Mchepuko wa Kikorea umeng'ang'ana nirudi nao Tz

Mchepuko wa Kikorea umeng'ang'ana nirudi nao Tz

Kuna mmbongo alikuwa jirani yetu miaka hiyo, alikwenda Urusi kusoma miaka 7. Alijaliwa kupata watoto 3 katika miaka hiyo 7. Alipomueleza mama yao kuwa ana mke nyumbani, yule mama alimumbia chukua wanao uondoke. Yule baba alimueleza mkewem akamuelewa, basi ilikua familia kumbwa mle ndani. Mama yao mmbongo aliwalea kwa upendo sana.
 
Mkuu mm nakushauri tulia kwanza mpaka utakapo maliza papers zenu then kaa nae mwambie ukweli wote koz hyo tayari ni mzazi mwenzako...baada ya hapo ndio mtajua cha kufanya bora uanze Huko kumaliza hiyo mishe kuliko kumleta huku na hata pia ukimtoroka unadhan Tanzania mbali kama mbinguni? Anaweza kuja huku kukutafuta tuu! May be kupitia Jina lako au ofisini. Cha msingi tulia Kwanza mwambie ukweli Ww Mwanaume bhana pambana kwanza ugenini Huko koz una mke tayari. Bora yy Huko kuna maisha mazur kuliko huku Tanzania usije wapa mzigo watoto wako baadae.
 
Nimelipenda hili wazo, nitalizingatia. Ila itabidi niache baadhi ya vitu vyangu ili asishitukie mapema.
Aaaaah! Utazingatiaje Mawazo tofauti!?? Nataka nikushauri mkuu, Mimi mwanaume mwenzako, na shida yako Ni yangu, Mimi mwenyewe nimedanganya kwa Mzungu, kabla sijakushauri nambie......Huyo Mkorea anajua kuwa Una Mtoto au Watoto???
 
Kama ni chai feki huulazimishwi kunywa.
Sawa lakini umetuwekea chai mezani bila sisi kujua ni chai ya samadi ya ngombe,bahati mbaya mimi nimemeza bila kujua na sasa tumbo langu linanguruma,halafu wewe unaniuliza eti sikulazimishwa,.,.,sasa huoni ni afadhali ningelazimishwa ningeshtukia lakini wewe umenitrick kitapeli ili niumwe tumbo.
 
Wewe naye!!! Sijui ndo kunogewa. Jaribu kumtafutia kijisababu uanze kumzoesha kukaa naye mbali...akikuudhi kidogo unakuwa mbogo haswa ikiwezekana unajidai umewamba hutaki mawasiliano naye kwanza. Kidogo kidogo ataanza kulegea mwenyewe. Ikishindikana basi nenda hata hadi huko Busan then mtoroke nenda Japan kwa meli...hakikisha mizigo ya mhimu umemwachia jamaa yako ili aje nayo. Hili saga solution ni kutoroka...Hata unaweza ukacancel ticket pia ukajifanya kutafuta kazi hapo korea...then baada ya muda unatoroka. Familia yako inahusika zaidi, huyo mtoto wa kikorea akikua atakuja kukutafuta, kama Barack Obama alivyofanya!!
Nimekusoma mkuu, nitachanganya na za kwangu.
 
Kuna mmbongo alikuwa jirani yetu miaka hiyo, alikwenda Urusi kusoma miaka 7. Alijaliwa kupata watoto 3 katika miaka hiyo 7. Alipomueleza mama yao kuwa ana mke nyumbani, yule mama alimumbia chukua wanao uondoke. Yule baba alimueleza mkewem akamuelewa, basi ilikua familia kumbwa mle ndani. Mama yao mmbongo aliwalea kwa upendo sana.
Angekuwa ameshajifungua si tatizo.
 
kosa kubwa ulilofanya ni kumpa yeye akakate tiketi,,,wenzako huwa hawaagi,,ungeendelea kuwa nae then ungemtoroka bila kujua siku unayoondoka, ukifika Tz unawasiliana nae kumweleza ukweli. nakushauri fanya juu chini badilisha tarehe ya safari ikiwezekana weka ya siku za karibu kabla ya tarehe ya mwanzo halafu mtoroke. ukifika huku utawasiliana nae kumwambia ukweli. Lazma ujue kwamba wa korea na wa japan ndio wanawake wanaoongoza duniani kote kwa uaminifu na kuwa na mapenzi ya kweli. nakushauri usimwambie ukweli kwamba umeoa kwasasa atakufanyia kitu kibaya sana. nimeshuhudia wengi wamefanyiwa mabaya. jitahidi toroka halaf umwambie ukweli ukiwa Tz
 
Naogopa kutoa maneno matamu kwani utajihisi mwenye haki, natumai we ni msomi wa ngazi ya masters na katatizo ulikonacho ni O level tena Div 5. Iyo n simultaneous equation solve bila four figure. Hakikisha no intersection. To make long story short.....njoo na mkorea Tz kaa nae kwa muda tafuta Dada wa ndan kabla ya kufika Tz na nyumba + thaman za ndan . Mkifika mnaendeleza maiaha then utariport kwa wife baadae na usimwambie chochote mpaka ujue hatma ya mkorea/mke mdogo. Ni game rahisi ukijitoa ufahamu vinginevo ....ndi ndi Ndiiindiii ndi
 
Aaaaah! Utazingatiaje Mawazo tofauti!?? Nataka nikushauri mkuu, Mimi mwanaume mwenzako, na shida yako Ni yangu, Mimi mwenyewe nimedanganya kwa Mzungu, kabla sijakushauri nambie......Huyo Mkorea anajua kuwa Una Mtoto au Watoto???
Hajui.
 
