Mchumba wangu katolewa kizazi

Mchumba wangu katolewa kizazi

m nadhan mjadili hili suala kiundan we we na mwenzi wako. kuwa kama mtaoana kuhusu watoto itakuaje, km ikiwezekana mnaweza hata kuadapt mtoto mkamlea akawa wenu. kwa sababu sidhan km ni vyema ukamkimbia kisa hilo tatizo. kwan kabla hujafa hujaumbika. mjadili kwa upana sana hilo jambo kabla ya ndoa.
 
Kama ndoa kwako sio kwa ajili ya watoto muoe, lkn kama familia ni muhimu basi usimuoe ili kumuepushia maumivu ya kuchepuka na kuzaa nje

Mtihani huo...maana malengo watu wanakuwa nayo mazuri tu mwanzoni...wakikaa miaka say 10 unashangaa mtu kabadili mawazo...labda waanze kabisa na kutafuta watoto yatima wa kulea...lakini wakisema wakae peke yao, lazima watachemsha...

Na kiafrika ndugu...ndugu wanaharibu sana yani....ukute familia ya mwanaume wawe waelewa...lakini kama ni wale wale...nao wanaweza kuwa chanzo cha kukuza tatizo siku za usoni...
 
You have made an impressive point I must say, but that is if you believe we are the same as other species.
Humans are not the same as other species(@ least that is what i believe). And by saying that we are not entirely guided by the laws of science which by the way are not complete because they were put by men and we haven't entirely understood how things in this world works.

The laws which I believe in dictates in Genesis 2: 18 The Lord God said, "It is not good for the man to be alone. I will make a helper suitable for him."

No children were dictated in that equation when God decided to give Adam a wife. Walibarikiwa baada ya kuunganishwa ndio wakaambiwa wakazae. Ila Mungu hakumuumba Eva kwa sababu Adam alitaka mtoto.

Kama umeamua kuishi kama wanyama ni kweli ili specie yetu iendelee tunahitajika tuzae na tuzae...
Na kulingana na laws za evolution (You either change or die) Huyo bi dada hastahili kuishi kwa sababu hakuna njia anaweza kurudisha
kizazi(Unless there is...)
Hata kisayansi I still can't belive kuwa hiyo couple moja isipozaa tutaface extinction!!!

With all the due respect, i agree with you to some points, but saying that humans are not the same as other species and are not guided by law of science/ Nature is completely stereotype thinking and this is not your problem, it has been the selfish nature of human being trying to put himself on top of all species there exists on the planet Earth, that's is why they indulge themselves in environmental manipulation..see ..pollution, and degradation, for his selfish nature of survival,if you will see the evolution tree.. we are not old species as reptiles, still some species have Millions of years of existence on this planet, we have not touched even more than 0.5 Mil years, the matter of fact we respond almost equally in all characteristics of higher mammals and living cells..see reproduction, excretion, growth, Nutrition, death..etc etc.. there is no point in saying that we are so unique than other species..... Religious view point that we are intelligent than other species still hold true in science too, but living in this world without perpetuation wont make this world grow any better and eventually if sufficient members of the community will believe this, human species will go in extinction, and that is not the Gods will of creation.... there is nothing wrong in being re productively deformed, only staying with something just because of circumstances, i don't live in circumstances.......back to this guy in concern, he should decide what he specifically wants in marriage rather than reacting religiously to everything, which in some cases it will not work at all... if you go through the Bible, KJV... see.... my people are perished for the lack of knowledge.....
 
Habari waungwana, naomba kusaidiwa kimawazo nifanye nini katika hili.

Nina mchumba wangu ambaye tumekuwa katika mahusiano kwa takribani miaka miwili na nusu, japo sijawahi kujitambulisha kwao mpango wa utambuzi ulikuwa ni mwezi huu wa November na mipango ilikuwa ishawafikia wazazi.

Hivi majuzi mchumba wangu aliugua gafla tumbo na baada ya vipimo alilazimika kufanyiwa upasuaji uliopelekea kuondoa mfuko wa uzazi ili kunusuru maisha yake.

Ukweli nimechanganyikiwa nini nifanye, hasa ikizingatiwa tunapendana sana.

Lakini nawaza je, ndo hatutapata familia yenye watoto kabisa kama tutaoana? Tafadhali hebu nijengeni kifikra.

kaka shirikisha ndugu zako kwanza
maana kibongobongo huo mtihani kusema za ukweli
haya masuala ya kuadopt sijui nini kwa familia zetu za kiswahi wengi wetu bado sana kuelewa
si tunajua mtoto ni yule aliyepatikana kwa sperms za baba na zikaingia kwa mama
so ni mtihani hapo kwenye ushauri
 
Habari waungwana, naomba kusaidiwa kimawazo nifanye nini katika hili.

Nina mchumba wangu ambaye tumekuwa katika mahusiano kwa takribani miaka miwili na nusu, japo sijawahi kujitambulisha kwao mpango wa utambuzi ulikuwa ni mwezi huu wa November na mipango ilikuwa ishawafikia wazazi.

