa wakapima uhalisia wa jambo lenyewe na kuchukua maamuzi yenye manufaa kwa nchi yetu.MAsha siyo sawa na Ze comedy!



Toa sababu za msingi ambaoz unadhani utajenga hoja masha ajiuzuru siyo kwa kuangalia jambo moja ambalo halina manufaa kwa nchi yetu.Suala la Ujambazi limekuwapo muda mrefu sana hapa nchini na chimbuko lake linajulikana sana.Watu tuna data tumekaa kimya!

Usalama wa Rais umekuwa matatani toka lini?au kuna mipango uanyoijua wewe ambayo sisi hatuijui ya kumdhulu mkwere?

Jambo lilitokea Mbeya alina tofauti na lilimpatya Bush Majuzi,Je waziri wa ulinzi wa marekani kajiuzuru.U are missing a point hapa.Usalama wa Rais hauko chini ya wizara ya Masha..waulize watu wa idara watakueleza

Kama umetumwa ,basi aliyekutuma hakujipanga vyema..

wakulu,tuendelee kukata ishu!

Nitakujibu maswali yako yote kwa sentensi hii moja kutoka kwenye signature ya bow bow

When a leopard starts devouring its young ones, it starts by accusing that young one of smelling like a goat
 
Jk amfute kazi aliyevujisha siri ya mkutano wa baraza lake la mawaziri. Inapaswa iwe kama alivyotendewa lowasa aliyesemekana kummegea siri mengi juu ya ule ugomvi wake na manji .

Serikali inapaswa idumu ktk usiri wa mipango mikuu ya kidola. Haiwezekani leo tunamjadiri fmes then kesho raia mwema front page au fmes anaenda ktk redio mbao yake na kupiga mkwara!!!!

Usalama wa nchi unatikiswa na aina hii ya ujasiri kiburi wa watu wa aina ya mengi.

Siyo kila siri ni siri ya manufaa ya Taifa na endelevu. Swala la kumfilisi mtu anaefanya biashara/kazi zake kihalali ni siri ya serikali? Serikali gani badala ya kufikiria kutoa incentives kwa wazawa kama Mengi wanaotoa daily breads for to thousands of Tanzanians, eti ushauri afilisiwe halafu unasema eti ni siri ya serikali.

Imeshaonekana dhahiri sio kwamba Mengi anataka publicity stunt, hivyo mbali ya Mengi ameipata wapi hiyo siri au ni nani amempa Masha has to be accountable kwa nafasi yake na kufanya kishauri upuuzi huo.

Siri kufichuka, hakukuanza leo, hata hivyo siku hizi kufichuka kunazidi kwa sababu ndani ya hao decision-makers wengi wao wameshachosha the whole direction ya wenzao (hao mafisadi).

Hizo siri zingekuwa endelevu na kwa manufaa ya nchi kweli mtoa siri achukuliwe hatua, ila kwa hili Masha has to go, kwa kujiuzulu au Vasco Da Gama amemteme!
 
Nitakujibu maswali yako yote kwa sentensi hii moja kutoka kwenye signature ya bow bow

When a leopard starts devouring its young ones, it starts by accusing that young one of smelling like a goat

ukishindwa kwa hoja ni lazima utalete viroja ili kufurahisha jamvi!

Mkuu bado tupo..
 
Muheshimiwa Gembe unamtetea sana Mh Masha katika hili.Mwache ajitetee mwenyewe.
Sikubaliani na suala la kujiuzulu maana hili bado si suala zito kufikia hatua hiyo. Lakini kuna umuhimu wa wanasiasa kuwa careful na public statements wanazotoa kwa wananchi.
Mh Masha anaonekana bado hajaiva katika milolongo ya kisiasa na jamii.
Never !,I repeat, never loose your cool in public on any issue.Wananchi will pick out your brains as JF has superbly done.
Katika sakata hili la Mengi vs Masha ni wazi pumba iko wapi na mchele u wapi.
 
Hii issue imeishia wapi??????

