Kesi ya Mmasai anayeshutumiwa kumuua Mchina inavutia kimedani. Nipo interested nayo kuona kile jeshi letu litafanikiwa na kwa muda gani

Kesi ya Mmasai anayeshutumiwa kumuua Mchina inavutia kimedani. Nipo interested nayo kuona kile jeshi letu litafanikiwa na kwa muda gani

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
37,311
Reaction score
86,733
Habari za jumapili!

1. Wiki kadhaa zilizoisha taarifa za kuuawa mchina zilizagaa mitandaoni.

2. Mshukiwa wa mauaji hayo akiwa ni mtu mmoja ambaye jina lake halikutajwa isipokuwa kabila lake la maasai.

Hii ni kusema taarifa inaripotiwa mchina auawa na mmasai.

3. Wamasai ni moja ya Makabila makubwa, yenye nguvu hasa ya kimila na kidesturi, yenye mifumo mizuri ya kifamilia, KAZI, ulinzi,

4. Wamasai ni moja ya kabila ambalo wanaakili na wanaongozwa na kanuni ya Low key au low profile.

5. Mbinu kubwa waitumiayo wamasai katika Kanuni ya Low key ni kujifanya wajinga, wasioelewa mambo, washamba lakini kimsingi ni watu wanaoelewa mambo Sana kuliko watu wengi.

6. Umasai ni Kabila lakini hapohapo Umasai ni Dini. Watu wengi hasa waswahili hawajui hili. Umasai ni kabila lakini pia ni Dini kwa Wamasai.

7. Wamasai popote walipo ni ndugu. Tofauti na makabila mengine.

Wamasai huunganishwa na umasai wao kisha huonana ndugu wa damu moja kikoo.

8. Wamasai wengi hasa wa mjini hawana anuani rasmi. Unaweza kuwaona wakienda na kurudi huko mabarabarani lakini usijue wanapoishi.

9. Hata humu ndani, wapangaji unaweza kukuta tangu kuzaliwa hujawahi kupanga nyumba moja na wamasai.

10. Wamasai wengi hupanga nyumba moja. Wao kwa wao. Kwa hapa Dsm utakuwata hasa maeneo ya msasani kule kuanzia msasani macho. Huko utawakuta wamepanga nyumba na wanaishi huko.

11. Wamasai waliopo mjini nazungumzia Dar es salaam, wala sio Arusha maana huko ni kwao. Wengi hao hasa vijana taarifa zao hazijasajiliwa katika mifumo rasmi.

Sio ajabu ukamkuta hana NIDA wala Vote Id.

12. Wamasai wengi wanaumoja, wanashirikiana Sana. Wana ule moyo WA kuonana ni ndugu.

13. Wamasai wengi waliokuzwa umasaini wanafundishwa elimu za ulinzi, usalama na mambo ya kimedani.

Sio ajabu hata mbinu za kujifanya majinga yasiyoelewa kitu ikawa sehemu ya mkakati wao wenye kuzaa matunda.

14. Kwenye tukio la Mauaji kama hilo lililotokea huku mshukiwa mkuu akiwa huyo mmasai. Angekuwa mtu wa jamii nyingine ndani ya Siku Saba angekuwa ameshatiwa nguvuni. Lakini kwa masai tunaenda wiki ya pili tukiitafuta ya tatu.

15. Masai wengi hawana picha mitandaoni. Sio ajabu picha itakayotumika kumsaka ikawa ni Ile ambayo ni passport size aliyoombea kazi. Na kama aliomba zamani inamaana kwa sasa inaweza kuathiri ufuatiliaji wake.

16. Fikiria wewe ndiye mpelelezi wa kesi hiyo.

Mshukiwa amekimbia, mshukiwa hatumii simu,

Mshukiwa Hana picha mtandaoni,

Umepewa picha ya passport size labda ya zamani,

Wazazi wa mshukiwa ni wamasai ambao wanaule umoja na undugu, Rafiki zake nao ni wamasai na wanaule umoja.

17. Wewe ni mpelelezi, wiki mbili zimeisha sasa. Hapo bado kuna wamasai wa Kenya. Kwamba kama atakimbilia Kenya bila Mawasiliano ya simu upelelezi wako unazidi kuwa mgumu.