Hivi majuzi mchumba wangu aliugua gafla tumbo na baada ya vipimo alilazimika kufanyiwa upasuaji uliopelekea kuondoa mfuko wa uzazi ili kunusuru maisha yake.

Ukweli nimechanganyikiwa nini nifanye, hasa ikizingatiwa tunapendana sana.

Lakini nawaza je, ndo hatutapata familia yenye watoto kabisa kama tutaoana? Tafadhali hebu nijengeni kifikra.

Muoe kaka mahaba kama huna plan yakuzaa for lyf ila kama unamalengo ya familia sasa hapo ndio shida itakapo anziaa
 
muoe tu kaka everything is possible through Jesus christ..just do ur part n jesus will do the rest..be blessed.
 
pole sana..

sorry kama kuna mtu ameishataja

but mkitaka kupata mtoto mnaweza kuchukua mbegu zenu na kuzipandikiza kwa mwanamke mwingine atakayejitolea.

tafadhali tembelea
IVF Clinic — Dar IVF & Fertility Clinic - Tanzania

Mmmnnnhhhh
Mwanzo nilitaka kusema hivi hivi lakini nikawaza...je kizazi kikitolewa mbegu zinabaki????

Nadhani wanaotumia hiyo njia ni wale wenye tatizo kwenye mfuko wa uzazi lakini wana kizazi...labda tuombe ufafanuzi wa wataalamu wa afya....

Unless unataka kusema baba achukue mbegu afu apandikize kwa mwanamke mwingine...yani ampe mimba bila sex...

Wako wamama wa hivyo Thailand wanafanya illegally...sababu ya njaa
 
pole kwa matataizo ila kma una mpenda kama unavyodai na yeye ndo pumziko la roho yako muoe tu watoto mta adupt
ila kama lengo la kumpenda ni kwa ili akuzalie watoto usimpotezee muda bora umuache mapema
 
Habari waungwana, naomba kusaidiwa kimawazo nifanye nini katika hili.

Nina mchumba wangu ambaye tumekuwa katika mahusiano kwa takribani miaka miwili na nusu, japo sijawahi kujitambulisha kwao mpango wa utambuzi ulikuwa ni mwezi huu wa November na mipango ilikuwa ishawafikia wazazi.

Hivi majuzi mchumba wangu aliugua gafla tumbo na baada ya vipimo alilazimika kufanyiwa upasuaji uliopelekea kuondoa mfuko wa uzazi ili kunusuru maisha yake.

Ukweli nimechanganyikiwa nini nifanye, hasa ikizingatiwa tunapendana sana.

Lakini nawaza je, ndo hatutapata familia yenye watoto kabisa kama tutaoana? Tafadhali hebu nijengeni kifikra.

Hapa kuna kupeana moyo lakini jambo la msingi busara ni muhimu kwako katika kufanya uamuzi sahihi kwa manufaa yako na familia yenu. Umeeleza wazi kuwa uchumba wenu bado haujawa wazi kwa wewe kutojitambulisha bado ili mlikuwa katika jitihada za kufanya hatua hiyo. Kama mngekuwa mmeshafunga ndoa ni kufungamana kwa maisha tayari lakini maadamu hilo bado mna nafasi ya kufanya maamuzi upya kwa ajili ya kuondoa mkanganyiko katika maisha yenu ya baadaye.

Sijajua wewe mfuasi wa dini gani, ya jadi, kiislamu au kikristo? Hata hivyo matarajio na matamanio katika familia za kiafrika ni kupata baraka ya Mungu kwamba zaeni mkaongezeke na kuijaza dunia. Moja ya matarajio makubwa katika familia ni kuzaa watoto na ndicho kinachotazamiwa na familia toka pande zote. Sitarajii kwa imani za kiafrika kuoana ni kwa ajili ya kuishi mume na mke tu.

Pamoja na kwamba Mungu ni mweza yote, lakini ametuumba na vitendea kazi vya miili na utashi wetu kushiriki kazi ya uumbaji, na pale maumbile ya miili yetu yanapokosa viungo vya uzazi dhahiri tusimdai mno Mungu kwamba atafanya yote na tusilazimishe miujiza ya Mungu ifanye hivyo ingawa katika misahafu imetoke kufanyika katika historia ya wokovu wetu.

Hili ni jambo la kukaa pamoja wewe na mchumba wako kulizungumza na kuelezana hali halisi, kama mnapenda kuwa na mtoto kwa njia ya kurithi na mkakubaliana kwa hilo sawa, lakini kama mnataka mtoto wa kutoka maungoni mwenu hili halitawezekana. Hayo ni masikilizano yenu wawili kwa uwazi na kufanya uamuzi wa busara wa pamoja kwa manufaa kwa familia za pande zote mbili.