Ina maaana tumeshahau, na Masha kasahau ahadi aliyotoa hadharani?????

kweli sisi ni wadanganyika.

Its now time to call for resignation of Mr waziri for being Promiseless

Ishu bado haijaisha..itaisha vipi?

It is now A time For Masha to show he can.

Mie huwa nashangaa sana watu ambao huwa wanampapalikia yule mzee ,ukiangalia alivyoa waangamiza vijana wa ze comedy utajua ni mtu wa namna gani na asivyo na aibu lile suala alilishupalia sana vijan wa watu wakose riziki.

hivi kweli?
 
Siyo kila siri ni siri ya manufaa ya Taifa na endelevu. Swala la kumfilisi mtu anaefanya biashara/kazi zake kihalali ni siri ya serikali? Serikali gani badala ya kufikiria kutoa incentives kwa wazawa kama Mengi wanaotoa daily breads for to thousands of Tanzanians, eti ushauri afilisiwe halafu unasema eti ni siri ya serikali.

Imeshaonekana dhahiri sio kwamba Mengi anataka publicity stunt, hivyo mbali ya Mengi ameipata wapi hiyo siri au ni nani amempa Masha has to be accountable kwa nafasi yake na kufanya kishauri upuuzi huo.

Siri kufichuka, hakukuanza leo, hata hivyo siku hizi kufichuka kunazidi kwa sababu ndani ya hao decision-makers wengi wao wameshachosha the whole direction ya wenzao (hao mafisadi).

Hizo siri zingekuwa endelevu na kwa manufaa ya nchi kweli mtoa siri achukuliwe hatua, ila kwa hili Masha has to go, kwa kujiuzulu au Vasco Da Gama amemteme!

Huu mjadala inaelekea hauna mashiko kabisa kwa sasa na hautusaidii kama Taifa kwa sababu nyingi tu ila napenda nizitaje chache:

-Kama kuna sababu ya kumtaka Masha ajiuzulu inaweza kuwa si hii ya ukurupukaji wake kwa Mengi kwani ana mengi tu ambayo yatamfanya Muungwana afikiri upya kwanini asimuondoe katika nafasi yake ya sasa.

-Naamini na Masha anaamini kwamba haikuwa wakati mwafaka kwa kiongozi mwenye kuongoza wizara nyeti kama kama yeye Wizara ya Mambo ya Ndani kukurupuka na kujibu kauli ambayo haikuwa inamlenga mtu moja kwa moja. Wizara hiyo vyombo vyya ulinzi vyenye watu wenye busara na makini wenye taaluma za sheria na usalama ambao wangeweza kuachiwa wafanye kazi yao wakishirikiana na wenzao wa UWT.

-Kwa imani yangu hiyo wale wote ambao wanawapenda au wanatumwa au wanashabikia ama wana bifu zao na Masha ama Mengi watulize bongo zao na kuangalia Tanzania kama Taifa tunahitaji nini kwa sasa na nguvu zetu tuelekeze wapi badala ya kuendeleza malumbano ambayo hayajengi.

-Naamini na wengi tu wanaamini kwamba Mengi alipopata ushahidi wa alichokisema aliamua kukisema tena baada ya kuwa na imani kwamba nguvu waliyonayo watu kama Masha si dola tu bali ni nguvu zaidi ya dola na mijadala humu ndani inadhihirisha hili, kwa hiyo akaona kwamba nguvu yake pekee ni umma wa Watanzania ambao wakisikia na mukiendelea kujadili kama munavyoendelea humu hakuna atakayetekeleza jambo lolote kwa HILA. Mfano ni kelele alizozitoa wakati wa sakata la Malima bungeni, kelele za kumtaja EL ziliwafanya waliokuwa wakilambishwa asali wajue wameumbuka na wakashindwa kutekeleza azma yao kwa kuwa walikuwa UCHI tayari.

