Membe: Hatutawaomba radhi Rwanda


Kigogo....hapa suala si kumchokoza mtu, maanake huu sio mchezo wa kitoto wa kuputa watu wazichape! Kama nilivyokwambia hapo juu hii ni strategic move ya kuondosha balaa la vita katika nchi tunazopakana. Adha ya wakimbizi kutoka Congo sisi ndio tunaozijua, adha ya wakimbizi toka Burundi sisi ndio tulihangaika nazo, adha ya wakimbizi toka Rwanda sisi ndio tulihangaika nazo. Sasa suala la Burundi lilikwisha kwa msaada wa Tanzania na nchi marafiki baada ya lile jeshi la kabila moja kukubali mazungumzo na waasi kuanzia CNDD-FDD and FNL. Sasa Kagame hataki mazungumzo na waasi halafu anaweka proxy forces kule Congo. Hilo kimkakati halikubaliki.....!
 
Mbona hawaambii Marekani wapatane na ALQAEDA????????????
Au awaambie Nigeria Wapatane na Boko Haramu????????????????

Kwani hufahamu kuwa Marekani na serikali ya Afghanistan wana mazungumzo na Taliban....! Hufahamu kuwa Pakistan inafanya mazungumzo na kundi la marehemu Beitullah Mehsud....!
 
Kwani hufahamu kuwa Marekani na serikali ya Afghanistan wana mazungumzo na Taliban....! Hufahamu kuwa Pakistan inafanya mazungumzo na kundi la marehemu Beitullah Mehsud....!
JK ndo mshauri ama????
 

Pale DRC kuna makampuni ya Kimataifa kutoka Marekani,na mataifa makubwa ukipeleka jeshi katika nchi ambayo USA inamaslahi NCHI YAKO INALIPWA PESA na Serikali ya marekani.Na tumepeleka majeshi haraka ndani ya DRC,ili Rais wa Obama akifika Tanzania tumwambie,sasa tupatie fedha ya kusaidia kutuliza vita ndani ya DRC.

Unacheza na usanii wa Kibongo,lazima Obama achomolewe pesa.!!!!!
 
Hakuna kuomba Radhi.Naunga mkono msimamo wa serikali ya Tanzania.Pia ili kuepusha haya huko baadae Serikali ya Tanzania ifanye mazungumzo na vikundi vya Uamsho
 
Asante sana mkuu, kuna mijitu humu sijui ni mitusi au ni uelewa mdogo kwamba Tanzania isijiingize katika mambo ambayo hayaihusu. Kama ni mtanzania basi ana uwezo kufikiri mdogo sana. Utulivu wa Congo ni kitu muhimu kwa Tanzania, haitapokea wakimbizi ambao wanaleta tamaduni ambazo ni hatarishi kwa Tanzania, silaha na ujambazi, magonjwa, kufekwa misitu nk. Mtu mwenye mawazo hayo aende kigoma, biharamuro nk ataona athari nilizozitaja. Mimi namsupport Kikwete kwa asilimia mia.
 

hizi ni propaganda chafu za watusi na m 23 ! Siku zenu zinahesabika.
 

nafarijika sana ninapogundua kuna watanzania tunaloliona hili! Hatutakata tamaaa mpaka vibaraka kama kagame wakose pa kutokea.
 
Hizo ndio sera zetu za nje?
Nikuingilia sovereignity ya nchi nyingine ambayo tunapaswa kuomba radhi.
Kama Membe ataendelea kung`ang`ania kutoomba radhi,then Rwanda watatangaza mgogoro na sisi kitu ambacho kitashusha hadhi ya nchi yetu kimataifa.
Tuwe wepesi wa kukiri makosa sio ngangari hata kwa vitu ambavyo tumekosea.
 
wenje kauliza toka lini rais kikwete akawa msemaji wa fdlr, tunasubiri jibu kwa membe.

wanja sijui wenje....ndio yule matusi man? Kweli chadema chama cha fujo...hivi mpaka rais akipendekeza amani kwa jirani mnapinga wakati hapa tulipokea wakimbizi wa rwanda zaida ya 3,000,000 wakasababisha matatizo chungu mbovu...leo rais anapendekeza njianzuri ya kupatanza kuacha vita...chadema wana dhihaki hatua ya kikwete...
Mheshimiwa zitto hakika ni pekee yake mwenye upeo chadema nzima wengine...ni wapo tu .....siasa za maji machafu
 
Mkuu chukua tano, you are great thinker
 

Hata kama watatangaza mgogoro, so what? Tumia ubongo wako kufikiri Tanzania inapata athari kubwa sana kutokana na mgogoro wa Congo wewe nenda Kigoma utajua matatizo yaliyoletwa na wakimbizi. Tanzania imechoka kupokea wakimbizi wanaotokana na upuuzi wa Kagame
 
Kikwetu unanikosha mno, kuna mijitu humu sijui ndo michora mazombie kwenye paper zao . Posting zao za kipuuzi kabisa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…