18. Binafsi hii kesi inanivutia Sana. Kwani nataka kuona umahiri wa jeshi letu kimedani katika mazingira kama haya.

Karibuni kwa mjadala

Taikonmaster

Kwa sasa Dar es salaam
 
Huyo Mmasai watamkamata kama ataendelea kutumia simu, na pia kuwasiliana na watu wake wa karibu. Ila kama atagundua huu mtego, basi uwezekano wa kutiwa nguvuni haupo.

Kwanza majina yao yenyewe tu ni utata mtupu! Ukija kwenye sura sasa, karibia wote wanafana! Hawana anuani ya makazi! Wanaishi maisha ya kuhamahama (nomadic)!!

Aisee kama wewe ndiyo mpelelezi lazima kichwa kiume!
 
Huyo Mmasai watamkamata kama ataendelea kutumia simu, na pia kuwasiliana na watu wake wa karibu. Ila kama atagundua huu mtego, basi uwezekano wa kutiwa nguvuni haupo.

Kwanza majina yao yenyewe tu ni utata mtupu! Ukija kwenye sura sasa, karibia wote wanafana! Hawana anuani ya makazi! Wanaishi maisha ya kuhamahama (nomadic)!!

Aisee kama wewe ndiyo mpelelezi lazima kichwa kiume!

Kweli Kabisa.
Na mimi nilikuwa nawaza kama wewe hapa.

Kingine kama aliondoka na milioni 10 zitamsaidia pakubwa ku escape. Kwa sababu kibongobongo 10M ni pesa nyingi Sana.
Fikiria mwalimu wa Degree kwa mwaka anakunja 9M
 
Unazungumzia nyara ya taifa

Ila sema nimewahi kukutana na masai wasafi

Ila Kuna wapumbavu wa kimasai wakuitwanga wa Arusha hii namba chafu sana
 
Masai waone hivyohivyo.
Wanajifanyaga hamnazo, lakini ni watu smart sana
Hawa wanajitoa Ufahamu hiyo ni kweli

Wamejaa masaki sanaa mpaka msasani na wanaaminika

Huyo aliyeua kama kweli ni masai lazima apatikane najua hiyo

Kama hapatikani huyo sio masai

Masai analinda geti analipwa 400k na anang'ombe kwao Mia mbili na hawazi

Kukuta masai anaua sio rahisi hizo ni takataka za arusha
 
Kitu kimoja tu muhimu nchi hii hakuna intelligence ya maana zaidi ya uchawa kuna mengi sana wanapuyanga mno ila ngoja tunyamaze

Ukiwa nje ya mifumo intelligence sio rahisi kukunasa.
Ndio maana wahalifu bobevu Jambo la Kwanza wakishafanya tukio wanajitoa kwenye mifumo.

1. Mfumo wa ndoa.
Ukiwa mhalifu ukishakuwa na familia uwezekano wa kukamatwa upo kwa asilimia kadhaa.

2. Mfumo wa Social media na teknolojia
Kama mitandao ya simu, mitandao ya kijamii.

3. Mifumo ya Kidini.
Sijui muislam, sijui mkristo na unahuzuria Sana huko.

4. Mifumo ya siasa na ajira
Kama kuwa na vote id sijui NIDA

5. Mifumo ya elimu
Sijui ulisoma, msingi, secondary mpaka chip.
Hiyo mifumo inakutengenezea connection ambayo connection hiyohiyo ndio inatumika kukukamata.
Wahalifu wengi WA viwango vya juu. Kama walikuwa wakisoma wanakuwa hawana marafiki ni watu wakujitenga na kukaa pekeake.
Watu wa hivi ni ngumu kuwanasa.