-Kama Mengi aliyoyasema yangekuwa si ya kweli, isingekuwapo hoja ya kumsaka mtoa siri na kama hiyo ndiyo SIRI ya serikali na si taarifa ya Kagoda, Meremeta, Deep Green, Mwananchi Gold basi TUMEKWISHA maana zote hizo ziliandikwa na kutangazwa na juzi mbele ya Masha na Makamu wa Rais, Meng alihoji "Kagoda ni mdudu gani" hadi Masha akageka na kumshangaa Mengi lakini hakutoa kauli ya kumtisha pamoja na kuwa kauli ya Mengi ni kali kuliko aliyoitoa kuhusu Waziri Kijana, ila ya Waziri Kijana inamgusa mtu binafsi na hivyo tunaaminishwa kwamba SIRI ama USALAMA wa Taifa ni SIRI na USALAMA wa VIONGOZI wachache.

Naomba na ninapenda kuona kwamba huu mjadala uzingatie MASLAHI ya Taifa na vichwa vya JF, yaani wale wenye uelewa mkubwa waangalie ni jinsi gani wanaweza kutuchangamsha na mambo mazito tuliyozoea humu JF.

JF ndiyo iliyosimamia kidete mambo yote mazito mapema kabisa kama Richmond, EPA na mengine ambayo bado yako katika mchakato na baadaye watu wengine kuyabeba sasa tusipoteze muda wetu kujadili watu badala ya vitu.

Kumekuwa na mambo mazito yanaendelea huko Dodoma, tumesahau kabisa kwamba wafanyabiashara kama Tanil walitoa mchango kwa UVCCM na walipelekwa na viongozi vijana bila kujali mustakabali wa vijana wa taifa hili. Tunafahamu mahusiano kati ya Tanil, Vithlani na viongozi wetu wa sasa hilo linaweza kuwa jambo muhimu kujadiliwa.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, UWALAANI MAFISADI, INSHAALAH USHINDI UPO
 
Muheshimiwa Gembe unamtetea sana Mh Masha katika hili.Mwache ajitetee mwenyewe.
Sikubaliani na suala la kujiuzulu maana hili bado si suala zito kufikia hatua hiyo. Lakini kuna umuhimu wa wanasiasa kuwa careful na public statements wanazotoa kwa wananchi.
Mh Masha anaonekana bado hajaiva katika milolongo ya kisiasa na jamii.
Never !,I repeat, never loose your cool in public on any issue.Wananchi will pick out your brains as JF has superbly done.
Katika sakata hili la Mengi vs Masha ni wazi pumba iko wapi na mchele u wapi.
Mkuu G,

Mie siku zote huwa nasimamia kwenye haki.kipindi kile Msoala kafnaya blunder nilimuunga sana mkono Mzee Mwanakijiji katika azimio lake na kama mnakumbuka tulisign makubaliano(Bahati mbaya sana mzee akung'oka)

Ila hili la Masha siko tayari kuunga mkono,na nina sababu zangu!Tunahitaji nidhamu na usiri wa vikao vinavyohusu nchi yetu,sasa kama kuna mtu ambaye anaweza kumfuata mfanyabiashaara na kumwambia mambo ya vikao vya juu,basi hastahili kuachwa!

Kama ni Masha alisema(wanavyoamini wengi) basi achukuliwe hatua,kama Mengi aliambiwa na 'Mzee MWanakijiji' basi aseme ili tukate mzizi wa fitina.

Kuan katabia ambako mie sikukapenda has akale ka kuwarekdoi wale wazee wangu wa kiisilamu.alitaka kuchochoa suala baya sana kuliko yote na kosa lake lilianzi hapo
 
Mkuu FDR.Jr,

Mambo ya siri ambayo wote wanawajibika kuyalinda ni yale yenye manufaa kwa nchi.

Mtu analeta ujinga wa kutaka kumfanyia unyama raia wa Tanzania bila sababu za maana, unataka hao wote waliosikia wakae kimya?

