Mchina aliyepata "A" tisa NECTA

Mchina aliyepata "A" tisa NECTA

watafiti walikuja na hitimisho kwamba Wamarekani wenye asili ya kwetu Afrika wana IQ ndogo kulinganisha na Wamarekani wenye asili ya Ulaya

Kikwete aliwahi kusema kuwa ukisoma au ukisikia kitu Usikipokee kama kilivyo changanya pia na akili zako.

Hivi unaamini wazungu wana IQ kubwa kuliko waswahili? Mtu mwenye IQ kubwa anaweza kaa bungeni na kupitisha sheria ya watu kuoana wa jinsia moja na kuipigia debe dunia nzima?

Wazungu wamekubaliana kuwa kuparamiana watu wa jinsia moja ni kitu sahihi.IQ ZAO ZIKO JUU?
 
Kwa mtazamo wangu umeaminishwa kuwa ni hivyo na wewe ukaamini kwamba IQ yako ni ndogo.Hakuna kitu kama hicho. unawaelezea vipi watanzania wanaokwenda kusoma nchi ambazo mfumo wao wa elimu unaendeshwa kwa lugha za kihispania,kichina,kirusi,kifaransa,kireno,kidachi,kibelgiji,kijerumani nk na bado wakachanganywa na wazawa na wakafaulu mitihani yote na kuhitimu ktk vyuo vikuu vyao na hata kuwa wanafunzi bora.Na unapozungumzia wamarekani weusi si swala la IQ bali ni swala la mazingira ,umasikini,kuathirika kisaikolojia na fursa duni vilivyokidhiri ktk jamii husika ndiyo vinavyochangia kuwa na uelewa mdogo.


Nisome vizuri labda utanielewa, najinukuu ukusadia ,,najua kwamba data hazitoshi kuweza kuhitimisha chochote lkn labda kuna ukweli ndani yake kwamba watu wa Asia wana IQ kubwa klk wote Duniani kwa maana sijawahi kusikia Mwafrika diaspora akiongoza kwa kwenye mitihani huko aliko kama yuko naomba nisahihishwe!
 
Media na waandishi wa habari naona gumzo limekua mchina kushika nafasi ya pili na kupata B ya kiswahili, mbona mshindi wa kwanza hawamzungumzii au kwa kua yeye si mchina!?

Ulimbukeni huu jaman,mchina anapewa airtime sana kuliko mtanzania
 
100% nakuunga mkono, pia hizo hizo IQ za weusi walio wengi waliandama london eti kupinga yaliyotokea zanzibar na wengine wanadai eti wanaenda fungua kesi ulaya kwa kunyimwa haki zao za uchaguzi wa haki, hizi IQ wazungu wanaendelea kupima na kujiridhisha zaidi kuwa tafiti zao ziko sahihi, tena inawezekana walipendelea maana hizi IQ ziko sub zero kabisa!
Tatizo unalodai kuwepo kwako unaenda kwa watu kutaka wakusaidie kulitatua ilhari wee ni mtu mzima mwenye 'akili' timamu, Hovyo kabisa! Unazira kisha unadai unanyimwa haki, hizi ni akili kweli?
Mleta mada umeumganisha vizuri point zako kuanzia kwa mchina mpaka kwenye uhalisia.

Ukijaribu kuangalia mleta uzi na wewe mmeungana katika hoja, sina shida na hilo ila sijui mnachoshangaa ni nini wakati mnasema waafrika weusi wana IQ ndogo ikiwepo na Magufuli. Sasa kama hilo ni kweli huoni hata huyo Magufuli akipingwa ni sawa kwani ni wazo la mtu mwenye IQ ndogo kutokana na rangi yake? Jamani mnajaribu kumsifia Magufuli mpaka mmefikia mahali mnaweka kashfa ili hoja zenu zikubalike za kumsifia Magufuli? Huwa mnashangaza sana, mnalazimisha kusifia tu, lakini akiambiwa ukweli kwamba ni kipi kikubwa alichofanya ambacho mwananchi anaweza kusema wangalau sasa anaona tofauti kwenye maisha yake, mnaishia kusema bado ni mapema!! Sasa kama ni mapema sana kwanini mumsifie kupita kiasi wakati bado ni mapema?
 
Hivi kwani watanzania wangapi kila mwaka wanapata A au B za lugha ngeni kama Kiingereza, Kifaransa zinazofundishwa mashuleni hadi leo iwe nongwa hivi mchina kupata B tu ya kiswahili?


Kusema ni Waafrika wangapi huongoza ni rahisi sana kila mtu anaweza kusema na ndiyo maana nikatoa changamoto kama yupo Mwafrika Diaspora aliongoza huko aliko nchi nzima mtaje, ni rahisi kivivyo tu!
 
Nisome vizuri labda utanielewa, najinukuu ukusadia ,,najua kwamba data hazitoshi kuweza kuhitimisha chochote lkn labda kuna ukweli ndani yake kwamba watu wa Asia wana IQ kubwa klk wote Duniani kwa maana sijawahi kusikia Mwafrika diaspora akiongoza kwa kwenye mitihani huko aliko kama yuko naomba nisahihishwe!