Kaka chonde chonde usije lopoka ukamwambia ukwel huyo mkorea.....hutorud Tz nakuambia, utafanyiwa zengwe hutosahau maishani mwako..kama una hela kata ticket mpya ya nyuma ya siku ulizotaka kuondoka, then nyanyuka kimia kimia...hayo ya mimba wale ni wazaz wake watarudiana tu kuwa familia.
Ukiona imebuma" fanya kama walivyoshaur wadau, njoo nae Tz bora ajue kila kitu uko hapa kwenu madhara ya kudhuliwa yanweza kuwa machache...japo anaweza nunua bastola pia ukapigwa ......
Mpangie nyumba arusha...mwambie ukwel...safiri kwenda kwako..kaa week moja...then mrudie utakuta akili imemtulia na atakuwa na jibu
 
Rafiki Kwa sasa upo ugenini na jinsi huyo binti alivyokupenda ukifanya kosa dogo litakalo sababisha maamuzi mabaya juu yake tambua kua hio familia inayokusubiri Tz inaweza isikuone so kua makini sana ktk nyakati hizi za mwisho isijekua yale ya Ng'oswe, nivyema ata ukaja nae na ayo mengine yakatokea ukiwa huku Ila c huko kk.
 
Wadau,

Nahitaji mchango wa mawazo yenu kama kichwa cha habari kinavyojieleza. Kisa chenyewe ni hivi mimi ni diaspora ambaye nipo Korea kimasomo tangu November 2014. Mwezi Juni 2016 nahitimu masomo. Nimeoa na tumebarikiwa kuwa na watoto wawili.

Nikiwa huku Korea ya Kusini nilianza mahusiano na mdada wa kikorea, ni mrembo ila si wa kutisha sana si unajua watu wa ukanda huu kinachowapendezesha ni rangi tu waliyonayo vinginevyo kama wangelipakwa rangi nyeusi hakuna atakaye watamani.

Mdada huyu anajiheshimu sana tulianza kuzoeana kama classmate tu. Alikuwa karibu sana na mimi mpaka tukaanza kuvuka mipaka na kuwa wapenzi. Kosa nililofanya ni kwamba sikuwahi kumweleza ukweli kuhusu hali yangu ya ndoa, yaani nilimdanganya kwamba mimi sijaoa.

Tulianza mahusiano kwa siri kwasababu ya kuhofia jamaa zake wasijue kuwa anamahusiano na ngozi nyeusi. Ilifika wakati usiri ukawa unashindikana maana tulikuwa tunaenda club pamoja na kurudi na kulala aidha sehemu ninayoishi au anayoishi yeye. Kuna wakati mama yake aliwahi kuja juu sana akasema kwamba niachane na bintiye vinginevyo ataliwasilisha swala hilo polisi na ninaweza kufutiwa visa ya kuishi Korea.

Tulishauriana na binti kuwa tuachane ili nisije nikaharibu future yule binti akadai yeye akadai hawezi kuachana na mimi kwasababu hajawahi mjua mwanamume mwingine zaidi yangu tangu azaliwe. Na swala la yeye na mama yake anasema hawezi fanya chochote kwasababu yeye ni mtu mzima anapaswa kufanya maamuzi yake bila kuingiliwa na mtu. Nilimsihi tuendelee kwa siri ili nisije nikaharibikiwa kimasomo.

Mwezi uliopita mdada kanimaliza kabisa kaniambia anaujazito wangu, nimechoka mpaka sasa anasisitiza kuwa tunarudi wote Tanzania. Mwanzo nilijua ni utani lakini mpaka nimejua kuwa hatanii. Kwasababu ya urahisi jana Jumatatu nilimtuma yeye aende kunikatia ticket ya ndege amerudi na ticketi mbili yangu na ya kwake tunayosafiri pamoja.

Nimeshikwa na mfadhaiko, nimejaribu kumwambia tu kwa busara kwamba yeye angebaki kwanza ili nikafanye maandalizi ya kumpokea maana mimi nilipotoka nilikabidhi nyumba niliyokuwa naishi hivyo kwenda mahali na mgeni sina mahali pa kufikia itakuwa si vizuri.

Yeye amesisitiza kuna shida gani nikatapo lala naye atalala hata kama kibarazani. Pia akasema hawezi kuendelea kuwepo Korea maana ndugu zake wanaweza hata kumwambia atoe ujauzito wangu na pia wanaweza kumtenga ni heri akaondoka akaenda kuishi na mtu anayempenda hata kama ni sehemu ya tabu.