Kushirikisha wazee kutoleta uamuzi wa busara zaidi. Wao wana mengi ya kukushauri kwa busara na uzoefu wa maisha ya ndoa, bora umejua hilo mapema kabla hamjaoana.
 
Una uhakika wewe unao uwezo wa kuzalisha?
 
Mtihani huo...maana malengo watu wanakuwa nayo mazuri tu mwanzoni...wakikaa miaka say 10 unashangaa mtu kabadili mawazo...labda waanze kabisa na kutafuta watoto yatima wa kulea...lakini wakisema wakae peke yao, lazima watachemsha...

Na kiafrika ndugu...ndugu wanaharibu sana yani....ukute familia ya mwanaume wawe waelewa...lakini kama ni wale wale...nao wanaweza kuwa chanzo cha kukuza tatizo siku za usoni...

Kweli ni mtihani, na inahitaji nguvu ya ziada kuushinda. Ukweli mchungu ni chaguo zuri kuliko uongo mtamu, nina wifi yangu hana amani na kutwa kujihisi kwa kutopata mtoto na kaka yangu naye anateseka kwani anakuwa extra mwqngalifu kwa kila anachokiongea ili asimkwaze mwenzake; yaani nyumba inakuwa so cold kwa mipaka. Pamoja na uangalifu huo bro alichepuka na kupata mtoto; sasa mtoto anafichwa hadi unamuonea huruma
 
Kwa wakatoliki ikiwa mmoja anajijua hana uwezo wa kuzaa na akamficha mwenzake ndoa yao yaweza kutenguliwa, maana définition ya ndoa ya kikatoliki watoto wanaingia. Hii ni kuonesha jinsi gani swala la watoto ni zito maana sio kila siku ndoa za wakatoliki zinatenguliwa.
Mleta mada ni heri kumuumiza leo tu kwa kuvunja uchumba kuliko kumuumiza maisha yake yote kwa udanganyifu. Mungu atamjalia atapata passion ya kitu kingine iwe kazi au biashara. Sio kila mwanamke kaandikiwa ndoa.
 
Kweli ni mtihani, na inahitaji nguvu ya ziada kuushinda. Ukweli mchungu ni chaguo zuri kuliko uongo mtamu, nina wifi yangu hana amani na kutwa kujihisi kwa kutopata mtoto na kaka yangu naye anateseka kwani anakuwa extra mwqngalifu kwa kila anachokiongea ili asimkwaze mwenzake; yaani nyumba inakuwa so cold kwa mipaka. Pamoja na uangalifu huo bro alichepuka na kupata mtoto; sasa mtoto anafichwa hadi unamuonea huruma

Huo mtihani ni pande zote mbili ingawa hapa watu wengi wanaangalia mwanaume...
Mke pia hatoweza kujiamini hata mumewe amwakikishie kiasi gani kuwa its okay..

Ningekuwa mimi huyo dada nisingekubali kuolewa...natafuta yatima nalea mwenyewe...sitaki kumizwa wala kuumiza wengine...sipendi kabisa kuhurumiwa hurumiwa au kuishi na wasi wasi...

Nilimuona Happiness Magese kichwa sana aliposema hana mpango wa kuolewa kwa kuwa anajua hakuna mwanaume anayekubali mwanamke asozaa...na hataki kukwaza watu...she is real smart...

Ila najua kuna baadhi ya wanaume ambao si waafrika hawataki kusikia kitu kinachoitwa mtoto...kwa hiyo chance ipo kupata wa hivyo kama yuko majuu...
 
Habari waungwana, naomba kusaidiwa kimawazo nifanye nini katika hili.

Nina mchumba wangu ambaye tumekuwa katika mahusiano kwa takribani miaka miwili na nusu, japo sijawahi kujitambulisha kwao mpango wa utambuzi ulikuwa ni mwezi huu wa November na mipango ilikuwa ishawafikia wazazi.

Hivi majuzi mchumba wangu aliugua gafla tumbo na baada ya vipimo alilazimika kufanyiwa upasuaji uliopelekea kuondoa mfuko wa uzazi ili kunusuru maisha yake.

Ukweli nimechanganyikiwa nini nifanye, hasa ikizingatiwa tunapendana sana.

Lakini nawaza je, ndo hatutapata familia yenye watoto kabisa kama tutaoana? Tafadhali hebu nijengeni kifikra.

tafuta mwingine bana.
 
mi ushauri wangu mwingine km kweli unampenda bora umuache kaoe kwingine kwa sababu ukimuoa sidhani km utakubali ukae bila watoto utaanza kupiga show za nje ukipata mtoto baas unaweza jisahau ukahamia kwa mwenye mtoto kabisa huyu mdada ikala kwake
we muache for good kaoe kwingine
usije ukamuumiza bure
 
Remote watu wana imani humu jamvini balaa...! Engine imeng'olewa watu wanasema kwa imani gari itapanda mlima kitonga? Aaaah!

Hahaha hy miujiza haipo tena ilikuwa enz za mitume
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom