GE2025 Mchinjita: Raia kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali iseme ni Wasiojulikana, hiyo ni Serikali au Takataka?

GE2025 Mchinjita: Raia kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali iseme ni Wasiojulikana, hiyo ni Serikali au Takataka?

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025
Kasema ukweli kabisa.Watanzania tusahau takataka kutuletea mazuri Bali tutarajie kuletewa takataka tu
 
Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Bara, Isihaka Mchinjita amesema, "Unapofika mahala una Serikali ambayo raia wake wanaweza kwenda kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali inasema walioua ni watu wasiojulikana — hiyo ni Serikali au takataka?"

"Haijawahi kutokea duniani kote, kukawa na takataka iliyopata hadhi kuitwa Serikali kisha takataka hiyo ikatengeneza sheria safi za kuleta Serikali isiyotakataka."

Yes ni kweli ni TAKATAKA, na wanaoongoza hiyo serikali wamejaa matope kichwani. Hivi serikali kutumia TISS inamchukua mwananchi asiye na hatia, wanamtesa, wanamtoboa macho na kumwagia Acid usoni na kumtupa msituni......Hiyo ndiyo mnasema ni serikali? Ninyi mnaotetea serikali hamjawahi kupoteza ndugu, wazazi au wapendwa wenu kwa kukamatwa na kuua na serikali. Waliona shida gani kumpeleka mahakamani kama ana kosa. Acheni ujinga ninyi.
 
..watawala walitakiwa wajiulize kwanini vyama vya upinzani vinatumia lugha ngumu.

..kwa maoni yangu hizo lugha zinaelezea mateso na dhuluma wanayopitia wapinzani.

..Mjumbe[ally kibao] wa Kamati Kuu ya chama kuuwawa na maiti yake kutobolewa macho haliwezi kuwa jambo dogo kwa chama cha siasa.

..dhuluma hiyo, au zozote zinazofanana na hiyo, haiwezi kuzungumziwa kwa lugha lainilaini, au za bashasha.

..Watawala wajifunze, na wajisahihishe, badala ya kuwapingia waliodhulumiwa namna ya kulia na kulalamika.
Ht wajinyee jukwaani hao wapumbavu hawawezi kupata ht mbunge moja, sasa huyo si kavimbiwa uvundo?
 
Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Bara, Isihaka Mchinjita amesema, "Unapofika mahala una Serikali ambayo raia wake wanaweza kwenda kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali inasema walioua ni watu wasiojulikana — hiyo ni Serikali au takataka?"

"Haijawahi kutokea duniani kote, kukawa na takataka iliyopata hadhi kuitwa Serikali kisha takataka hiyo ikatengeneza sheria safi za kuleta Serikali isiyotakataka."

Hee duu!! Kusha anza kuchangamka.... Amazing!?
 
Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Bara, Isihaka Mchinjita amesema, "Unapofika mahala una Serikali ambayo raia wake wanaweza kwenda kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali inasema walioua ni watu wasiojulikana — hiyo ni Serikali au takataka?"

"Haijawahi kutokea duniani kote, kukawa na takataka iliyopata hadhi kuitwa Serikali kisha takataka hiyo ikatengeneza sheria safi za kuleta Serikali isiyotakataka."

Serikali takataka ha ha ha ha ha
 
Makamu Mwenyekiti wa ACT Wazalendo Bara, Isihaka Mchinjita amesema, "Unapofika mahala una Serikali ambayo raia wake wanaweza kwenda kuokotwa kwenye mabasi mchana kisha wakafa, halafu Serikali inasema walioua ni watu wasiojulikana — hiyo ni Serikali au takataka?"

"Haijawahi kutokea duniani kote, kukawa na takataka iliyopata hadhi kuitwa Serikali kisha takataka hiyo ikatengeneza sheria safi za kuleta Serikali isiyotakataka."

Sasa hizi Kauli si ndio Huwa zinaleta ukakasi au?
 
Lugha yake sio ya kistaarabu
Lakini wewe unafikiri watu wanaootea/kuuawa wanafanyiwa hivyo "kistaarabu"!

Lakini niungane nawe hapa, kuuliza kama kweli huyu mtu karuhusiwa na chama chake kuyasema haya aliyosema kuhusu "serikali takataka" iliyoPo madarakani.
 
Lakini wewe unafikiri watu wanaootea/kuuawa wanafanyiwa hivyo "kistaarabu"!

Lakini niungane nawe hapa, kuuliza kama kweli huyu mtu karuhusiwa na chama chake kuyasema haya aliyosema kuhusu "serikali takataka" iliyoPo madarakani.
Kuua au kuteka siyo ustaarabu lakini it doesn’t make you a better person Kwa kutumia lugha zisizofaa
 
Bila lugha ngumu ni ngumu sana kuondoa takataka kwenye Vichwa vya Muafrika!
Lugha ngumu haijawahi lupata mafanikio popote iwe Africa au nje ya africa

Tusijitoe fahamu
 
Back
Top Bottom