Baba yako akigombana na jirani huwezi kusimama upande wa jirani hata kama jana yake alimkwida mama yako. Lazima utakuwa upande wake. Ndicho kimefanyika hapa. Ni busara ya kawaida.
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
Kafulie huko, hivi nyinyi mnapotaka congo iongee na majambazi wa m23 mnafikiria nini? Eti mnajidai mmekomboa rwanda mmekomboa kutoka kwa nani? Kagame anaweza kulinganishwa na Samora? Wacheni upuuzi. Vita vyenu vya kugombea madaraka vimetuletea balaa nchini kwetu kwa kukosekana amani sehemu za magharabi nyinyi kwa kiburi chenu mnaona sawa tu. Genocide mmejitakia wenyewe kwa uroho wenu wa madaraka, tumewastahi vya kutosha lakini hamuelewi kwa kiburi chenu. Haya nendeni kaongeeni na hao ndugu zenu rwanda sio nyinyi peke yenu kwanza wao ndio wengi.Ushauri wa JK haukuwa mzuri huwezi kukaa meza moja na jambazi. Ila kwa yeye anaweza maana anakaa nao anakula nao wale wa EPA wa RADA wote anaishi nao. Rwanda are serious hawamchekei mtu na ndio maana wanaendelea. Watanzania watu wa ajabu sana eti leo wengi mnamtetea. Hivi kila siku mnamponda kwa maamuzi yake yasiyo na mashiko leo mnamtetea nini sasa? kachemsha kachemsha na hajawahi patia PERIOD !!
Hapo sasa nimewaelewa kumbe ndicho mnachokifanya. Lakini mfano wako hauna mashiko baba si sawa na rais, kumbe ndo maana anafanya blanda mnamuangalia kwa sababu baba yenu. Baba anafananishwa na mfalme sio rais kaka.
this is coming from wenje???? one of those classless politicians waliojazana CDM anaongea upuuzi wowote kisa bunge lipo LIVE
this is coming from wenje???? one of those classless politicians waliojazana CDM anaongea upuuzi wowote kisa bunge lipo LIVE
Aitaka serikali ya Kagame ipatane na wapinzani badala ya kutumia mabavu.
Asisitiza Tanzania ipo tayari kuwapa ushirikiano kama ikiombwa.
Mi nashindwa kuelewa Kikwete ana maslahi gani na vita ya Kongo hadi kujiingiza kwenye migongano ambayo ni totally BASELESS. Au ndio ule uvumi kuwa Riziwani anataka kuingia kwenye biashara ya almasi na mbao za Kongo?
Membe na Kikwete wanaweza kuwa wanatafuta sifa kwa kuwa watu wengi wanapenda siasa za KI_GANGWE lakini kidiplomasia haiiweki nchi yetu pazuri. Huku Chini Malawi mgogoro hawajautatua, then wanatafuta ugomvi wa KUNUNUA na Rwanda, hatujui kesho itakuwa nani??
Mind you Tanzania ndio nchi yenye uchumi dhaifu na maendeleo duni kwa sasa kwenye ukanda wa Afrika mashariki huku bajeti yake ikiwa tegemezi kwa asilimia 41. Kwa uchumi huu wa hospitali hazina dawa na akina mama wanalala wanne wanapojifungua hatuna haja ya kutafuta migogoro na majirani. FDLR hawatuhusu sisi watanzania na ni matatizo ya ndani ya Rwanda kwa nini tujihusishe?? Je siku Kagame akiibuka na kumshauri Kikwete aende walau kutoa POLE kwa mjane wa Mwangosi, Kikwete atafurahi?? Mbona Membe na CCM yake hawajakaa kwa majadiliano na watu wa Mtwara kuhusu matumizi ya gesi but wanataka majadiliano kwenye nchi za watu?? Wajanja tumenusa kitu hapo...
Mkuu hana lolote anamtetea mjomba/kaka yake.