Mengi vs Manji: Ukweli ni upi?

tafiti then jadili

hiyo Press Release ya NSSF ilikuwa danganya toto ili kuzima issue.

Baada ya hii Press UCLAS walikuja juu sana na kukataa katu kuwa hawajawahi kufanya tathimini au kushiriki kwenye tenda ya kufanya tathimini. ALiyefanya hiyo kazi ni mtu binafsi ambaye ni mfanyakazi wa UCLAS na hakufanya tathimini hiyo kwa niaba ya UCLAS bali aliifanya kama kazi binafsi na haina uhusiano wo wote na UCLAS

Pili kuhusu tathimini ya Serikali kupitia Mtathimini Mkuu, Wizara husika ilikataa katu kufanya kazi hiyo. Kumbuka hata mpaka juzi Katibu kuu kwenye wizara husika alikuja juu kupinga hiyo kauli.

Hili swala ni lizito sana labda tulianzishie mada yake pekee.
 
Hii imewahi kujadiliwa hata huko lakini kwa kusua sua!

Leo nimesikia Manji amemwaga milioni 40 kwa wana Yanga! Anajifanya kuwa MJANJA SANA??!
 
Aljazeera said:
Hili swala ni lizito sana labda tulianzishie mada yake pekee.

Yeah,kuepuka kuchanganya mada kulikotokea... naona hii taarifa ya NSSF (+ associated comments) either ifunguliwe mjadala tofauti au ihamishiwe kule kwenye topic ya Nssf,quality Garage,mengi & Ippmedia iliyoanzishwa na Dr.Who
 
Aljazeera,

Uliyosema ni kweli kabisa na hata kulikuwa na mjadara mkubwa saana ndani ya wahadhiri wa UCLAS kuhusu swala hili, na ninaweza kuushusha kama itahitajika.

Kuhusu Manji kuifadhili Yanga, ukweli huyu jamaa ameona ili kujikinga na haya lazima ajibanze Yanga ambapo anajua hata JK ni mpenzi mkubwa mno ili apate wa kumtetea, na anajua fika Gulamali alivyoitumia Yanga kujipatia umaarufu, the same Dewji ameitumia Simba pamoja kuwa naye alifanya mambo ya ajabu saana katika kuua shirika moja enzi za ruksa.
 

Posting ifuatayo nimeikutauta Darhotwire forums.Ni kuhusu Mengi lakini aliyeiposti huko anaonekana dhahiri kuwa Mujahidina flani jast like huyu "Tafiti Then Jadili"

😕

JIHADIST AGENDA?
 
tafiti then jadili said:
Hii ni taarifa ya NSSF kwa vyombo vya habari ambayo Mengi na magazeti waliamua kuiblow out of proportion:

When it comes to allegations about corruptions they (the accused) can always rely on your staunch support and defence.
 

HIVI WEWE UMEFANYA UTAFITI KWA KIASI GANI KABLA YA KUJA KUTOA UTETEZI WAKO KWA WATUHUMIWA WA UHUJUMU WA UCHUMI WETU?UNALALAMIKA KUHUSU "EPISODE YA THISDAY/KULIKONI vs MANJI" WAKATI KUNA "EPISODE" NYINGINE ZIMEKUWA ZINAENDELEA MIAKA KADHAA eg IPTL SCANDAL,NA SASA HIZI POROJO ZA UTATUZI WA TATIZO LA UMEME.YOU HAVE GOT SERIOUS ISSUES AND I JUST CANT UNDERSTAND WHY DO YOU ALWAYS SIDE WITH THE UNSCRUPULOUS CHARACTERS (THE CORRUPT,BANDITS,THOSE MILKING OUR ECONOMY,ETC)

THE WAY TO GO IS NOT TO TAFITI AND THEN JADILI (THAT'S ALREADY PROVED USELESS.AND YOU ARE A LIVING EXAMPLE) BUT TO THINK OF TANZANIANS AS PEOPLE WHO DESERVE EVEN BETTER SERVICES FROM THE RULERS.
 
