Wadau na wanaharakati, hii issue ya Nay wa mitego ilikua ni mpango wa kuwatoa wananchi kwenye mapambano ya kuhoji vyeti vya kijana kutoka Koromije.
Serikali yetu inatambua udhaifu wa wananchi wake, hawachelewi kupuuza mambo ya msingi, na hawawezi kwenda na beat mpaka mwisho..
Baada ya kuona mambo yameshika pabaya, na Baba hawezi kufanya maamuzi magumu juu ya aibu hii, wakaamua kujitoa ufahamu juu ya habari ya Nay... Sasa wananchi wamehamisha mawazo yao yapo kwenye mshangao na kuacha agenda ya vyeti vya Bashite...
Jamani wadau na wazalendo wa kweli naomba tukaze uzi lazima kieleweke....
Nimeshuhudia mzee mmoja akitemeshwa kazi akiwa anasubiri miezi 4 kustaafu, kwa ajili ya vyeti fake, huku akikosa mafao yake yote ya miaka 35 aliyotumikia kazini,.. Kwann Bashite awe salama na wengine wakiwa wameumia? Aluta kontiniua....Bashite weka vyeti.