Haliwezi kuishi hivi hivi aisee...Mkuu move on,ili suala limeishia hapo.
Kabisa mkuu...!Ujinga wa kuongozwa na vilaza haukubaliki.
Naamini kuwa wapo wanasheria weledi wa masuala mbalimbali ikiwemo yanayohusiana na kughushi vyeti!
Ninashauri hii kitu ipelekwe mahakamani lifunguliwe jalada juu ya hizi taarifa Makonda za kughushi vyeti!
Mahakama ndio njia pekee itakayoweza kuthibitisha taarifa hizi kama ni za kweli ama la!
Naona Necta na Ndelichako wapo kimya sana.
Makonda apekwe mahakani kule awasilishe nyaraka zote zinazohusiana na elimu yake, na ili ikithibitika hakufoji basi anaweza kusafishika, lakini endapo itabainika kafoji basi sheria ichukue mkondo wake!
Mkuu wa mkoa ni kiongozi mkubwa hasa ikizingatiwa huyu Makonda anaongoza watu zaidi ya mil5 halafu anakumbwa na kashfa kubwa hivyo!
..wanasheria pelekeni mahakani!
Halaumiwi kwa kuendesha vita dhidi ya mihadarati! (Wanaomlaumu wanakosea) Bali atalaumiwa sana kwa kusemekana kutumia cheti kisicho chake na ameshindwa kukanusha wala kuthibitisha kitu kinachopelekea watu waamini kuwa tuhuma ni za kweli! (Kuwa kimya maana yake ni kukubaliana na tuhuma)Kweli ndugu Wanga, mtu akilaumu na yeye atalaumiwa, akihukumu na yeye atahukumiwa. Makonda yeye alishughulikia madawa ya kulevya na sasa watu wanamsakama kwa yanayodaiwa kuwa ni kasoro katika vyeti vyake. Hivi asingesema neno juu ya madawa ya kulevya haya tungeyasikia? Kwa hiyo viongozi wetu wafumbe vinywa vyao waache kuufanya uongozi kwa kuwa wakisema neno nao watasemwa? Makonda angekuwa anatumia madwa ya kulevya ingeeleweka kama watu wangemshutumu kwa shughuli hiyo? Lakini hatuna habari kama anatumia. Hata kama hana vyeti sahihi (mimi sijui ukweli upo wapi), basi asihukumiwe kwa sababu alijaribu kusema kitu juu ya madawa ya kulevya na hatima ya vijana wetu nchini.
Mr. Wanga umechukua mkondo unaofaa kurekebisha mtiriririko wa shutuma kwa Ndugu Makonda. Nimekuelewa kuwa unataka watu wanaomlaumu wawe "fair". Ni kama umewauliza hao wanaomtuhumu kuhusu vyeti vyao wenyewe vikoje? Hata kama vyeti vya mtu ni vizuri lakini sijui kama ni sawa kuvishambulia vyeti vya mtu mwingine kwa kuwa tu amesema kitu juu ya madawa ya kulevya. Ikiwa mheshimiwa atavitoa vyeti nadhifu vya taaluma zake hawa wanaosema sana watakuwa na lililobaki la kusema?
Nakumbuka shauri la Rais mstaafu wa Marekani Mhe. Barack Obama alivomaliza kejeli za kuzaliwa kwake baada ya kutoa cheti sahihi cha kuthibitisha kuwa yeye alizaliwa Marekani; na ni Mmarekani kwa maana hiyo na hivyo kustahili kuwa Rais wa Marekani. Utendaji wa Obama leo unalinganishwa na ule wa mkosoaji wake mkuu Mhe. Donald Trump (Rais wa sasa wa Marekani) na unaonekana ulikuwa bora hadi kipindi hiki pamoja na kushutumiwa juu ya cheti chake cha kuzaliwa. Nisingependa kumsisitiza Mhe Makonda kutoa vyeti vyake vinavyozungumziwa, hiyo itakuwa ni kuicheza ngoma ya wakosoaji wake. Yeye achape kazi kwani anajua ni nani alimweka hapo na kwamba mpaka anaipata nafasi hiyo utaratibu unaotakiwa ulifuatwa.
Halaumiwi kwa kuendesha vita dhidi ya mihadarati! (Wanaomlaumu wanakosea) Bali atalaumiwa sana kwa kusemekana kutumia cheti kisicho chake na ameshindwa kukanusha wala kuthibitisha kitu kinachopelekea watu waamini kuwa tuhuma ni za kweli! (Kuwa kimya maana yake ni kukubaliana na tuhuma)
Historia itamkumbuka kama shujaa kwenye vita dhidi ya madawa ya kulevya na kanjanja wa elimu aliyewahi kuwa *C!
Imeniumiza sana MTU niliyekuwa nampigia upatu humu kama shujaa wa Taifa kumbe ni kanjanja wa elimu! Vinginevyo aweke wazi majina yake na vyeti toka primary hadi chuo kikuu!
MTU akitaka kujidanganya mwenyewe na adhani kuwa ni untouchable! Hayupo hata mmoja! Wako wapi kina Ghadafi, Sadaam Hussein, Mobutu! Wote hao enzi zao walidhani ni untouchables! Wote mnajua walivyokuja kuadhirika! Ukitenda haki unakuwa jasiri kama simba vinginevyo hata watoto utashindwa kuwatazama machoni!Katika hii nchi kuna watu ambao ni UNTOUCHABLES!
MTU akitaka kujidanganya mwenyewe na adhani kuwa ni untouchable! Hayupo hata mmoja! Wako wapi kina Ghadafi, Sadaam Hussein, Mobutu! Wote hao enzi zao walidhani ni untouchables! Wote mnajua walivyokuja kuadhirika! Ukitenda haki unakuwa jasiri kama simba vinginevyo hata watoto utashindwa kuwatazama machoni!Katika hii nchi kuna watu ambao ni UNTOUCHABLES!
MTU akitaka kujidanganya mwenyewe na adhani kuwa ni untouchable! Hayupo hata mmoja! Wako wapi kina Ghadafi, Sadaam Hussein, Mobutu! Wote hao enzi zao walidhani ni untouchables! Wote mnajua walivyokuja kuadhirika! Ukitenda haki unakuwa jasiri kama simba vinginevyo hata watoto utashindwa kuwatazama machoni!Katika hii nchi kuna watu ambao ni UNTOUCHABLES!
..Chini ya Mwembe huo, (yaani kabla ya kuvuka Mto Uenge ukielekea Uhuru) palikuwa panauzwa Tangawizi saa za jioni..Miaka hiyo pale NATA hotel kwa pembeni kulikuwa na mwembe. Jirani na ile temple ya wahindi.
Unaikumbuka Soweto?