Draft ni mchezo wa akili tu. Kuna formula (copy)nyingi tu. "Mguu wa jini, kilosa, five ball, kingi fala, na mingine. Mtu akikuwekea copy ya fiveball tayari yeye ana sare wewe utafute. Mguu wa jini ukiuingia hutoki. Kilosa huu mimi ndio naukubali, ni full msuli. Ukiuangalia unaona kila mtu ana nafasi ya kushinda. Ila mara nyingi aliyeanxa kucheza anashinda.
Hawa ndio mabingwa wa Tanzania.
1. Mangwelele. Huyu anapatikana buguruni.
2. Juma mchafu huyu hana kijiwe maalumu. Yeye kacheza draft dsm nzima kila kijiwe.
3. Ronaldo huyu yupo sinza nadhani palestina. Ni sheeder.
4. Godziller huyu maskani yake ifakara. Ila yeye anatembea mikoani. Hii ni kazi yake na inamwingizia kipato.
Note
Ili ijue draft ukubali mambo mawili.
1. Uwe mchafu kwa maana unashinda vijiwe vya draft huna muda wa kufua na kuoga.
2. Ukonde. Maana huna muda wa kula. Muda wooote unagonga kete tu.
Ref. Juma mchafu niliyemtaja hapo juu, jina lake ni juma. mchafu ni nick name yake. Na ni kweli ni mchafu. Hafui wala haogi.