Mlalahoi said:
Posting ifuatayo nimeikutauta Darhotwire forums.Ni kuhusu Mengi lakini aliyeiposti huko anaonekana dhahiri kuwa Mujahidina flani jast like huyu "Tafiti Then Jadili"

JIHADIST AGENDA?

Mlalahoi, kwa jinsi hizo points na lugha zilivyofanana, inawezekana kabisa zikawa zimeandikwa na the same person au wanaofahamiana.

Uliponiacha tu ni hapo ulipoilink na ujahidina, maana so far sikuona kutajwa masuala ya dini katika hizo posts mbili.

Regardless of the "agenda' kama ipo, Vipi hizo points zina ukweli?
 
Mzee Tafiti,

Nimesema hivi hii habari siijui, sasa usinilazimishea tuuu ili upate kujiosha upuuzi wako, director wa NSSF nimemuona kwa macho yangu bungeni akiwa na Kingunge, na Malima, saaa za jioni, the next thing I know ni Malima kulivalia njuga hili suala, namba zilizohisuka na hayo majengo sizijui, halafu sio kwamba habari zikiandikwa kwenye magazeti ya bongo lazima kila mtu asome, tena huko bongo tuliacha kuyasoma siku nyingi huwa tunaingia huku na kupata data,

Sasa hivi niko NY, na nikaamua kuongea na mzito mmoja wa nchi kuhusu hiyo issue, sikusema kama wewe kuwa "NINAJUA", kama wewe ulivyosema kwenye hoja ya ubalozi wa UHOLANZI, ambako ulikamatwa kuwa hujui, mimi nimesema sina uhakika na hiyo issue na nimesema kuwa nikirudi bongo nitaifuatilia kwa makini, na nikaomba radhi kuwa hii issue haifanani na posting yangu ilipaswa kuwa kwenye Manji/Mengi, kwa hiyo posting yangu ni
tofauti na ya kwako ya kudai unajua wakati ulikuwa unajua dhahiri kuwa hujui, upokamatwa badala ya kuomba radhi ukaanza uabunuwasi kuwa ooh mimi nimekosa lakini wengine huwa hawakubali, NONESENSE!



sasa ninakuona unataka kunivuta kwenye hoja zako za kudai balozi ana-sexual relations na mama wa ki-sirilanka, ulipoambiwa kutoa ushahidi ili balozi arudishwe ukakaa kimya, ukasema Dr. Kitine ni form six, ukaambiwa hatujawahi kusikia form six akiwa lecture wa university Canada!, ukasema Mzee marehemu Mzena ni darasa la nne-nane, kumbe mzee amesoma na Lusinde na mzee Chiume, kule Makerere, hakukuwa na wanafunzi wa darasa la nne?

Niliposema kuwa habari za Sozigwa nimepata kwa kigogo mmoja, mbona usiseme kuwa ni za uongo? Mzee wangu nafikiri ulishagundua kuwa wazee wengi humu walishakuweka sehemu fulani na habari zako, ukalia sana kuwa Es akisema basi, wakakupinga kuwa huna ukweli zaidi tu ya kutetea viongozi wezi, sasa kama kawaida yako huwezi kuandika humu bila ya kulitaja jina langu, mzee wangu at this point wewe ni mjumbe tu kama wengine huna lolote special kama ulivyotaka kujifanya mwanzoni kwa kutumia jina langu, huwezi kuwa UK ukajua mambo ya bongo, yaani data hizo tuachie sisi wa kunyumba, au kukaye huku Ruvuma mpaka Maputo, au Matimila!

Na mzee wangu Nungwi,

kama hapa ndipo mahali pako pa kutafuta heshima, samahani sio wote tunaokuja hapa kutafuta heshima, mambo ya Freeman nilikwambia kuwa wewe unamjua sana, lakini CCM ndiyo iliyoshinda, uchaguzi tena ni 2010,

na kwa taarifa yako sasa ni kwamba Freeman ameamua kutogombea tena urais na atagombea ubunge tena Hai, sasa ameamua kuyasikiliza tuliyomwambia kwa siku nyingi ya kuimarisha Chadema toka ngazi za chini, kama CCM, ninayasema haya kwa sababu ninamfahamu bro, sasa kama hutaki itabadilisha nini?

