Tume ya Katiba
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 4,896
- 1,866
WAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amesema mtu yeyote anayehitaji kugombea urais mwaka 2015 anahitaji kusikia sauti ikimwambia omba na si kukurupuka.
Membe alisema hayo leo jijini Dar es Salaam, wakati akijibu maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari likiwemo la kutajwa kuwania urais 2015.
Katika mkutano huo uliolenga kuzungumzia msimamo wa Tanzania kuhusu Jamhuri ya Watu wa Sahara Magharibi na Morocco, Membe alisema hajaisikia sauti ikiniambia omba urais ila kwa ubunge aliisikia.
"Mtu yeyote anayetaka kuomba urais 2015 anahitaji kusikia sauti ikimwambia kila saa omba, yani akilala sauti hiyo anaisikia na hata akitembea … kama akikurupuka lazima awe ameteuliwa na chama chake na kukubalika.
"Kwa upande wangu mimi sijaisikia hiyo sauti ikiniambia omba urais ila kwa ubunge niliisikia, hivyo nikiisikia nitawaambia," alisema.
Akizungumzia tuhuma zilizoelekezwa na mmoja wa viongozi wastaafu nchini kwamba anajenga hoteli nje ya nchi, alisema kuwa aliyezitoa tuhuma hizo hana tofauti na mganga anayedaiwa kutoa uchawi mkoani Lindi aitwaye Kingwendu ambaye amekuwa akitoa habari za kutatanisha.
"Kingwendu amekuwa akipita katika baadhi ya vijiji na kukusanya wananchi na kuwaambia anayeua watoto wenu ni mama mmoja ana macho mekundu, anakaa upande wa kushoto.
"Wananchi huenda kumkamata mzee na kumjeruhi na wanapokamatwa wanadai ni Kingwendu kawaambia wakati yeye Kingwendu akiitwa anasema hajataja mtu jina.
"Katika ngazi ya Taifa tumeweza kuwa na vingwendu wengi, hivyo ni lazima tuwawajibishe watu kama hao vinginevyo wataleta matatizo, kama tunataka kuwa na taifa lenye ustawi lazima tuwabane watu kama hawa wazungumze ukweli," alisema.
Membe alitaka atafutwe aliyetoa tuhuma hizo na ahojiwe ili aeleze ukweli na endapo atamtaja yeye ndipo ahojiwe huku akisisitiza kwamba kuwepo na vingwendu kutawatesa wananchi hivyo wanapaswa kuwajibishwa
Sosi:
HabariLeo | Membe- Msikurupuke kuwania urais 2015
Membe alisema hayo leo jijini Dar es Salaam, wakati akijibu maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari likiwemo la kutajwa kuwania urais 2015.
Katika mkutano huo uliolenga kuzungumzia msimamo wa Tanzania kuhusu Jamhuri ya Watu wa Sahara Magharibi na Morocco, Membe alisema hajaisikia sauti ikiniambia omba urais ila kwa ubunge aliisikia.
"Mtu yeyote anayetaka kuomba urais 2015 anahitaji kusikia sauti ikimwambia kila saa omba, yani akilala sauti hiyo anaisikia na hata akitembea … kama akikurupuka lazima awe ameteuliwa na chama chake na kukubalika.
"Kwa upande wangu mimi sijaisikia hiyo sauti ikiniambia omba urais ila kwa ubunge niliisikia, hivyo nikiisikia nitawaambia," alisema.
Akizungumzia tuhuma zilizoelekezwa na mmoja wa viongozi wastaafu nchini kwamba anajenga hoteli nje ya nchi, alisema kuwa aliyezitoa tuhuma hizo hana tofauti na mganga anayedaiwa kutoa uchawi mkoani Lindi aitwaye Kingwendu ambaye amekuwa akitoa habari za kutatanisha.
"Kingwendu amekuwa akipita katika baadhi ya vijiji na kukusanya wananchi na kuwaambia anayeua watoto wenu ni mama mmoja ana macho mekundu, anakaa upande wa kushoto.
"Wananchi huenda kumkamata mzee na kumjeruhi na wanapokamatwa wanadai ni Kingwendu kawaambia wakati yeye Kingwendu akiitwa anasema hajataja mtu jina.
"Katika ngazi ya Taifa tumeweza kuwa na vingwendu wengi, hivyo ni lazima tuwawajibishe watu kama hao vinginevyo wataleta matatizo, kama tunataka kuwa na taifa lenye ustawi lazima tuwabane watu kama hawa wazungumze ukweli," alisema.
Membe alitaka atafutwe aliyetoa tuhuma hizo na ahojiwe ili aeleze ukweli na endapo atamtaja yeye ndipo ahojiwe huku akisisitiza kwamba kuwepo na vingwendu kutawatesa wananchi hivyo wanapaswa kuwajibishwa
Sosi:
HabariLeo | Membe- Msikurupuke kuwania urais 2015