Huyo aliyevujisha hiyo siri alifanya la maana sana.

nachelea kusema huu usijekuwa ndio mchezo wa lyatonga, ninyi mmekula kiapo cha kula nyama za watu kwa pamoja iweje leo anapotajwa kipenzi chako unasisimkwa na kukikana kiapo chako tena kwa siri, hili halikubaliki asakwe na apewe kibano cha nguvu, sirikali ni serikali Mtz, hapo ni lazima JK amfukuze huyo kwanza, kwanza ni kwanini yamuhusuyo mengi tu ndio yanatoka huko sirini na yeye ndiye breaking newser wetu always? Asakwe na na anyonywe macho huyo kwanza kabla ya Masha
 
Mkuu G,

Mie siku zote huwa nasimamia kwenye haki.kipindi kile Msoala kafnaya blunder nilimuunga sana mkono Mzee Mwanakijiji katika azimio lake na kama mnakumbuka tulisign makubaliano(Bahati mbaya sana mzee akung'oka)

Ila hili la Masha siko tayari kuunga mkono,na nina sababu zangu!Tunahitaji nidhamu na usiri wa vikao vinavyohusu nchi yetu,sasa kama kuna mtu ambaye anaweza kumfuata mfanyabiashaara na kumwambia mambo ya vikao vya juu,basi hastahili kuachwa!
Kama ni Masha alisema(wanavyoamini wengi) basi achukuliwe hatua,kama Mengi aliambiwa na 'Mzee MWanakijiji' basi aseme ili tukate mzizi wa fitina.

Kuan katabia ambako mie sikukapenda has akale ka kuwarekdoi wale wazee wangu wa kiisilamu.alitaka kuchochoa suala baya sana kuliko yote na kosa lake lilianzi hapo


Kwanza kabisa vikao vya siri vya serikali vya kumfilisi raia wake mwisho wa siku anapewa nishani aliotoa siri maana huu ni upuuzi sio wakufanyia vikao rasmi ni wazembe wa hali ya juu.
Pili inaonyesha jinsi hilo baraza lilivyo na mambo binafsi yasioyo kuwa na manufaa kwa nchi na ndio maana kila mmoja anaweka maslai yake mbele na wanamgawanyiko mpaka siri mbaya zinavuja.
 
Mkuu G,

Mie siku zote huwa nasimamia kwenye haki.kipindi kile Msoala kafnaya blunder nilimuunga sana mkono Mzee Mwanakijiji katika azimio lake na kama mnakumbuka tulisign makubaliano(Bahati mbaya sana mzee akung'oka)

Ila hili la Masha siko tayari kuunga mkono,na nina sababu zangu!Tunahitaji nidhamu na usiri wa vikao vinavyohusu nchi yetu,sasa kama kuna mtu ambaye anaweza kumfuata mfanyabiashaara na kumwambia mambo ya vikao vya juu,basi hastahili kuachwa!

Kama ni Masha alisema(wanavyoamini wengi) basi achukuliwe hatua,kama Mengi aliambiwa na 'Mzee MWanakijiji' basi aseme ili tukate mzizi wa fitina.

Kuan katabia ambako mie sikukapenda has akale ka kuwarekdoi wale wazee wangu wa kiisilamu.alitaka kuchochoa suala baya sana kuliko yote na kosa lake lilianzi hapo

Gembe

Kikwete amesema Tanzania itapata madhara kutokana na economic tamoil inayoendelea, wanakaa kujadili jinsi ya kumfilisi mtu...... na kuita siri, lini watatua matatizo ya uchumi na umasikini???

Wanafunzi wa vyuo vikuu, walimu, wazee wa EAC wameshindwa kulipa mafao ama ada zao mnakaa kumfanyizia mengi........ na kuita siri eti aliyevujisha siri atafutwe.... Nani ana gharamia hiyo operation????

wameshindwa kukamata mafisadi wa EPA, green Finance, Meremeta na mengine wanao muda wa kujadili kumshugulikia mfanyabiashara tena mpasha habari mkuu kwa umma, ni Lini mtakaa kutatua mambo mzito ya nchi yetu?????

