Membe amkosoa Magufuli

Membe amkosoa Magufuli

kwa hiyo uchafu wa Membe utawekwa wazi tu endapo atamshambulia kipenzi chakoPombe,
yani Membe asipomshambulia Pombe anabaki kuwa msafi.

Ngoja NIJIRIDHISHE Kwanza Kama Hayo Maneno Kayatoa YEYE KAMA YEYE au Mwananchi WAMEANDIKA Tu KUCHOCHEA VUGUVUGU LA UHASAMA Ndani Ya CCM. Ila Kama Ni Kweli KAYASEMA Hakyanani NITAFUNGUKA HADI YASIYOJULIKANA ( Kama Noma Na Iwe Noma ). Narudia Tena WASEMENI Wote Lakini Siyo MALAIKA Wetu Na Chaguo La Mungu Rais Dr. MAGUFULI. Na Ndiyo MAANA Tunataka Kwa UDI NA UVUMBA AKABIDHIWE CHAMA UPESI ILI ATURUDISHIE CCM YETU YA HAYATI BABA WA TAIFA Mwalimu Julius Kambarage Burito Nyerere ILI ATUONDELEE AKINA " CCMUKAWA ", " CCM CHUKI, FITINI NA HARIBU " Na " CCM TETEA UFISADI KWA GHARAMA YOYOTE ILE " Ambao WAPO WENGI SANA CHAMANI.
 
Ni kweli JPM atakwenda nje ila anataka ajipange kwanza. Sasa unaanzajw kukimbilia nje bila kuweka mambo sawa. Ni.mapema mno kusema hataki kwenda nje
 
Haya sasa Balozi Sefue, Olesendeka na Bulembo iteni press mumjibu Bernad Membe.
Ukiwa ccm ni marufuku Kutumia akili yako....MEMBE alipokuwa Waziri akitetea Safari za JK alipoingia MAGUFULI aliziponda sasa Ameibuka tena kuponda nadhani kuna mahari kabanwa....Ingawa ana Hoja issue nikwanini hakusema mwanzo wa Utawala wa Magufuli au alikuwa anasikilizia kwanza....Huyo SEFUA na SENDEKA watasikiliza Sauti ya Tumbo itakavyosema...nawao utawasikia tu
 
“Lakini unaweza kuwa na idadi hiyo hiyo ya mayai na ukaamua kuyagawanya; mayai matatu unayaweka kwenye mfuko mmoja, mawili kwenye mfuko mwingine na yaliyobaki kwenye mfuko mmoja. Maana yake ni kwamba utaendelea kuwa na mayai kumi lakini idadi ya mifuko imepungua. Hapa sasa utakuwa hujapunguza gharama za kuyatunza hayo mayai."

Si kweli!!! gharama imepunguzwa kutoka kuwa na mifuko 10 hadi mifuko 3 au 4 tumeokoa fedha ya kununua mifuko

“Lazima utakwenda mwenyewe au mawaziri wako na hasa Waziri wa Mambo ya Nje kwa sababu kuna vikao nje ya nchi ambavyo mabalozi hawaruhusiwi kuingia.

“Ukijaribu kujifanya kisiwa utakuwa kama Zimbabwe. If you isolate yourself you will be isolated (ukijitenga, utatengwa).”


Ina maana Membe hajui kuwa siku hizi kuna TEKNOHAMA? Iwapi maana ya video
Conferencin.....?

 
Kwani Membe ana cheo gani nchini kwa sasa...hana haki ya kutoa maoni na sio lazima yafuatwe...Tayari rais ana jopo la mawaziri wasomi, makatibu wasomi na hata washauri wengi wa uchumi...so sio lazima.....Ilimradi sie tunataka tuone matokeo na ahadi zake za maendeleo zitekelezeke baasi...na nchi ikue kiuchumi....Hayo ya kupunguza au kuongeza au kusafiri nje sie hayatuhusu
 
Bulembo na Ole Sendeka wasiishie kumjibu Makongoro wamjibu na huyu
Membe atuachie Rais wetu, kama anaona inamuuma sana, atafute malimao akamue tani nzima anywe ili kichefuchefu kimtoke. Rais ni Magufuli yeye asubiri kutumbuliwa tu.
 
Huyu bwana naye ni jipu la uso. Yeye yuko sahihi kutokuona madhara ya kusafiri hovyohovyo kwa sababu ndiye aliyekuwa mshenga wa safari za holela, sasa amwache ngosha afanye kazi, kama alikuwa na mapendekezo mazuri juu ya safari hizo mbona hatukuyaona wakati wa uwaziri wake?
akumbuke kila zama na kitabu chake, sasa ndio kwanza tuko kwenye yaliyomo kwenye kitabu cha zama za ndg. Magufuli, hata sura ya kwanza hatujafungua washaanza kusema kitabu kibaya?
 
Back
Top Bottom