Membe amshukia KITINE, amfananisha na "Kingwendu"

.....uwezo wa Kitine kuongoza ni mkubwa several folds ukilinganisha na huyo Membe (Membe analifahamu hili kwa sababu huyu ni bosi wake pia), uwezo wa kitine ni wa demokrasia uchumi na wa Membe ni wa demokrasia siasa (u-kingwendu).... kwa hali tuliyofikia tunahitaji kiongozi atakayetutoa hapa alipotuachia huyu mkuu wa kaya anayemaliza muda wake ambaye uwezo wake pia ni wa demokrasia siasa!!!!!! Membe hata hiyo sauti inayoisema ikikuita kaa pembeni, nina amini watu wenye uwezo watajitokeza,........
 
Tumemuelewa sana,

Huu si muda wa fasihi na ushairi. Huu ni muda wa clearcut facts.

Akisema habari za sauti anaweza kumaanisha wito, wengine tutaona anatuyayusha tu na kusikia sauti ni dalili ya schizophrenia.

Hatutaki ushairi, tunataka uongozi.

- Sawa sawa hapa tupo pamoja for once!

William.
 
Hivi Membe anavyotuambia kwamba aligombea ubunge baada ya kusikia minongonezo hizo ni kauli za kutoa kiongozi mkubwa serikalini kama yeye? Tanzania bana ni zaidi ya uijuavyo. Hizo whisper ultras anazosema Membe kama zinamsaidia yeye hilo ni juu yake na maluweluwe yake yanayoendelea kichwani mwake. Lakini aliita waandishi wa habari bila aibu akasema hivo, dah. Anyway ni mwanaccm na hicho ndo chama kinachoongoza serikali. Mungu tunusuru hata kabla ya 2015.
 
... If you want to shoot shoot don't talk. Aliyetoa tuhumu amwage na majina ya wahusika, sio kusema 'kuna mtu fulani
 
- Mkuu PM vipi tena Kitine amemuita Membe, mwizi anayeficha hela nje agombee urais nazo, sasa akiitwa kingedu hutaki vipi? Una tatizo na Membe nini mkuu wangu, hafai kwa kosa gani hasa alilofanya kwenye policies zake akiwa Wizara ya nje?

- Kwenye kampeni za siasa kuchafuana ni kawaida, lakini hukalii kukumbatia ya zamani unasahau unaanza upya, I mean wacha chuki na Waziri Membe, kama ana makosa kwenye policies zake ziseme, lakini ya kampeni za siasa yalishapita sasa yupo kwenye kutawala, onyesha mapungufu yake kiutawala,

- Kitine hana u-senoir wowote ni simply muongo sana na ni mwizi, tena yeye na mkewe, ila kwa vile system yetu ni ya kusameheana ndio maana ana ubavu hata wa kuita wengine wezi, nashangaa mtu makini kama wewe kumuita a proven thief wa hela za wananchi kwamba ni senior, senior wa nini hasa? labda wizi wa hela za wananchi, wananchi wanakufa Muhimbili pale kwa kukosa dawa, wengine wanadanganya na kuiba hela za wananchi hao hao na kwenda nje kufanya shopping, wewe unamuita senior pleaseee!

- Waziri Membe na wananchi wote wa nchi hii wana haki ya kugombea anything, hawa kina Kitine ndio tatizo kubwa sana kwa taifa letu, maana ni majungu majungu tu alipokuwa usalama aliwahi kumakamata nani? PM wewe nakuheshimu sana kwani najua ni mtu makini sana lakini huwa una tatizo sana na mtu yoyote anayetaka uongozi CCM, isipokuwa Lowassa tu, huwa sikuelewi!


William.

Mtu unayejitia unashabikia utawala wa sheria yaani kila kosa lithibitishwe mahakamani, sasa hapa naona unajikanganya, naomba utueleze huyu 'proven thief' alithibitishwa na mahakama gani?
 
Willy hata afanyeje hatakuwa kiongozi nchi hii atabaki kuwa vuvuzela kwenye mitandao!!

Wala msimpe umuhimu wowote kwamba anaweza kuja kuwa kiongozi, alibahatika babaye , yeye asahau!
 
- Kamati ya Bunge kutokana na EVIDENCE zilizotolewa na Waziri Membe, kumbe ulikuwa hujui? No wonder!

William.

Hivi wewe unaishi nchi gani? toka lini kamati ya bunge ikawa ni chombo cha ku-prove guiltness ya mtu, inavyoeleweka kamati zinatoa mapendekezo/maazimio kwa serikali na serikali inachukua hatua within its limits then kama kuna mambo ya jinai ni mahakama ndo inathibitisha,kwa kuwa wizi ni jinai, je ni mahakama gani ilithibitisha wizi wake? acha porojo wewe, leo una msimamo huu kesho mwingine, hueleweki! una-pretend kuwa ni mpenda sheria kumbe na wewe ni 'Mr. Majungu' got you babe!
 
Membe ....bado yupo na senior wake ...kumuita kingwendu.....nadhani ,Kitine hakumpa majina ya kashfa wala kumtaja jina .....sasa kajihisi ...ukirusha jiwe gizani atakayelia limempata!!!! ...