Nashukuru kama mmeanza kulana wenyewe, maana mmoja wenu akianza kunukia kama mbuzi wa bangusilo, nae atamtaja mbuzi halisi ni nani, na mbuzi halisi wa bangusilo atasema chui na mbwa mwitu wa watanzania ni kina nani. Na hapo Masha na wengine watatiwa kikaangioni na wananchi
 
Jk amfute kazi aliyevujisha siri ya mkutano wa baraza lake la mawaziri. Inapaswa iwe kama alivyotendewa lowasa aliyesemekana kummegea siri mengi juu ya ule ugomvi wake na manji .

Serikali inapaswa idumu ktk usiri wa mipango mikuu ya kidola. Haiwezekani leo tunamjadiri fmes then kesho raia mwema front page au fmes anaenda ktk redio mbao yake na kupiga mkwara!!!!

Usalama wa nchi unatikiswa na aina hii ya ujasiri kiburi wa watu wa aina ya mengi.

Mkuu DRR.Jr
Siri sirini? Siri gani hizo? Hawawezi kutunza siri kwani wana mtandao hata madarakani waliingia kwa kuvujisha siri za wengine na zaidi kuzitumia kama propaganda. Wamejisahau sasa wanavujishiana wao kwa wao... Ukianza kula nyama na mtu huachi... JK Nyerere
job true true
 
Gembe mkuu acha kuleta spin zako hapa; Masha alimpa Mengi siku zaba atoe ushahidi wa allegations zake ama sivyo angemchukulia hatua kali{ NDIO MAANA YA ATAKIONA}. Sasa hizo saba zimepita zimekuwa kumi na mbilil ndio tunamuuliza Masha siku ulizompa Mengi zimepita je umekwishamshikisha adabu? Swali ni jepesi ingawa mlishaanza na spin zenu za hovyo kumsingizia Lilian!!
 
Mkuu G,

Mie siku zote huwa nasimamia kwenye haki.kipindi kile Msoala kafnaya blunder nilimuunga sana mkono Mzee Mwanakijiji katika azimio lake na kama mnakumbuka tulisign makubaliano(Bahati mbaya sana mzee akung'oka)

Ila hili la Masha siko tayari kuunga mkono,na nina sababu zangu!Tunahitaji nidhamu na usiri wa vikao vinavyohusu nchi yetu,sasa kama kuna mtu ambaye anaweza kumfuata mfanyabiashaara na kumwambia mambo ya vikao vya juu,basi hastahili kuachwa!

Kama ni Masha alisema(wanavyoamini wengi) basi achukuliwe hatua,kama Mengi aliambiwa na 'Mzee MWanakijiji' basi aseme ili tukate mzizi wa fitina.

Kuan katabia ambako mie sikukapenda has akale ka kuwarekdoi wale wazee wangu wa kiisilamu.alitaka kuchochoa suala baya sana kuliko yote na kosa lake lilianzi hapo

GEMBE NA FEMS NI WALE WALE WAACHENI HAWA WAENDELEEE KUTOONA MAKOSA YA MASHA( WANATIA AIBU) sijui wanafaidi vijisenti vya ufisadi wa huyu Masha dah
 
GEMBE NA FEMS NI WALE WALE WAACHENI HAWA WAENDELEEE KUTOONA MAKOSA YA MASHA( WANATIA AIBU) sijui wanafaidi vijisenti vya ufisadi wa huyu Masha dah



Jamaa wana bore basi tu kwa kuwa wanaandika na sisi tunawajibu kwa kuandika ndio ustaarabu wa hapa.Ila wanajaribu kila jinsi kupindisha mambo.Mwanzoni kule kwingine humu wa sauti za umeme alituambia kuwa serikali haina haraka sisi tukashangaa haina haraka lakini ndio yenyewe imetoa siku saba!
 
Una uhakika Gani kama Masha ameudanganuya Umma,AU umeshaenda Kumuuliza ana mpango wa kuchukua hatrua gani?siku zote tuwe wavumilivu na tupime jambo lenyewe huku tukisubiri maamuzi.

Alitumia sauti ya UMMA kumpa Mengi siku saba la sivyo angekiona. Je, wewe umashaenda ukamuuliza kwa nini alikurupuka kutoa siku saba. Kwanza tulimsubiri atoke majuu, sasa tena tumsubiri - ameingia mitini nini.

