Mchina aliyepata "A" tisa NECTA

Mchina aliyepata "A" tisa NECTA

Nimemsikiliza yule Mwanafunzi mchina , wakati anahojiwa, lakini kiswahili anacho ongea si kiswahili sahihi sana japo anajitahidi sana na ninapenda kumpongeza kwa kuiweka Tanzania ktk Ramani ya Dunia.

Mfano nimesikia akisema " watoto mengi", "nilitumia masaa nyingi" napata wasiwasi sana kwenye mfumo wetu wa Elimu na kujiuliza maswali yasiyo na majibu pengine.

1. Inawezekana mitihani ya sasa ivi ni kama ya kuchagua huhitaji kujua kila kitu. Au ni udhaifu wa mitihani yetu kwa kuwa haina mtihani wa kuongea japo sidhani kama ni muhimu sana kuwa na mtihani wa "oral"

2. Inawezekana wasahihishaji waliamua kupotezea baadhi ya makosa ambayo hayana athari kwenye tafsiri iliyokusudiwa na mwandishi.

3. Watoto wa sasa ivi wavivu kusoma hadi kupelekea asiye kiwezea vizuri kiswahili akifanya bidii anakuwa bora kuliko wale wanao kijua vizuri.

Funzo kwa watz
Kumbe hata yale ambayo tunadhani hatuna maarifa ya kutosha tukiweka bidii tunaweza kushangaza Dunia.

Sina maana amependelewa. Naheshimu bidii yake na natambua kuwa ni mwanafunzi mwenye akili sana.
Mkuu una point japo watanzania wengi huwa sio wadadisi na wanaojiuliza mambo. Ni uvivu kwa kwenda mbele anacholetewa ndio hicho hicho. Udadisi ulio uonyesha kwenda maswali yako ni mzuri. Mimi mfumo wa mtahani wetu unatoa nafasi kwa wanaokariri kushinda. Lakini ni muhimu sana ukajua kwamba hizo shule nyingi unazoona zinapazisha kwa kiwango cha juu (hasa binafsi) pamoja na kufundisha vizuri lakini huwa ni wajanja wa ''kuonyesha'' wanafunzi mitihani ili shule zao zikubalike. Hili nalo ni jipu linalohitaji umakini wa hali ya juu sana kulitumbua kwani linafanyika kwa uficho sana.
 
Nimemsikiliza yule Mwanafunzi mchina , wakati anahojiwa, lakini kiswahili anacho ongea si kiswahili sahihi sana japo anajitahidi sana na ninapenda kumpongeza kwa kuiweka Tanzania ktk Ramani ya Dunia.

Mfano nimesikia akisema " watoto mengi", "nilitumia masaa nyingi" napata wasiwasi sana kwenye mfumo wetu wa Elimu na kujiuliza maswali yasiyo na majibu pengine.

1. Inawezekana mitihani ya sasa ivi ni kama ya kuchagua huhitaji kujua kila kitu. Au ni udhaifu wa mitihani yetu kwa kuwa haina mtihani wa kuongea japo sidhani kama ni muhimu sana kuwa na mtihani wa "oral"

2. Inawezekana wasahihishaji waliamua kupotezea baadhi ya makosa ambayo hayana athari kwenye tafsiri iliyokusudiwa na mwandishi.

3. Watoto wa sasa ivi wavivu kusoma hadi kupelekea asiye kiwezea vizuri kiswahili akifanya bidii anakuwa bora kuliko wale wanao kijua vizuri.

Funzo kwa watz
Kumbe hata yale ambayo tunadhani hatuna maarifa ya kutosha tukiweka bidii tunaweza kushangaza Dunia.

Sina maana amependelewa. Naheshimu bidii yake na natambua kuwa ni mwanafunzi mwenye akili sana.
Wakati tunaingia chuoni..kuna mzungu alifeli screening test ya English wakati sisi wengine tulipeta..sasa sioni haja ya kushangaa...
 
Tuhuma za fedha kutumika kuhonga wasimamizi na walinzi wakati wa mitihani, hasa kwenye shule binafsi, awamu hii ya utumbuaji majipu izifanyie kazi.
Hili lipo sana hasa baada ya shule za binafsi kuingia kwenye ushindani wa kuvutia wanafunzi ili kuwa na pato kubwa na zuri.
 
Mzungu/ Mmarekani mwenyewe kamshindwa Mchina, we ndio utamuweza? Unatengeneza iPhone yako ya milioni moja leo kesho Mchina anatoa kama hiyo hiyo kwa laki mbili... Hawa jamaa ni noumer...
 
Tanzania ya Jk na kiswahili kuwa lugha ya kufundishia hats vyuo vya elimu ya juu....big up Mkwere na BRN yako.
 
Mbona wabongo wanafumua A za kingereza, kifaransa na kiarabi hamshangai




Ndio maana nimekwambia tupo tofauti mkuu mimi watu walikuwa wanapiga kiswahili nilikuwa nawanaonea wivu sana maana kila nikikukuruka mbishi naishia kwenye C tu
 
Samahan wakuu...unawezaje ukaandika halafu ukashindwa kuongea??
Hilo swali waulize watu wote waliosoma combination za sayansi kama PCB,pcm hawa Kiukweli kwa kushuka tu ni hatare lakin mwambie aongee english ni mitihani,fanya utafiti utajua
 
Samahan wakuu...unawezaje ukaandika halafu ukashindwa kuongea??
Mkuu kiswahili cha kuandika huumizi kichwa ni kama kujua hisabati, sarufi, kivumishi, nomino na mzizi mkuu wa neno baaaas biashara imeisha. Wapo wazungu wanafeligi somo la english je wajua hlo pia wapo wabongo ndo mamasta katika kunfuu. Ukibisha muulize Mkoroshokigoli
 
Seriously?? Vp kihusu wanaijeria, wanajua kingereza lakini unaonaje matamshi yao?
hatuzungumzii lafudhi , tunazungumzia usahihi. nigeria wanaongea kingereza sahihi sema wana tatizo la lafudhi
 
Tuhuma za fedha kutumika kuhonga wasimamizi na walinzi wakati wa mitihani, hasa kwenye shule binafsi, awamu hii ya utumbuaji majipu izifanyie kazi.
Hii kitu naisi hâta FEDHA xuls inahusika,kwa anayejua jaman,atupe taarifa hapa
 
Wakati tunaingia chuoni..kuna mzungu alifeli screening test ya English wakati sisi wengine tulipeta..sasa sioni haja ya kushangaa...
Then hapa kazini tunafanya kazi na mkorea alikuja hajui kiswahili but alikuja na dictionary mbili moja ya ya kikorea to Swahili...so kila neno jipya analinukuu na tafsiri yake..sasa hv Amelia mswahili typically....sasa tujiulize ni wabongo wangap wakiendaga nchi za wenzetu wanaendaga na dictionary zao...ni juhudi binafsi zinazowafanya wafaulu ana kupenda kujifunza
 
ninachojua no kwamba izo shule mtihani wanapewa one week before as a test and baadae wanakuja kuufanya Sikh ya nekta amini usiamin.

Wakubwa ndo waandaji wa mitihani na Sikh ya modulation wanaenda walimu wao so wanajua mtihani utakuwaje.

nyie APA jf mnabwabwaja tu
 
Back
Top Bottom