Mchina aliyepata "A" tisa NECTA

Mchina aliyepata "A" tisa NECTA

Ndio, with evidence
Si kweli, story za mtaani haswa zile za kwenye maeneo karibu na mafundi viatu, haiwezekani mwenye PHD akaweza akashindwa kuongea kingereza halafu mwenye degree moja ya economics tena ya mwaka 1975 akaweza kuongea kwa ufasaha kingereza, Watanzania tunao uwezo wa kuamini habari ya kijinga tukazifanya zikawa ndio za maana na zile zenye mantiki tukaziona ni za kijinga.
 
Si kitu cha kawaida jamani awe nani binadam wote Ni sasa hiii nayo Ni habari duuuh
 
Media na waandishi wa habari naona gumzo limekua mchina kushika nafasi ya pili na kupata B ya kiswahili, mbona mshindi wa kwanza hawamzungumzii au kwa kua yeye si mchina!?

Ulimbukeni huu jaman,mchina anapewa airtime sana kuliko mtanzania
Assume wewe ni muandishi wa habari na katika pita pita zako ukakutana na vijana wawili boda boda mmoja mbongo mwenzetu na mwingine mzungu , wote wako bize kuita abiria, yupi kwako atakuwa news?
 
ni kawaida ,mbona kuna wabongo wanapata A kiingereza? Alikaa darasan akawa na nidhamu na bidii ya kutosha akafaulu. Ni kawaida sana
 
View attachment 324142

Mara Nyingi Sana jina linaweza kuwa sababu ya wewe Kupenya ama Kukwama kwenye maisha. Baada ya matokeo ya Kidato cha Nne siku ya Jana Story kubwa ni Mchina aliye pata nafasi ya Pili kitaifa ambaye ni Mchina.

CongCong Wang ambaye amepata A tisa na B Moja Ya Kiswahili anasema Cong Maana yake ni Clever na Wang Maana yake ni King... So Jina lake lina maana Clever Clever King. Katika Mtihani wa Mock mkoa wa Dar alikuwa wa 2.

Alianza kusoma darasa la pili alipomaliza darasa la saba akaamua kuchagua NECTA badala ya Mfumo wa CAMBRIDGE sababu mfumo wa NECTA ni mgumu zaidi.

Kiswahili ni lugha yake ya 4 kujifunza anasikitika kupata B wakati MOCK alipata A.

Kati ya masomo aliyokuwa anafurahia zaidi ni somo la Historia ambalo mwalimu alikuwa anafundisha vizuri sana kama Movie.

Source: Clouds Media Group
Hii shule ina historia nzuri tangu ianzishwe,nimeona video ya huyu dada,anagonga swanglish vizuri hâta kushinda masista do wa tz....hongera zake
 
Si kweli, story za mtaani haswa zile za kwenye maeneo karibu na mafundi viatu, haiwezekani mwenye PHD akaweza akashindwa kuongea kingereza halafu mwenye degree moja ya economics tena ya mwaka 1975 akaweza kuongea kwa ufasaha kingereza, Watanzania tunao uwezo wa kuamini habari ya kijinga tukazifanya zikawa ndio za maana na zile zenye mantiki tukaziona ni za kijinga.
Tukupandishie video clip ujionee? Utafanya mjadala ugeuke bure hapa, kuna watu huwa hawaguswi humu na ukimgusa utaitwa Majina yote
 
Mimi nilisoma na binti mmoja wa kihindi anaitwa shazma Jeffer nakumbuka alikuwa anatuongoza darasani Hadi somo la kiswahili Ingawa aliingia hajui kiswahili,Kwa aliemaliza forest hill 1995 atakubaliana na mimi!
 
Tuacheni utani wachina ni wagumu sana kuelewa huyo mchina ni genius tu kazaliwa hivyo.. Mimi nimesoma na wachina nchi za nje ni vilaza hatari. Wao wataluburuza tu kwenye Hesabu basi ..
Hao wanaweza kubadili hata matokeo kisayansi maana hata wamarekani wamekubali.
 
Tukupandishie video clip ujionee? Utafanya mjadala ugeuke bure hapa, kuna watu huwa hawaguswi humu na ukimgusa utaitwa Majina yote
Video clip moja ambayo anaongea na mkandarasi?, mnayo video clip wakati anaidefend PHD yake?. Anazo video clips nyingi sana ambazo nyinyi kwa sababu ni watu one sided hamuwezi kuzionyesha. Nyinyi ndio mnaosema Makonda alimpiga mzee Warioba wakati sio kweli, nyinyi ndio mnaosema Makonda kamfunga kamba za viatu Ridhiwani wakati sio kweli. Nyinyi habari za kipuuzi ndio za maana kwenu, na yale ya maana mnayaona ujinga. Watanzania walipowapiga chini mwaka jana walitazama mbali sana. Hamuwezi mkamtumia Mr Zero kama mtu muhimukwenye kampeni halafu mkastahili kupewa nchi. Jipangeni kwa ajili ya 2020, huu ujinga wa kusema eti rais hajui kingereza upelekeni kwa watoto wa shule ya msingi.
 
Kusema ni Waafrika wangapi huongoza ni rahisi sana kila mtu anaweza kusema na ndiyo maana nikatoa changamoto kama yupo Mwafrika Diaspora aliongoza huko aliko nchi nzima mtaje, ni rahisi kivivyo tu!
Yaaah yupo mkenya aliesoma uingereza aerospace engineering na akawapiga chini wazungu wotee kwa kupata maksi za juu sanaa
 
Halafu mTz anapata F na kiswahili na anachukulia poa tu? The difference
 
Si kweli, story za mtaani haswa zile za kwenye maeneo karibu na mafundi viatu, haiwezekani mwenye PHD akaweza akashindwa kuongea kingereza halafu mwenye degree moja ya economics tena ya mwaka 1975 akaweza kuongea kwa ufasaha kingereza, Watanzania tunao uwezo wa kuamini habari ya kijinga tukazifanya zikawa ndio za maana na zile zenye mantiki tukaziona ni za kijinga.
Usibishe wewe, ni kweli kuna walimu wa vyuo vikuu hawako fluent kiingereza,
 
Back
Top Bottom