Wakati mwingine huwa unakosa hoja mpaka unageuka kituko. Hivi sisi watanzania na ugumu wote huu wa maisha tuache kufanya na kufuatilia mambo ya msingi kubadili maisha yetu, tukae tunafuatilia diaspora gani ameongoza mtihani huko majuu? Halafu ukishajua ndio utakuwa umesonga mbele kimaendeleo. Mbona kama mnaleta hoja za kitoto halafu mnataka muishie kusifiwa kwa utoto wa aina hii?
 
Ukijaribu kuangalia mleta uzi na wewe mmeungana katika hoja, sina shida na hilo ila sijui mnachoshangaa ni nini wakati mnasema waafrika weusi wana IQ ndogo ikiwepo na Magufuli. Sasa kama hilo ni kweli huoni hata huyo Magufuli akipingwa ni sawa kwani ni wazo la mtu mwenye IQ ndogo kutokana na rangi yake? Jamani mnajaribu kumsifia Magufuli mpaka mmefikia mahali mnaweka kashfa ili hoja zenu zikubalike za kumsifia Magufuli? Huwa mnashangaza sana, mnalazimisha kusifia tu, lakini akiambiwa ukweli kwamba ni kipi kikubwa alichofanya ambacho mwananchi anaweza kusema wangalau sasa anaona tofauti kwenye maisha yake, mnaishia kusema bado ni mapema!! Sasa kama ni mapema sana kwanini mumsifie kupita kiasi wakati bado ni mapema?


Na ndiyo hapo swala la IQ linapokuja sasa, kwa jamii nyingine mtu hawezi kumuhukumu Raisi aliyok madarakani kwa muda wa miezi 3 tu kwamba hajaboresha maisha, hakuna jinsi ambavyo unaweza kulielezea jambo kama hili isipokuwa uwezo tu mdogo wa kufikiri siyo tusi ni ukweli TU!
 
Sijaelewa hapo kiini cha thread yako ni ipi! Ni IQ au Sukari au Mchina kuongoza kiswahili!? Au ni tangazo la Magufuli kustopisha sukari kutoka nje!?
 
hii mada yako inahusu siasa au huo utafiti?
weusi kwa wastani wana uwezo mdogo wa kufikiri ila mambo ya kumpinga/kumuunga mkono magufuli hapa nadhani sio relevant
maana anayepinga hili suala la kuzuia sukari kutolewa nje yupo sahihi kwa kua itapunguzia ushindani kwa viwanda vyetu na na efficiency pia itapungua
magufuli nae yupo sahihi pia kupiga marufuku kutasaidia kuvibeba viwanda vya ndani
so anayepinga na anayeunga mkono wote wapo sahihi kwa namna moja au nyingine na sio kusema wana iq ndogo
 
Kama anaishi Tanzania sio mchina no mtanzania mwenye asili ya china
 
Tunanunua magari ya mabilioni ya shilingi kwa ajili ya wabunge na mawaziri, wakati wanafunzi wanakaa chini, wanaanza kupata matatizo ya mgongo kabla hata hawajafikisha umri wa kubalehe!!. Tuliua mashirika ya umaa mengi sana halafu unamsikia mwanasiasa akilalamikia ukosefu wa ajira kwa wasomi vijana!!. Ukweli unaposemwa wenye hasira za haraka hukasirika lakini wenye kutafakari mambo huwa wanamshukuru Mungu kwa kujua waanzie wapi katika utatuzi wa matatizo mengi.

IQ zetu zina mushkeli, mtu anamlaumu waziri wa afya kwa sababu ya uchafu ulioko nje ya nyumba yake, lakini jioni anakwenda bar na kunywa bia zaidi ya tatu na anawapa ofa marafiki zake, wakati ile fedha aliyoiacha pale bar angeweza kununua vifaa vyote muhimu vya usafi.
 
Kwa wale ambao labda hawafahamu Bell Curve ni nini, hii ilipendekezwa na Wanasayansi wa Kimarekani waliokuwa wanafanya utafiti wa IQ (uwezo wa kufikiri na kutatua matatizo) kwa watu wa asili tofauti tofauti hasa nchini Marekani ambapo kuna watu wa jamii ya kila aina yaani Wazungu (Ulaya), Weusi(Afrika Kusini mwa Sahara), Waasia (Wachina, Korea, Japan &Co.) , lengo lao lilikuwa ni kutaka kujaribu kuelezea hali ya maisha ya jamii mbalimbali yaani kwa nini jamii fulani ni masikini klk jamii nyingine!

Hawa watafiti walikuja na hitimisho kwamba Wamarekani wenye asili ya kwetu Afrika wana IQ ndogo kulinganisha na Wamarekani wenye asili ya Asia na Ulaya na hii inaelezea kwa nini Wamrekani weusi wako kwenye ngazi ya chini ya Kimaendeleo ukilinganisha na jamii nyingine!
Walienda mbali zaidi na kufanya test IQ Dunia nzima na sisi huku kwetu tulikuwa wa chini kabisa wa kwanza wakiwa watu wa Asia (Japani, Uchina, Korea &Co.) wakifuaitwa na Wazungu wa Ulaya!