Issue ya Manji pamoja na kutoijua kwangu, tayari ninajua kuwa analindwa na vigogo wengi wa serikali yangu ya CCM, kama ni billioni moja au 20, haibadilishi kitu! Kama hamna data za kujadili hii issue kubalini kushindwa lakini sio kutafuta mchawi ambaye hayupo!

Na Mzee wangu Mwanakijiji,

Ninajua kuwa ulikuwa unaitafuta namba ya simu ya PM, ili umhoji ni hii hapa cell yake # 0744-800-000, usipompata mpigie Akukweti kwenye cell# 0745-555-555, na ukitaka namba ya kigogo yoyote yule nitakupatia, au ukitaka kumhoji JM, cell yake ni # 784-544-544!, Kingunge ni # 0744-310-064,

kazi njema ndugu yangu!
 
Jaribu # 744-777-777, kama hupati nifahamishe nitakupa nyingine!, au msaidizi wake wa karibu sana # 748-783-996, ambaye atakupatia au kukuwekea appointment naye!

Kama haziendi nifahamishe nitakupa nyingine!
 
Mimi huwa sibishani na tafiti maana nilisha jua ni mbabaishaji wa makusudi ama kutokujua . Alipewa maonyo mengi lakini akawa haelewi naona wakati anaambiwa kuja hapa hakukaa chini nakutafiti kabla hajaingia hapa .Mwangalieni huyu maana anaweza kubishana hata na jiwe wakati halisema ama kibao ambacho kinaweza kukuonyesha toilet ni kule kwa mshale lakini chenyewe hakijawahi kufika huko chooni .
 
Duh,

Maskini topic ya nungwi imebadilishwa mpaka imevurugika sasa, imeenda NSSF na sasa imekuwa ni kumjadili/kumshambulia tafiti.

Nlikuwa na hamu ya kujua ukweli kuhusu hayo mabilioni yaliyopotea... maana to me the news was fishy.. na kulikuwa na 'rumours' kuwa ni kweli Mengi ameattempt hilo dili na likakaribia kushtukiwa. Sasa akafanya preemptive defence ya kutangaza kuwa kuna watu wametumia jina lake kuattempt wizi. Sasa nlitarajia wazee wenye data humu watazimwaga.

Inanshangaza sasa kuwa badala ya kudiscuss issues tunamdiscuss mchangiaji. Regardless of whether data kaleta tafiti au mtu mwingine, the issue is whether aliyoyaleta hapa yana ukweli au la, the message rather than the messenger.

Kwa mfano, ikiwa ni kweli kuwa Mengi kawaibia walemavu ... I don't see atashindwa vipi kutapeli hayo mabilioni. Ikiwa ni kweli kuwa anakwepa kulipa VAT na kodi nyinginezo, nae pia ni mhujumu wa uchumi ... no better than the other BANDTIS and CORRUPTS.

Kwa maoni yangu hii ripoti ya NSSF imekuja hapa kimakosa, hata hivyo .. badala ya kumshambulia mletaji ... ilikuwa tudiscuss ukweli/uongo/mapungufu ya ripoti hiyo.


My attempt to get us back to the topic.
 
Kulikoni

Ni kweli Mengi hana tofauti na wezi wengine kama akina Manji etc . Lakini hawa ndiyo wanao sikika kwamba ni wazawa . Issue hii ya Mengi iko polisi kwa upelelezi hakuna mwandishi wa habari anaweza kudiriki kwenda kwa DCI kuuliza mwisho wa upelelezi inapelekea kufa kifo cha kawaida kama ilivyo kwene kuwachunguza walio tuhumiwa kugushi vyeti na kuitwa ma Dr. kazi kubwa sana TZ media imelala na wanachi ndiyo kabisaaaaaaaaaaa
 
Kwa kuheshimu taratibu zetu za kidemokrasia nayapokea yote yanayosemwa dhidi yangu binafsi badala ya kujadili yale ninayopost some people have decide to go for the softer option in a discussion yaani kumjadili mjumbe badala ya ujumbe.

