Mchungaji Gwajima: Daudi Albert Bashite alipata division Zero

Mchungaji Gwajima: Daudi Albert Bashite alipata division Zero

Habari kwenu wanajamiiforus!
Awali yote napenda niseme kuwa Mimi ni Miongoni mwa watu ambao bado wanamkubali na kumuunga mkono Ndugu Rais Magufuli na nasema hili ili ieleweke kuwa sio tu wale wanaotizamwa kama hawamkubali Rais ndio wanaotafakari na kufurahi Haki na usawa ukitamalaki, leo na mimi nimeona niandike kuhusiana na suala la Vyeti feki, na hoja ya mtumishi wa umma kuwa amevunja sheria na bado akiwa Kazini.
Hoja yangu ni kuhusu namna Serikali inavyolichukulia suala la hoja ya mkuu Wa mkoa wa Dar Es Salaam kuwa alitumia cheti cha mtu cha kidato cha nne, Masikitiko yangu makubwa ni kuwa:-

1. Rais amekuwa siku zote ni mtu wa maamuzi ya haraka na kwa wakati, lakini katika hili amechelewa sana sana kulichukulia uamuzi unaostahili, watumishi wengi sana sana waliacha kazi na wengine kukamatwa kwa kutumia vyeti feki na Kwa sasa wanashangaa kuona kwa nini Rais na Viongozi wengine sio wakali na kujiuliza kama Serikali huangalia vyeo katika kufanya maamuzi.

http://m.ippmedia.com/sw/habari/kiama-wenye-vyeti-kuwa-mwezi-huu

2. Kuanza kuzuka kwa taarifa mbalimbali kuhusu kutumika kwa jeshi la polisi katika kuadhibiti watu au mtu anayeonekana kutaka kuonyesha unaodaiwa kuwa ni ukweli kuhusu vyeti vya Mkuu Wa mkoa wa Dar Es Salaam, kitu ambacho kimeanza au kitaanza kuichafua Serikali na taasisi zake.

3. Kuanza kudharaulika kwa taasisi ambazo huhusika na kutafuta, kuchakata na kutoa taarifa kuhusiana na mtu anayeweza kuwa Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama.

4. Kuibuka hisia za ukabila na ukanda kwa watu wanaotajwa yaani mamlaka ya kuteua na kuteuliwa kwa kuwa ni wa kabila na ukanda mmoja, Jambo hili limeanza kuhuzunisha watu na hata wengine wanaona kama ndio sababu ya mamlaka kuchelea kufanya maamuzi kwa wakati.

5. Kuibuka kwa hoja ya kupuuzwa kwa Wapiga kura na wananchi ambao Rais amekua akisema wamemtuma kuwafanzia kazi, Mamlaka imeonwa imekuwa nzito sana sana.

Kwa hoja hizo za masikitiko yangu napenda kuiomba mamlaka ya uteuzi kutosita na kuona kuwa labda ikichukua hatua za kuhusu vyeti itadharauliwa na watoa hoja, nikimaliziamalizia napenda kuisisitiza Sana Serikali ichukue hatua za kumsimamisha kazi mkuu huyo wa mkoa ili uchunguzi ufanyike(utaratibu wa kawaida).lakini pia wale watafutaji na wachakataji wa taarifa wasione aibu labda ya kuonekana labda hawakuchakata na kuchunguza vizuri kuhusu Ndugu tajwa na huwenda labda walitajiwa tuu na marehemu wakaona anafaa bila hata ya kujiridhisha. Kwa sasa nawashauri wachukue hatua kulingana Sheria.
Mkuu wa mkoa pisha uchunguzi uheshimike na Serikali ionekane haiangalii vyeo katika maamuzi.
Wako katika hapa kazi tu.
Hmjamii
 
Kweli dar ni dar na kolomije ni kolomije, haya angeyafanya kolomije wala isingekuwa nongwa.

hahahaaaa...mkuu nimecheka hadi machozi yamenitoka.Nikisikia hako kajina kolomije najikuta nacheka tuuu ukiongeza na Daudi Bashite naishia kugalagala down kwa cheko la nguvu...
 
