My God!! Moja, Kwa hivyo amefanya taratibu zote za visa nk kisirisiri, bila wewe kujua? Yaani tuseme barua ya mwaliko amepata wapi? Mwaliko wake unaonesha atafikia wapi? Pili, Tz anakuja kama nani? Maana unaposema anakufuata, anakufuata kama nani? Anakaa mpaka lini? Tiketi amenunua return au one way? Kwa nini? Maana kama analazimisha kuja kama unavyosema, then anakuja kama visitor tu, ambapo lazima awe na tarehe ya kurudi. In fact lazima awe na return ticket. Sidhani kama mtu anaweza kuamka na kuamua kununua tiketi, kisa umemtuma kwenda kununua tiketi yako. Funguka ili watu wakushauri zaidi