Inashangaza mambo yoooote ninayochangia humu ndani kama mwanachama mwingine yeyote mimi naitwa mtetezi wa wala rushwa!! yaani hii ni kali, nimeitwa mbishi kama jiwe yaani mzee mugishagwe licha ya kuamua kuwithdraw my comments kwenye ile topic uliyoweka na kukuomba radhi bado unaona kwamba mimi ni mbishi....katika kanuni za busara ni kujifunza wakati gani you have to move on...


Naam in the spirit of our mjadala kuhusu mabilioni yaliyopotea ambayo ndio mada halisi mshukiwa ni mengi au at least alitakiwa kuwa ni yeye manake haingii akilini kwamba pesa zote zile zipotee halafu kusiwe na japo mengi kuitwa katika kituo cha polisi kuhojiwa!

Jambo kuu ni kuwa taarifa aliyotoa yeye ni kuwa kuna watu wametumia jina lake kuanzisha charity na wamepokea misaada kutoka shirika la umoja wa mataifa ambapo jamaa wamepokea bilioni arobaini na moja na kutoa bilioni thelathini na tisa!

Taarifa hiyo ilisema vile vile kuwa Mengi ana account katika benki hiyo sasa maswali yangu ni haya kwa wachangiaji na mamlaka husika:

-Hizi ni fedha ambazo zilikusudiwa kutolewa kwa jamii nchini tanzania for good causes imekuwaje licha ya taarifa hiyo kutoka kwa NGUMA ambae ni company secretary wa IPPGROUP bado kusiwe na kauli yoyote kutoka POLISI,UN,NBC au serikali kwa ujumla katika taasisi zake za kuzuia ufisadi?

Tukumbuke hapa tunazungumzia takriban robo ya mapato ya serikali kwa mwezi!

- Mengi baada ya kuona kuwa kuna watu wametumia jina lake kuiibia UN and in other ways kuwaibia wananchi wa tanzania ambao kikhalisi hasa walistahili kuwa ndio beneficiaries wa hizi pesa kwa nini asitoe taarifa kituo cha polisi au relevant authority yeyote badala yake kukanusha tu.

Nimemjua Mengi for a long time kuamini kuwa anapenda kuonekana kama ni mtu wa watu mwenye kujali utu na maadili mema, kama raia mwema wa tanzania kwanini hakutoa taarifa kunakohusika au tu kuomba wahusika matapeli washughulikiwe?

- Benki ya NBC nayo inalake swali kwanini baada ya kuona jina la mmoja wa account holder wao [ripoti ilieleza kuwa mengi ni account holder hapo] wasijaribu kuhoji iwapo anataarifa na fedha au taasisi hii?

Ni basics gani zimetumika kufungua akaunti hii?

Nimeshawahi kuwa mwanachama, mwanzilishi na kiongozi katika taasisi kadhaa za hiari Tanzania na najua utaratibu ni kwamba unapofungua akaunti ya taasisi basi unahitaji kuwa na zaidi ya mtu mmoja kuweka sahihi zao na hao ndio wanakuwa authorised officials katika masuala ya fedha mara nyingi huwa ni mweka hazina na mwenyekiti au katibu na hawa majina yao yanafahamika wazi, sasa tuseme benki haiwajui hawa watu au vipi?

-Ili taasisi iweze kuqualify na misaada mizito kama mabilioni haya inabidi iwe na usajili katika ofisi ya msajili wa vyama vya hiari tanzania ambayo inaoperate chini ya wizara ya mambo ya ndani, nao wamekaa kimya!

-Naam kuna walakini mkubwa kwa waandishi wa habari tanzania kama asemavyo Mugishaghwe manake haya ni maswali nyeti yenye kuhitaji majibu, sifikirii kama watu wenye uchungu na nchi yao wataweza kuona kiwango hiki na kuturn another page bila kujiuliza maswali kadhaa....

Hivi hapa kuna nini, wananchi tunahitaji kujua pesa hizi....
 
Nungwi,

Kwanza samahani kwa kutokujibu mapema, jamaa walikuwa wananisumbua, ikabidi nipoe kidogo ili wanisahau.

Ninahaidi kuwasiliana na NMB kuulizia. Suala ni tata sana.