Umma unaouongelea hapa ni upi?

Ni ule UMMA uliomsikiliza akifoka TBC1, ni UMMA wa watanzania waliochoshwa na ubabaishaji wa watu kama Masha na ni UMMA huo huo unamtaka ajiuzulu.

Tayari hapa umeshasema masha alihusika kwa asilimia 99%.Wewe ndiyounao huo ushahidi na pindi utakapohitajika basi peleka maelezo yako kama alivyosema ndugu yangu zitto.Mengi angekuwa naujasiri angekuja mbele pale na kumsema wazi wazi mtu aliyemtaja kuliko kuweka siasa katika kuelezea jambo.

Ina maana kama itathibitika alihusika na wewe unaunga mkono Masha ajiuzulu ama utatafuta tena mengine. Mengi hakuweka siasa, amehoji utendaji wa ofisa wa juu serikalini na mwenye jukumu la kulinda mwananchi anapomgeuka huyo mwananchi na kuhatarisha usalama wake. Alofanya Mengi ni ujasiri wa kuigwa.

Kimya kingi kina mshindo mkuu,spika huwa na msemo mmoja anaupenda sana..Mtu mzima basi na yeye na Mengi inawezekana walikaa wakapima uhalisia wa jambo lenyewe na kuchukua maamuzi yenye manufaa kwa nchi yetu.MAsha siyo sawa na Ze comedy!

Masha angepima kwanza maneno yake kabla ya kukurupuka bila shaka angelinda heshima yake. Lakini kwa kitendo alichokifanya siwezi hata kumfananisha na Ze-comedy - hawa wako makini zaidi na wanafikisha ujumbe unaoeleweka.

Toa sababu za msingi ambaoz unadhani utajenga hoja masha ajiuzuru siyo kwa kuangalia jambo moja ambalo halina manufaa kwa nchi yetu.Suala la Ujambazi limekuwapo muda mrefu sana hapa nchini na chimbuko lake linajulikana sana.Watu tuna data tumekaa kimya!

Kuna ya Keko, ya Albino, ya IMMA, ya EPA, ya Ridhwani n.k. Haya yameongelewa sana humu ndani na nashangaa bado sijui unataka nini zaidi. Kama una data zimwage humu - hii ni JF ama huna ujasiri huo.

Usalama wa Rais umekuwa matatani toka lini?au kuna mipango uanyoijua wewe ambayo sisi hatuijui ya kumdhulu mkwere?

Umsahau Raisi kutupiwa mawe, Halisi kufungiwa, hofu ya kufikisha wezi kwenye sheria ... Kama kawaida yako dont bury your head in the sand, leave that to the ostrich.

Jambo lilitokea Mbeya alina tofauti na lilimpatya Bush Majuzi,Je waziri wa ulinzi wa marekani kajiuzuru.U are missing a point hapa.Usalama wa Rais hauko chini ya wizara ya Masha..waulize watu wa idara watakueleza

Acha spin wewe - ndio ninyi hao hao mnaopiga kelele siku zote tusiige mambo ya wengine. Kumbuka Bush anaitwa lame duck president na kuna Rais anayesubiri tu kuapishwa,

Kama umetumwa ,basi aliyekutuma hakujipanga vyema..

Yale yale - na wewe aliyekutuma nani na kama kujipanga kwenyewe ndiko huko mbona kazi. Unavyopiga kelele kutetea mafisadi kunajionyesha hata kwenye "font" unayotumia - ni ya kibabe.

wakulu,tuendelee kukata ishu!

Hapa tupo pamoja, tukate ishu tuache ushabiki, urafiki, uswahiba, ushikaji na vitu kama hivyo. Masha has to GO, period.
 
Huu mjadala inaelekea hauna mashiko kabisa kwa sasa na hautusaidii kama Taifa kwa sababu nyingi tu ila napenda nizitaje chache:

-Kama kuna sababu ya kumtaka Masha ajiuzulu inaweza kuwa si hii ya ukurupukaji wake kwa Mengi kwani ana mengi tu ambayo yatamfanya Muungwana afikiri upya kwanini asimuondoe katika nafasi yake ya sasa.