Hawa jamaa walipingwa sana kwamba ni wabaguzi, Je hili la Mchina kuwa wa Pili kwenye mtihani wa kidato cha nne TanZania nzima inasema nini?
Amepata B ya Kiswahili, lugha ambayo siyo yake na wala sia ajabu haiongei nyumbani amewapita watoto wengi sana wa Kiswahili,
najua kwamba data hazitoshi kuweza kuhitimisha chochote lkn labda kuna ukweli ndani yake kwamba watu wa Asia wana IQ kubwa klk wote Duniani kwa maana sijawahi kusikia Mwafrika diaspora akiongoza kwa kwenye mitihani huko aliko kama yuko naomba nisahihishwe!


Nikiangali kwa mfano kwa hali ya kawaida Raisi aliyeonyesha uzalendo kama Magufuli alipaswa kuungwa mkono sana lkn bado kuna watu wanaponda kilam jitihada anazofanya badal ya kuungana naye na kumsaidia kutatua mataizo, Je hii haipo kwenye IQ? Yaani uwezo wetu wa kufikiri na kujua ni mihimu na nini siyo muhimu!

Nitatoa mfano Raisi amepiga marufuku uagizwaji wa sukari nje mpaka pale yeye atakapotoa Kibali kwa kujidhihirisha kwamba kweli kuna sababu ya kufanya hivyo kuna watu wamejaza seva ya JF wanampinga Raisi kwamba amekosea, wkt Raisi ameseam lengo ni kukuza viwanda vya ndani ili viweze kuongeza Uzalishaji na kuanjiri Watz wengi zaidi, lkn watu wanapinga, sasa kama siyo tatizo IQ ndogo nini?

Tayari wewe mwenyewe umeshaprove kuwa IQ ya weusi ni ndogo, andiko lako linachanganya mambo, issue ya sukari unaileta vipi kwenye issue ya IQ?
 
Na ndiyo hapo swala la IQ linapokuja sasa, kwa jamii nyingine mtu hawezi kumuhukumu Raisi aliyok madarakani kwa muda wa miezi 3 tu kwamba hajaboresha maisha, hakuna jinsi ambavyo unaweza kulielezea jambo kama hili isipokuwa uwezo tu mdogo wa kufikiri siyo tusi ni ukweli TU!

Ila kwa IQ hiyo hiyo ndogo unaweza kuanzisha hata post 10 kwa siku kusifia kupitia kiasi alichofanya kwa hiyo miezi 3!!! Aibu nyingine mpaka basi.
 
hii mada yako inahusu siasa au huo utafiti?
weusi kwa wastani wana uwezo mdogo wa kufikiri ila mambo ya kumpinga/kumuunga mkono magufuli hapa nadhani sio relevant
maana anayepinga hili suala la kuzuia sukari kutolewa nje yupo sahihi kwa kua itapunguzia ushindani kwa viwanda vyetu na na efficiency pia itapungua
magufuli nae yupo sahihi pia kupiga marufuku kutasaidia kuvibeba viwanda vya ndani
so anayepinga na anayeunga mkono wote wapo sahihi kwa namna moja au nyingine na sio kusema wana iq ndogo


Ingawaje nisingependa kuigeuza hii mada kuwa ya sukari huwo nimetoa kama mfano tu, yaani kwenye nchi za Jamii nyingine kama Asia, Ulaya, Marekani n.k sababu aliyoitoa Raisi haikupaswa kuwa hoja hata ya kujadiliwa, kwa maana Raisi ameeleza sababu kuamua hivyo nayo ni kukuza kwa kuviwezesha viwanda vya ndani na kila mtu mwenye IQ ya wastani Dunia hii anaelewa kwamba nchi zote kuanzia Marekani, Ulaya, Japani hata Uchina hujenga sera za kulinda viwanda vyake vya ndani kwanza hasa pale vinapokuwa kwenye ngazi ya chini ya Kimaendeleo!

Mpaka mwaka 1945 Marekani walikuwa wanafanya protectionism yaani walikuwa hawaruhusu ushindani ktk nje na wamekuja kuruhusu ushindani baada ya Vita Kuu ya Pili kuisha baada ya kuona sasa wamekosa mshindani yaani walivyoona kwamba sasa viwanda vyao vina competetive edge ndiyo wakaruhusu ushindani ktk nje, hata Uchina leo hauwezi kuwekeza Uchina kwa 100% ni lazima uingie ubia na Kampuni ya Uchina na hili linaeleweka Dunia nzima isipokuwa hapa kwetu TU na anachotaka kufanya Raisi Magufuli hakina tofauti na kinachofanyika Dunia nzima ila tofauti ni kwamba Dunia nje na kwetu kinaeleweka lkn hapa kinapingwa!
 
Back
Top Bottom