Mkuu wangu siku zote kuwa mwepesi kutambua kwamba ubora wa binadamu huanza na hulka ya mtu na haiwezi danganya watu wote. Na hakika mimi sii mmjoa wa watu wanaopanda mkenge kirahisi..Huyo Chenge kapokelewa kwao kwa maandamano haina maana mtu mwingine yeyote atakaye pokelewa kwa maandamano sii mbora pia wala haiwezi kuwa kinyume kwamba asiyepokelewa kwa maandamano ndiye mbora. Mfano wako wa Chenge hauwezi kutumika kwa Membe na pia sidhani kama huo uongo unaozungumzia unakuhusu muda ulokaa naye wewe kumfahamu vizuri Membe zaidi yangu.
Mimi sikuwa na ukaribu naye (Membe) hivyo, wala wengine wote nilowataja hapo nyuma. Sikuwa karibu na kiongozi yeyote nchi ama Canada, still naweza sema mazuri ya kiongozi. Kisha basi sidhani kama wewe upo karibu na Membe ama unaishi naye Tanzania hivyo unamfahamu vizuri. Huna ukaribu huo isipokuwa ni chuki za kisiasa na PENGINE unatumiwa..Hii ndizo siasa za Bongo kwani huwezi kumwitta mtu mwongo pasipo yeye kukuongopea jambo iwe wewe ama Taifa zima. kibaya zaidi mnashindwa hata kuutaja UONGO wake hadharani maana mnayatunga ya fitna kama tamthiria za kiyahudi. Labda wewe nambie Aziz ambaye ni balozi leo France alipelekwa Canada kufanya nini, maanake wewe wajua zaidi! Na inahusu vipi na yeye kuwa mmoja wa viongozi bora (ubalozi) ambao mimi nimewapitisha.
Wewe nambie uongo wake, kakuongopea ama katuongopea nini? Huyu ni kiongozi ambaye anafuata msimamo wa nchi kimataifa, laukama Membe katunga sheria ama maamuzi kinyume cha sheria tupe somo...maanake hata Tarik Mohammed Aziz alikuwa foreign minister wa Saadam na ali represent nchi yake kama alivyoagizwa na nchi yake. Ukimwita Aziz alikuwa mwongo mnafiki na kadhalika hilo litakuwa juu yako kwani sii makosa yako kutofahamu. Foreign minister wa Mugabe, Mubarak, Bush, Obama na wengineo wote hufanya kazi zao kulingana na msimamo wa mtawala, kuwahukumu wao ni kutofahamu utawala..
Nimesema jamaa ni mtu safi na kiongozi bora mwenye upeo mkubwa ktk maswala mengi ya ushirikiano. Siwezi kumlinganisha na kiongozi mwingine yeyote katika nafasi hiyo kwani ndiye pekee ameweza kuleta mijadala migumu na yenye uatata akitoa msimamo wake kwa maelezo ambayo wewe na wengineo hamyapendi...
Mkuu wangu tuna viongozi wengi magalasha Tanzania, na sidhani kama unatumia kipimo chochote kwani umeshindwa kabisa kusema lolote linalohusiana na accussation zako. Tumia mfano wangu siku zote nikimponda mtu huanza na makosa yake kisha kuanduika kilichotakiw akufanyika..Hapo hufungua hoja ya kujadili lakini hizi habari za mwongo, pasipo kusema alikuahidi nini hakutimiza.... sijui ni mtu wa kujipendekeza na kadhalika... hii picha isokuwa na rangi kabisa kwani hakuna kiongozi wala mtu yeyote asiyejipendekeza, hii ni kwa sababu kila mwenye nafasi ya fulani hutegemea mtu ama watu wengine kumpitisha...Ndivyo system inavyofanya kazi iwe JK au Obama, biashara ama unyumba. yote huetegemea jinsi unavyotumia nafasi hizo na kwa maslahi ya nani..