-Naamini na Masha anaamini kwamba haikuwa wakati mwafaka kwa kiongozi mwenye kuongoza wizara nyeti kama kama yeye Wizara ya Mambo ya Ndani kukurupuka na kujibu kauli ambayo haikuwa inamlenga mtu moja kwa moja. Wizara hiyo vyombo vyya ulinzi vyenye watu wenye busara na makini wenye taaluma za sheria na usalama ambao wangeweza kuachiwa wafanye kazi yao wakishirikiana na wenzao wa UWT.

-Kwa imani yangu hiyo wale wote ambao wanawapenda au wanatumwa au wanashabikia ama wana bifu zao na Masha ama Mengi watulize bongo zao na kuangalia Tanzania kama Taifa tunahitaji nini kwa sasa na nguvu zetu tuelekeze wapi badala ya kuendeleza malumbano ambayo hayajengi.

-Naamini na wengi tu wanaamini kwamba Mengi alipopata ushahidi wa alichokisema aliamua kukisema tena baada ya kuwa na imani kwamba nguvu waliyonayo watu kama Masha si dola tu bali ni nguvu zaidi ya dola na mijadala humu ndani inadhihirisha hili, kwa hiyo akaona kwamba nguvu yake pekee ni umma wa Watanzania ambao wakisikia na mukiendelea kujadili kama munavyoendelea humu hakuna atakayetekeleza jambo lolote kwa HILA. Mfano ni kelele alizozitoa wakati wa sakata la Malima bungeni, kelele za kumtaja EL ziliwafanya waliokuwa wakilambishwa asali wajue wameumbuka na wakashindwa kutekeleza azma yao kwa kuwa walikuwa UCHI tayari.

-Kama Mengi aliyoyasema yangekuwa si ya kweli, isingekuwapo hoja ya kumsaka mtoa siri na kama hiyo ndiyo SIRI ya serikali na si taarifa ya Kagoda, Meremeta, Deep Green, Mwananchi Gold basi TUMEKWISHA maana zote hizo ziliandikwa na kutangazwa na juzi mbele ya Masha na Makamu wa Rais, Meng alihoji "Kagoda ni mdudu gani" hadi Masha akageka na kumshangaa Mengi lakini hakutoa kauli ya kumtisha pamoja na kuwa kauli ya Mengi ni kali kuliko aliyoitoa kuhusu Waziri Kijana, ila ya Waziri Kijana inamgusa mtu binafsi na hivyo tunaaminishwa kwamba SIRI ama USALAMA wa Taifa ni SIRI na USALAMA wa VIONGOZI wachache.

Naomba na ninapenda kuona kwamba huu mjadala uzingatie MASLAHI ya Taifa na vichwa vya JF, yaani wale wenye uelewa mkubwa waangalie ni jinsi gani wanaweza kutuchangamsha na mambo mazito tuliyozoea humu JF.

JF ndiyo iliyosimamia kidete mambo yote mazito mapema kabisa kama Richmond, EPA na mengine ambayo bado yako katika mchakato na baadaye watu wengine kuyabeba sasa tusipoteze muda wetu kujadili watu badala ya vitu.

Kumekuwa na mambo mazito yanaendelea huko Dodoma, tumesahau kabisa kwamba wafanyabiashara kama Tanil walitoa mchango kwa UVCCM na walipelekwa na viongozi vijana bila kujali mustakabali wa vijana wa taifa hili. Tunafahamu mahusiano kati ya Tanil, Vithlani na viongozi wetu wa sasa hilo linaweza kuwa jambo muhimu kujadiliwa.

MUNGU IBARIKI TANZANIA, UWALAANI MAFISADI, INSHAALAH USHINDI UPO

- Mkuu Halisi, hapa tupo ukurasa mmoja na ubarikiwe!

Wazee wa sauti ya umeme, FMES.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom