Waga
JF-Expert Member
- Feb 6, 2008
- 322
- 14
1.
- Ahsante mkuu na heshima ikurudie pia, ingawa nilishamua kutoka hii mada lakini sina taizo kukujibu kwa kadri ya uwezo wangu wa kuelewa.
2.
- Ina maana msimamo wako huu ni kwa sababu una mgongano wa kimasilahi na waziri wa ndani, au?
3.
- Kutofautiana kwetu mawazo haina maana ya ushabiki wa anything, ila ni ku-practice demokrasia to the fullest, mtizamo wako ni kwamba hapa kuna kushabikia mtu, mtizamo wangu ni kwamba hapa kuna utata wa kisheria unahitaji kutatuliwa na pande zote mbili zipewe haki kisheria na ni lazima hii ishu iende kwenye sheria, kusiwe na anything less ili kupata ukweli wa kina na kwa faida ya wananchi in the future.
- Eti waziri wa jamhuri anachemka kwa kusimamia sheria za jamhuri ya kuwalinda wananchi wake ndani ya taifa?
4.
- Mkuu taifa limedumaa kwa sababu ya kutotii sheria, hakuna anayemkatalia Mengi kuwa ana uhakika na anachokisema, lakini ninasema hivi lazima kuwa na utaratibu kisheria, Mengi ana uhakika basi aupeleke kwenye sheria ili kama ni waziri mwenye makosa aabike not only kisheria bali hapa sasa hoja ya kumtaka ajiuzulu inakua na nguvu akifikia mahali akiabika kisheria,
- Sina tatizo na Mengi as individual anajua hilo, lakini nina tatizo kubwa na the way alivyoi-handle hii ishu, in fact toka ile ishu ya mashehe nilishaanza kua na wasi wasi naye na agenda zake, mkuu hili litakua ni taifa la namna gani ambalo wananchi watakurupuka tu na kuwarekodi wengine kwenye video na tapes, halafu kwenda kwenye media na kuwatishia nazo, wewe huoni kuwa huo ni u-Banana Republic? Sheria iko wapi?
- Sasa mwananchi anadai kuna waziri anamhujumu, kudai wkangu sheria itumike kuamua ukweli wa hii tuhuma kunanifanya niwe na beef na kampuni za Mengi? Hujanitendea haki hapo mkuu![/SIZE]
Mkuu Fmes heshima mbele as u used to say!
Hyo ni maono yangu tu mkuu na always huwa sipendi kudhulumu kile ninachokifikiria juu ya issue fulani, hayo niliyoyasema ndio ninayoyafikiria sasa kama nimekukwaza mkuu wangu naomba unisamehe ila niliyoyasema ndo nimeshayasema siwezi kuyabatilisha, ni matumaini yangu hujaghafirika sana mkulu wa kaya.