Ikumbukwe kuwa kazi kubwa ya Membe "mzee wa fitina " mwaka 2000 kuelekea 2005 ,ilikuwa ni kuwachafua watu wote waliokuwa na nia ya urais ili kumsaidia KIkwete ...mhanga wa kwanza wa wanamtandao alikuwa..
Hassan ( hassy ) Kitine
iddi Simba
Frederick Sumaye
Salim Ahmed Salim

Hawa kwa wakati tofauti walichafuliwa vibaya na wana mtandao.......Huyu Membe urais ...hafai kabisa....eti anasema ...kuna watu ..wanataka agombeeee ...mbona hatuwaoni....au CCJ?
Membe mnatuficha wewe na JK ndugu wa DAMU. Tunaelewa mamake Kikwete ni mama yako pia.
Tukikuchagua tutakuwa tumechagua msanii namba mbili!! HATUKUHITAJI JOKA LA MDIMU.
 
Willy hata afanyeje hatakuwa kiongozi nchi hii atabaki kuwa vuvuzela kwenye mitandao!!

Wala msimpe umuhimu wowote kwamba anaweza kuja kuwa kiongozi, alibahatika babaye , yeye asahau!

- Nifungulie thread hii hahinihusu, Uongozi haulazimishwi kwa nguvu huwa unakuja wenyewe, so relax bro na hizi kelele za mlango!

William.
 
Hivi wewe unaishi nchi gani? toka lini kamati ya bunge ikawa ni chombo cha ku-prove guiltness ya mtu, inavyoeleweka kamati zinatoa mapendekezo/maazimio kwa serikali na serikali inachukua hatua within its limits then kama kuna mambo ya jinai ni mahakama ndo inathibitisha,kwa kuwa wizi ni jinai, je ni mahakama gani ilithibitisha wizi wake? acha porojo wewe, leo una msimamo huu kesho mwingine, hueleweki! una-pretend kuwa ni mpenda sheria kumbe na wewe ni 'Mr. Majungu' got you babe!

- Fungua thread yake sitakuruhusu kuvuruga huu mjadala kama kawaida yako!, ingawa naona hujui kwamba sio mahakama iliyomlipisha pesa alizoiba, uliza kwa wengine nani walimlazimisha kufanya hivyo?

William.
 
Mtu unayejitia unashabikia utawala wa sheria yaani kila kosa lithibitishwe mahakamani, sasa hapa naona unajikanganya, naomba utueleze huyu 'proven thief' alithibitishwa na mahakama gani?

Duh, mkuu yaelekea wewe ni mgeni hapa Duniani. Basi ngoja tukueleze haya juu ya huyu Kingwendu:

1) Alijaribu kusomea PhD miaka 7 Canada, akashindwa na kurudi na PhD ya kujisingizia. hajamaliza PhD wala hana PhD. Ni miongoni mwa wanaodanganya kwamba wana PhD, hiyo ni fact.

2) Kingwendu alitimuliwa madaraka na Nyerere baada ya kuchakachuwa gari 2 kati ya gari 6 zilizookuwa zimekabidhiwa Tz kutoka Sheli Sheli. hiyo nayo ni fact.

3) Kingwendu alimdanganya Mkapa hadi mkapa akaidhinisha dola $63,000 kupitia wizara ya afya (sio dola 50,000 kama wanavyokosea magazetini) kwa matibabu feki ambayo yalitengenezewa risit fake na jamaa wa Nijeria aliyekuwa anajilia uroda kwa mke wa Kingwendu Toronto. Kingwendu alipobanwa, akazirudisha dola $60,000 bila kuwaambia waTz alizipata wapi, kuona ameumbuka Kingwendu akahonga kamati ya bunge. Kamati ikala mkwanja na bado ikamwambia Membe, naye hakufanya ajizi akamwangamiza Kingwendu. Na hiyo ni fact.

Hitimisho: Kingwendu amtaje waziri anayemtuhumu ili ngoma hii inoge, vinginevyo ana kila sifa ya kuitwa Kingwendu, zee la majungu, na ushauri wanggu hasipewe hata sekunde 2 kwenye Tv au magazeti hadi hapo atakapotaja jina la waziri anayemshutumu. Yaani yeye anamjadiri mwizi dk 15 lakini ukimuuliza jina anasema "kafanye uchunguzi". Kingwendu at best.
 
- Fungua thread yake sitakuruhusu kuvuruga huu mjadala kama kawaida yako!, ingawa naona hujui kwamba sio mahakama iliyomlipisha pesa alizoiba, uliza kwa wengine nani walimlazimisha kufanya hivyo?

William.

hata wale baadhi waliorudisha fedha za EPA hawakuamriwa na mahakama! waliwasihi wafanye hivyo la sivyo mahakamani!
issue ya Kitine sina uhakika alirudisha fedha kwa kulazimishwa au kwa ridhaa yake so as to cut the long story short, na inavyoelekea it was a clean transaction na ndo maana wabaya wake hawalisemi sana hilo kama wewe mshadadiaji!
 
Nchi ya wabwatukaji tu...si waziri,si mkurugenzi wala yeyote mwenye kauwezo/nafasi ya kualika "media" waje kushuhudia akimsuta fulani...Nilidhani mzee Kitine muda wa utumishi wake TISS hadi kufikia ukurugenzi angekua na nidhamu ya kuzungumza,na kuweka vipaumbele vyake vya wapi azungumze nini na uhakika wa jambo analozungumzia! Membe as well,mashimo anayochimba ajiwekee alama asije kutumbukia mwenyewe!
 
Back
Top Bottom