Kuhusu kujadili watu mi naona imekuwa kawaida humu, sijui kwanini!! Ila pia wakemewe waliokuwa wanapindisha topic kwa maksudi kabisa.

Ngoja nijaribu ndugu yangu, lakini mbele yangu naona harufu sio nzuri, nilitegemea magazeti ya this day na kulikoni yendeleze "episodes" za huo ujanja walifanyiwa bosi wao!!.

Imenishangaza kidogo.

FD
 

Yaani you just nailed it na natumai kutakuwa na majibu mapana na marefu na ya kina ambayo wana FORUM hii wanayo...kwani humu ni kama kisima cha ma PROFESA wa kufanya analysis bila ushabiki unaopendelea upande wowote
 
Hizi billioni 40 wamevuta wajanja wachache wa hapa mjini.Hizo pesa zilitoka UNAIDS. Na hio NGO yenye jina la Mengi ilianzishwa kwa ajili ya kuwajali watoto waathirika wa Ukimwi majumbani kwao,yaani watahudumiwa hukohuko makwao badala ya kuwa wanakwenda kwenye centers au zahanati.

Inasemekana kilichotokea mpaka IPP kushtukia ni query iliyotokana na hio account yenye hizo pesa.Mengi alipiga kelele sana,lakini baadae akawa kimyaaa,na habari zilizopo ni kuwa hao vijana walimkatia dola milioni 3.
Hao vijana sasa ndio matajiri wa kiafrika waoongoza hapa Dar,wamenunua majumba Masaki,Oysterbay...wana magari ya kifahari aina karibia zote,na magari yao huwa yanaletwa na ndege,sio meli!

Hili bomu sio rahisi kulipuka,kwa sababu;
-kwanza kwenye nchi ya kimaskini kama hii yetu kuwa na dola millioni 40,ambazo hazijaibiwa bongo hata hao wanaotakiwa kuku-prosecute watakutafuta urafiki.Uko mfano wa Franco Tromontano,ambaye ni mkurugenzi wa DTV,yeye hawezi kwenda ulaya,kuna arrest warrant kule Belgium,na walishaomba kuja kumtafuta hapa(sijui liliishia wapi).Yeye alipewa pesa kule kama mkopo sijui wa nini,akaja nazo huku,ndio wakaanzisha station ya TV na kiwanda cha kutengezea mafuta ya break na spring.Cha kushangaza baada ya habari hizo kutoka kwenye magazeti, kama mwezi baadae, akaonekana kwenye vyombo vya habari akilisakata rumba na Anna Mkapa,(wakati huo 1st lady)Ameji-embed kwenye TELEFOOD,hii sijui ni NGO au nini,lakini wadhamini wake ni yeye mwenyewe,Anna Mkapa,Jenerali Ulimwengu nk. Na mpaka leo anaonekana kwenye sherehe za viongozi na anaendelea na maisha yake kama kawaida,lakini ni mwizi!

-Pili,hii ni scandal kubwa kwa UNAIDS,kwa hio wao ni lazima watajaribu kulizima hili.Hizo pesa ni kutoka nchi hisani na kama bomu kama hilo linalipuka,they will be put under a microscope,na shady deals within the UN organisations ni mambo ya kawaida tu,(sio zamani sana kulikuwa na ile ya Oil for Food Programme ya Iraq...)kwa hio kazi za watu wengi zitakuwa at risk,kwa hio hatutasikia UNAIDS wametaka hao watu washikwe,wao watajaribu kwa kadri wanavyoweza kuonyesha kuwa hizo pesa zilitumika kama ilivyopangwa,ila ndio unakuwa ni mwisho wake hapo,hawatatoa pesa zaidi.Haya mambo yanafanyika sana within these organisations,ndio maana ikawa ni moja sababu ya Marekani kusitisha kutoa mchango wake UN,huko nyuma,lakini walielewana baadae.

Kwa hio uwezekano upo kuwa Mengi nae alifaidika,kwa sababu kelele zake zilizimika ghafla,na yule ni mfanya biashara Mchagga,kweli dola milioni 40 zipitie kwenye mgongo wake hivihivi tu,asione hata chenji!Lazima kavuta,lakini deal haikuwa ni yake.

-
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…