Membe: Msije Dar wakati wa ziara ya Obama

Membe: Msije Dar wakati wa ziara ya Obama

Dah saivi ukipita posta unaonekana bbc au cnn kazi kwetu waandishi wametapakaa
 
Mi ninachofurahia ni kuwa barabara yangu jana usiku imepigwa lami.

Leo asubuhi nimepita kitu lami mpaka raha.

Asante President Obama.
 
Kwa mie ninaekaa temeke itabidi nianze mazoezi ya kutembea kwa miguu.. Ina maana JK nae alivyoenda huko Marekani walifunga barabara na kuwaambia wananchi wasiende Washington DC..?
 
Waziri membe akiongea na cloud fm jana amewataka watu walioko mikoani ambao wangependa kuja kustarehe dar waarishe kwani hoteli zimejaa wageni na vilevile wananchi ambao hawafanyi kazi mjini ni bora wafute safari za kwenda mjini soma mwananchi
 
KAMJII...Kamekua sio JIJI tena..mweee Tunashindwa kuenea kwa ujio wa mtu mmoja!!!?? Je ingekuwa ni mkutano wa G8 Unafanyikia hapo Dar kwa siku 10 ,I ngekuwaje!!!??:whistle:
 
Anawaomba wasije dar sidhani kama anaamrisha watu wasije dar, kwenda sehemu hadi nyingine ni uhuru na haki ya mtu.
 
Mbona wanaifanya ziara hii kama vile ni ujio wa Yesu jamani?!!!!!! Yaani kama akija Obama matatizo yetu yote yatakwisha!!!!!!!Sasa mimi niko mkoani na kwangu ni Dar kwahiyo nisiende nyumbani kwangu kisa Obama? MY GOD THAT'S TOO MUCH. Maisha yetu yanatakiwa yaendele kama kawaida, wao wamarekani na matatizo yao ya kujitafutia maadui ulimwengu mzima KIVYAO....
 
Watangaze tu obama day watu tukale bata dar live au na huko nako wanapita?
 
Kauli za Membe huwa na utata siku zote,huyu hafai kabisa kuwa rais,ni mpayukaji bila kutafuta solutions za matatizo anakimbilia media
 
Eti tulisukume gari lake.
Ukiliona ushukuru Mungu.Si utaona.
 
Kaenda kuongea kwenye Radio ya waLiberali,,,wanamnyenyekea mtu ambaye anakuja kuwaibia kwa mikataba ya kina Mangungo.
 
Back
Top Bottom