Kuhusu pesa yeye anasema sio shida anakiasi cha fedha ambazo ukizibadili zinaweza kufikia hadi 150 m ambazo zilikuwa ni mirathi ya marehemu baba yake. Kiukweli mdada huyu amenisaidia sana kifedha. Sikuwahi kuwa na shida ya kifedha muda wote nikiwa Korea.

Hofu yangu ni nyumbani ambako mke na watoto wangu wananingojea kwa hamu, nimeshindwa hata kuwanunulia zawadi maana huyu mdada anajua kila kitu ninachofanya. Ndani kwangu ni kama kwake. Jana nilipanga nimwambie ukweli lakini nilipokuwa namtazama nikajua anaweza nivuruga mpaka nikashindhwa kufanya mitihani yangu ya mwisho. Pia nilimwonea huruma sana kwamba naye anaweza asifanye vizuri hiyo mitihani yake. Ananipenda sana mpaka namuonea huruma sijui nikimwangalia.

Nilikuwa nafikiri nimwache wakati narudi nikifika Doha wakati wa kubadili ndege nimchenge potelea mbali hata kama nitakula hasara ya ticket. Lakini nimejikuta naona hiyo itakuwa ni kazi bure maana mdada huyu anajua mpaka ninapofanya kazi anwani yangu ya Tz anazo hata akaunti namba ya benki yangu anayo mana kuna wakati nikiwa likizo Tz alishawahi kunitumia pesa kwenye akaunti zangu.

Mke wangu na wanangu wananisubiria kwa hamu sana, na wanadai niwapelekee zawadi japo natoa kisingizio kwamba nimebakiwa na fedha ya nauli tu. Cha ajabu wife akasema basi atanitumia kwa Western Union mana kuna vitu nilishawahi kuwapelekea ni vizuri sana na vilikuwa vinauzwa bei ya chini sana. Huku mrembo wa kikorea naye anahesabu siku zilizobakia ili aweze kuruka nami kuja Tz.

Msaada wa kutatua tatizo hilo wadau. Niko njia panda nampenda mke wangu nawapenda wanangu. Namhurumia Mkorea alivyojitoa kwangu.

Nawasilisha kwa ajili ya ushauri.
Mkuu hiï issue yako ni ndogo sana,
Njoo na Mkorea mpaka dar,nyumbani usiwaambie siku rasmi ya kurudi.
Chukua hotel na Mkorea kwa walau siku 2,then mkiwa katika mapumziko yaliyotukuka mwambie ukweli kwamba una mke na watoto wanakutegemea

Then mpe opption,kwamba mpange nyumba aishi kama mchepuko tena kwa siri kubwa, mpaka utakapo maliza kufile mambo yako na mkeo,mdanganye sheria za nchi haziruhusu kua nae kabla hujaachana na mkeo,otherwise nae anaweza kua matatizoni.

Option ya pili ni yeye kurudi korea.
Hope ataumia lakini lazima atachagua either option ya kwanza au ya pili.
 
Well, tambua huyo Mkorea Ana Damu yako tumboni, angekua Hana Mimba yako ungefikilia kumkimbia, so wazo la kumkimbia ondoa.

Huyo Mkorea Ana true love, kumbuka keshapoteza kila kitu kwa ajiri yako, ndugu mpaka marafiki, wewe ndo ndugu na rafiki yake.

Still bado Ni mwanamke Wako, mwambie wife umesogeza mbele siku ya kuondoka, Rudi naye na mpangie nyumba, mtoe mpeleke hata Mbuga ya wanyama, then umwambie ukweli kuwa Una mke, mwambie bado unamwitaji, na ndo maana ukakubari kurudi naye TZ, na blah blah za kutosha, majibu yake yatafanya ama ukamweleze ukweli wife au vipi, siku ambayo unaenda kwa wife iwe baada ya kujua uwamuzi wa Mkorea!

Usimkimbie coz Ana damu yako, usimkimbie coz ulishamkosanisha na ndugu zake!
 
Well said brother, baada ya mtihani kuna allowance ya wiki kama mbili hivi.
Swala la kujadiliana na huyu binti halitakiwi kabisa kwa sababu alionyesha dalili za kuwa makini ukimwambia nataka kwenda Shangani au Busan yeye anaweza kusema twende wote. Kwanza kwa muda aliokuwa nami amekata mawasiliano na ndugu jamaa na rafiki kampani yake ni mimi, hawezi akakaa siku nzima bila kuonana.
Aiseeee haya mapenzi toka nizaliwe niliyaona kwenye tamthilia ya ENDLESS LOVE PEKEE star tv....kumbe kwel yapo! Umependwa sana na hiki kiumbe bro ila sasa ndio hivyo....tumia akili sana hapa, huyu kujiua au kukua nje nje kwa kiwango hicho cha mapenzi
 
Back
Top Bottom