Jama mwanivunja mbavu nyie...hapa nilipo watu wanishangaa ninavokenua meno yangu makubwa huku nikisindikizwa na cheko La kiutu uzima.Maneno "kolomije na Bashite yanatawala kinywa changu.Anamletea mzaha mwanakijiji mwenza gwajima?
 
Ni kweli, huyu bashite anatakiwa kuwajibishwa ili kutoa funzo kwa wateule wengine.
 
amemteua mama salma angalau daudi atapumzika kidogo kujadiliwa manake watanzania wepesi sana kusahau
 
Inaweza kuwa ni kweli lakini sioni mantiki kwa anayejiita mtumishi tena wa Mungu kuendeleza vita. Siku zote watumishi wa kweli humkabidhi Mungu vita vyao. Daudi akasema Mungu pigana na wanaopigana nami...zaburi 35:1b

Hato hayatuhusu sis wananchi. Kuna wengine hawana Dini. Nchi inaendeshwa kwa sheria . Sheria inaruhusu kughushi vyeti??
 
So what? Uteuzi wa rais ni wa kisiasa? Au kielimu.. Hao wenye masters wamethubutu kufanya nini? Kikubwa?! Nitamshangaa pia JPM akisikiliza ushauri kama huu.

Kiongozi TZ anaruhusiwa kughushi vyeti. Labda nirekebishe. Mwananchi yoyote anaruhusiwa kughushi vyeti kuingia chuo?? Hilo ndio swali la msingi namab moja. La pili, kwa sababu hakustahili kwenda chuo, vyeti vyake si halali. Je, kwa amefikia hata minimum requirement za elimu kuwa Mkuu wa Mkoa kwa darasa lake la saba (allegedly)? Kwa kweli siwaelewi mnaotetea. Mnaonewa alafu mnafurahia. Wewe ukifanya hivi unafikiri utapona?
 
Naamini kuwa wapo wanasheria weledi wa masuala mbalimbali ikiwemo yanayohusiana na kughushi vyeti!
Ninashauri hii kitu ipelekwe mahakamani lifunguliwe jalada juu ya hizi taarifa Makonda za kughushi vyeti!
Mahakama ndio njia pekee itakayoweza kuthibitisha taarifa hizi kama ni za kweli ama la!
Naona Necta na Ndelichako wapo kimya sana.
Makonda apekwe mahakani kule awasilishe nyaraka zote zinazohusiana na elimu yake, na ili ikithibitika hakufoji basi anaweza kusafishika, lakini endapo itabainika kafoji basi sheria ichukue mkondo wake!
Mkuu wa mkoa ni kiongozi mkubwa hasa ikizingatiwa huyu Makonda anaongoza watu zaidi ya mil5 halafu anakumbwa na kashfa kubwa hivyo!
..wanasheria pelekeni mahakani!
 
Daudi Bashite kaforge huku Ndalichako, Kairuki kapigwa ngazi na walijitia kukagua wengine vyeti na wameacha kazi, hili swala likifika pia bungeni itakuwa vizuri zaidi, Daudi Bashite ni mwalifu mkubwa
 
Naamini kuwa wapo wanasheria weledi wa masuala mbalimbali ikiwemo yanayohusiana na kughushi vyeti!
Ninashauri hii kitu ipelekwe mahakamani lifunguliwe jalada juu ya hizi taarifa Makonda za kughushi vyeti!
Mahakama ndio njia pekee itakayoweza kuthibitisha taarifa hizi kama ni za kweli ama la!
Naona Necta na Ndelichako wapo kimya sana.
Makonda apekwe mahakani kule awasilishe nyaraka zote zinazohusiana na elimu yake, na ili ikithibitika hakufoji basi anaweza kusafishika, lakini endapo itabainika kafoji basi sheria ichukue mkondo wake!
Mkuu wa mkoa ni kiongozi mkubwa hasa ikizingatiwa huyu Makonda anaongoza watu zaidi ya mil5 halafu anakumbwa na kashfa kubwa hivyo!
..wanasheria pelekeni mahakani!
Mkuu move on,ili suala limeishia hapo.
 
Back
Top Bottom