GE2025 Mchinjita: Raia kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali iseme ni Wasiojulikana, hiyo ni Serikali au Takataka?

GE2025 Mchinjita: Raia kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali iseme ni Wasiojulikana, hiyo ni Serikali au Takataka?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Unaweza kukata tamaa kisa maisha yako yamekua magumu basi

..Ni lugha ya mtu ambaye anaamini amedhulumiwa, ameonewa, hajatendewa haki.

..tusiwabeze wapinzani, bali tuangazie nini cha kufanya ili mitizamo na lugha zao ktk siasa iwe chanya, badala ya hasi.

..Tanzania ni yetu Sote. Kila mmoja wetu, bila kujali itikadi za vyama, anastahili kuishi kwa amani, na furaha.
 
Kama wanafikiri kuteka na kupoteza watu ndio kutqfanya watu wawe waoga kusema, wajue wanajidanganyq.
 
Lugha ngumu haijawahi lupata mafanikio popote iwe Africa au nje ya africa

Tusijitoe fahamu
Endelea kujidanganya !

Hamtaki Lugha ngumu mwachieni Lisu,kwanini mmendelea kumuweka kizuizini?

Ili tuone kweli kama Lugha ngumu hazijawahi kufanikiwa!
 
..Ni lugha ya mtu ambaye anaamini amedhulumiwa, ameonewa, hajatendewa haki.

..tusiwabeze wapinzani, bali tuangazie nini cha kufanya ili mitizamo na lugha zao ktk siasa iwe chanya, badala ya hasi.

..Tanzania ni yetu Sote. Kila mmoja wetu anastahili kuishi kwa amani, na furaha.
Huko sahihi sana ndugu, huo nimetoa mfano kua wengine wanaweza kukata tamaa kwasababu ya maisha basi wakafanya kua liwalo liwe.
 
Kuua au kuteka siyo ustaarabu lakini it doesn’t make you a better person Kwa kutumia lugha zisizofaa
Ukitaka pawepo na "ustaarabu", na kuwa na "better persons"; hakikisha pasiwepo na hayo matendo maovu ya kuua watu; kwa vile tu wewe unafikiri siyo "wastaarabu".
Huwezi ku-'enforce/impose' ustaarabu kwa kuua au kuteka watu.
Ni yale yale mnayyo danganyia watu, kuweo kwa "AMANI", wakati hamtaki watu wawe na HAKI zao.
 
Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Bara, Isihaka Mchinjita amesema, "Unapofika mahala una Serikali ambayo raia wake wanaweza kwenda kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali inasema walioua ni watu wasiojulikana — hiyo ni Serikali au takataka?"

"Haijawahi kutokea duniani kote, kukawa na takataka iliyopata hadhi kuitwa Serikali kisha takataka hiyo ikatengeneza sheria safi za kuleta Serikali isiyotakataka."

Hii kweli haina ubishi
 
Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Bara, Isihaka Mchinjita amesema, "Unapofika mahala una Serikali ambayo raia wake wanaweza kwenda kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali inasema walioua ni watu wasiojulikana — hiyo ni Serikali au takataka?"

"Haijawahi kutokea duniani kote, kukawa na takataka iliyopata hadhi kuitwa Serikali kisha takataka hiyo ikatengeneza sheria safi za kuleta Serikali isiyotakataka."

Ni mpangonwaliopanga ili na wao wakamatwe isionekane Chadema inaonewa.
 
Kwani huwezi kosoa bila kudhalilisha utu na mamlaka ya Viongozi?

Kila mtu ana hisia
Kwa maana hiyo, hao viongozi wao kusemwa vibaya, hukumu yake ni kuuawa/kupotezwa?
Mungu mwenyewe anasemwa vibaya mara ngapi; hawa viongozi wenu ni zaidi ya Mungu?

Lakini niulize, hivi hizi ni tamaduni za wapi, maana naona wote mnaotetea haya maovu ni kama watu wa mlengo fulani? Lugha yenu ni moja, ni kama mmekariri toka mahala kuhusu maswala ya namna hii?
 
Kwa maana hiyo, hao viongozi wao kusemwa vibaya, hukumu yake ni kuuawa/kupotezwa?
Mungu mwenyewe anasemwa vibaya mara ngapi; hawa viongozi wenu ni zaidi ya Mungu?

Lakini niulize, hivi hizi ni tamaduni za wapi, maana naona wote mnaotetea haya maovu ni kama watu wa mlengo fulani? Lugha yenu ni moja, ni kama mmekariri toka mahala kuhusu maswala ya namna hii?
Kutukana mtu au Kiongozi sio kumkosoa au kumsema bibaya.,huko ni kufanya udhalilishaji.
 
Lugha yake sio ya kistaarabu
Ila kuua watu na kusema ni vijidrama na kifo ni kifo ndio ustaarabu?

Sasa nenda kwa mzee Kibao uwaambie kifo ni kifo kama alivyosema mama Abdul halafu uone kitakachotokea.

Au nenda kwao Soka uwaambie mwanao alijiteka kama polisi wanavyodai uone kitakachotokea.
 
Kutukana mtu au Kiongozi sio kumkosoa au kumsema bibaya.,huko ni kufanya udhalilishaji.
Bado hiyo haiwezi kuwa hukumu yake ni kuuliwa.
Na huku "kutukana", ni nini hasa. Kuna kipimo maalum kinachoonyesha ukisema maneno fulani fulani, huko ni kutukana?
Ni nani anayepima na kuamua kuwa maneno yaliyotumika ni ya kutukana na kudhalilisha. Kuna mahakama inayo amua haya?
 
Back
Top Bottom