Na mifumo mingine
Wengi wahalifu hawatumii mifumo hiyo
 
Apa bongo akuna medan wala taaluma za upelelezi zaidi utasomwa upepo wa ndugu wa uyo mchina upoje(serikali ya china) kesi inaweza zimwa au anaweza tafutwa masai yoyote akadondoshewa jumba bovu kumbuka watu wengi apa tz wamefungwa kwa kubambikiwa kesi na kumbuka wapelelez wetu hutumia sgasa,vitisho,lushwa kama muongozo wa upelez 80% huonevu hutumika 20% ukweli.haki,mazingira,medani,taaluma huleta majibu ya ukweli ya uchunguz au upelelez
 
Hawa wanajitoa Ufahamu hiyo ni kweli

Wamejaa masaki sanaa mpaka msasani na wanaaminika

Huyo aliyeua kama kweli ni masai lazima apatikane najua hiyo

Kama hapatikani huyo sio masai

Masai analinda geti analipwa 400k na anang'ombe kwao Mia mbili na hawazi

Kukuta masai anaua sio rahisi hizo ni takataka za arusha

Ni kweli. Sio rahisi Masai kuua.
Ila unaweza kuua mtu bila kukusudia yaani mwenyewe ukajikuta unashangaa.

Wengi wakiona wameua iwe kwa kukusudia au kutokukusudia kinachofuata ni kujihami maana mpaka ieleweke hujakusudia umesota vyakutosha
 
Ni kweli. Sio rahisi Masai kuua.
Ila unaweza kuua mtu bila kukusudia yaani mwenyewe ukajikuta unashangaa.

Wengi wakiona wameua iwe kwa kukusudia au kutokukusudia kinachofuata ni kujihami maana mpaka ieleweke hujakusudia umesota vyakutosha
Kina cha jeraha kina majibu tuwaache wataaluma wetu wapambane
 
Ukiwa nje ya mifumo intelligence sio rahisi kukunasa.
Ndio maana wahalifu bobevu Jambo la Kwanza wakishafanya tukio wanajitoa kwenye mifumo.

1. Mfumo wa ndoa.
Ukiwa mhalifu ukishakuwa na familia uwezekano wa kukamatwa upo kwa asilimia kadhaa.

2. Mfumo wa Social media na teknolojia
Kama mitandao ya simu, mitandao ya kijamii.

3. Mifumo ya Kidini.
Sijui muislam, sijui mkristo na unahuzuria Sana huko.

4. Mifumo ya siasa na ajira
Kama kuwa na vote id sijui NIDA

5. Mifumo ya elimu
Sijui ulisoma, msingi, secondary mpaka chip.
Hiyo mifumo inakutengenezea connection ambayo connection hiyohiyo ndio inatumika kukukamata.
Wahalifu wengi WA viwango vya juu. Kama walikuwa wakisoma wanakuwa hawana marafiki ni watu wakujitenga na kukaa pekeake.
Watu wa hivi ni ngumu kuwanasa.

Na mifumo mingine
Wengi wahalifu hawatumii mifumo hiyo
muhalifu hatumii facebook, instagram na mitandao mingine na hata kama ataamua kutumia atatumia anonymous ili asitambulike
 
Apa bongo akuna medan wala taaluma za upelelezi zaidi utasomwa upepo wa ndugu wa uyo mchina upoje(serikali ya china) kesi inaweza zimwa au anaweza tafutwa masai yoyote akadondoshewa jumba bovu kumbuka watu wengi apa tz wamefungwa kwa kubambikiwa kesi na kumbuka wapelelez wetu hutumia sgasa,vitisho,lushwa kama muongozo wa upelez 80% huonevu hutumika 20% ukweli.haki,mazingira,medani,taaluma huleta majibu ya ukweli ya uchunguz au upelelez

Hapana Mkuu.
Wapelelezi wapo usije kujichanganya.

Ukiona mambo yanaenda swege mnege ujue kesi imeshakuwa ngumu yaani ipo katika mazingira magumu.

Ila ukiua sasa hivi, ukaweza kujificha walau kwa Siku tatu mpaka Saba ujue wewe ni bingwa. Sio rahisi kujificha na kuikimbia serikali. Sio rahisi hata kidogo.
Labda usiwe na ID, utambulisho. Au ndani ya system wawepo wanaokuficha
 
Kesi za mauaji huwa zinachuku muda.

Labda uue mtu umfukie Sehemu na watu wasijue aliuawa na nani.

Lakini ukishajulikana umeua. Aiseeh kukimbia na kujificha ni ngumu Sana tena kama hauna pesa ndio kabisa.
Ukitoba Siku 7 hata Askari wenyewe watakupongeza
 
Back
Top Bottom