Tatizo la chama chetu hakipendi mawazo tofauti! mtu akisimama na kutoa mawazo tofauti anakuwa adui. Ndio maana nchi haiendi. Membe aachwe aseme tu anachotaka kusema, na wana "Kidumu" wengine pia waseme. Wengine wakosoe, wengine waunge mkono na kusifia, na serikali iangalie mawazo yote na kuchukua yenye manufaa na kuacha yale inayoona hayana maana. Na Ukawa nao waaachwe waseme, wakosoe nk. Na mwanahalisi na Mawio nao waseme.... Hiyo ndiyo demokrasia. Katika mengi yanayosemwa (kuna yatakayotufurahisha na mengine yatachukiza). NI muhimu kuvumiliana. Hatuwezi kuwa na nchi yenye watu wanaokubaliana katiuka kila kitu. Hii itakuwa nchi ya wajinga.